Hivi ndivyo Lowassa alishiriki Richmond

Hivi ndivyo Lowassa alishiriki Richmond

Mairo,

Je mnajua mchakato mzima wa uzabuni wa Serikali ulivyofanyika? Ukisoma hii taarifa, hakuna chochote kigeni ambacho ni cha kustaajabisha au usema kukiukwa kwa taratibu.

Suala la umeme ambalo lilileta Richmond lilitokana na kuhitajika kwa umeme wa dharura. Serikali kwa kupitia IMF/WB walikubaliana kuwa kwa kuwa hii ni emergency, zile protocal za ku-float tender kupitia zabuni na kadhalika ziachwe na kufanyike hiyo GNT.

Waziri Mkuu alipewa jukumu hili na Rasi na hakujichukulia uamuzi binafsi.

Kama mnakumbuka Kikwete alijitapa na kusema Richmond walipewa mkataba kutokana na kuwa na fees ndogo kuliko wengine, na ndipo tukahoji je mliangalia uwezo, lakini Serikali haikujibu.

Ukisoma hii habari, unaona ni mtiririko wa utekelezaji wa maamuzi ya Serikali na hakuna lolote lile.

Tena mbaya kuna TAHADHARI kijana wetu Eddo ametoa kuwa ikidhihirika yanayosemwa ni kweli, basi mkataba usitishwe na zaidi akasema itumike ile mbinu ya kutumia Letter of Credit kuwalipa hawa jamaa na si vingine!

Sasa kama mnajua L/C zinavyofanya kazi, mngejua kuwa Richmond walipaswa kuleta mitambo kwanza kabla ya kulipwa na kama wangeshindwa kuleta mitambo, wasingelipwa na mkataba ungekaa mguu pande!

Swali ni kwa nini Msabaha alikwenda kwa Meghji na Kikwete akiomba jama wapewe advance?

Ukisoma matendo ya Lowassa, hayana tofauti na ya Mramba au Yona ambao leo wanashitakiwa eti kwa uzembe ilhali kila walichokifanya kina Yona na Mramba kilikuwa na baraka za Serikali na kuchapwa kama agizo katika gazeti la Serikali.

Suala la kujiuliza tuhuma hizi za kusema alishiriki, je alishiriki kuhujumu au alishiriki kiutendaji kama alivyopewa jukumu hilo la kuhakikisha tunapata umeme wa haraka?

Mbona gazeti hili halichapi au kueleza jinsi Lowassa alivyokimbia Ikulu na kumwambia Rais wasitishe mkataba na Rais akakataa akasema anaogopa kesi London na tuendelee na mkataba ilhali ilishoaonekana kuwa Rochmond hawana uwezo?

Rev.Kishoka heshima mbele,

Ninaona hoja ya msingi hapa ambayo Mh.EL ataitumia kujisafisha.unless kama ni yeye aliyetoa maagizo ya maandishi kwa Mh.Msabaha kufukuzia advance Hazina tofauti na maelekezo yake mwenyewe ya awali ya kufungua Letter of Credit (LC).

Mpaka kwenye hatua ya kuagiza ifunguliwe LC naona Mh.Lowassa alikuwa sahihi sana,na kwa mazingira ya dharura ilikuwa ni sahihi kuwanyang'anya kazi TANESCO waliokuwa wanasuasua kufanya maamuzi.

Mhh! Nahisi EL ataponyoka kwenye hili la Richmond na hapo ndipo mbio zake za ikulu zitakapochukua kasi ya ajabu.Na hapo ndipo akina yakhe waliokuwa wanampiga vita watakapotafuta nchi ya kwenda kujificha.

Let's wait and see,sinema hii itakavyomalizikia. Je,Starring EL atauawa?
 
Wana JF,
Tokana na maada hii inaonesha wazi kwamba Lowasa hana kosa na alijiuzulu ili kuepusha mengi na makubwa zaidi.

Alipogundua kosa alimpa mkulu taarifa ili mkataba usitishwe, lakini mkulu alikataa kwa kuogopa kesi. Nani wa kulaumiwa kati ya hawa wawili?.
 
Wana JF,
Tokana na maada hii inaonesha wazi kwamba Lowasa hana kosa na alijiuzulu ili kuepusha mengi na makubwa zaidi.

Alipogundua kosa alimpa mkulu taarifa ili mkataba usitishwe, lakini mkulu alikataa kwa kuogopa kesi. Nani wa kulaumiwa kati ya hawa wawili?.
kwanini alifikia kufanya kosa? (ndio akamueleza Mkulu) kwanini hakumshauri raisi toka mwanzo njia bora ya kufuatilia suala hili?
Ukishirikiana na mwizi then ukashikwa, hutakiwi kutumia kinga ya mwingine kwenye suala lako. Sasa kama EL alishiriki, basi yeye ni mwizi tu, haina haja ya kusema baadae alimshauri mkulu kuvunja mkataba.
 
[QUOTE=Rev. Kishoka;629755]Mairo,

Mbona gazeti hili halichapi au kueleza jinsi Lowassa alivyokimbia Ikulu na kumwambia Rais wasitishe mkataba na Rais akakataa akasema anaogopa kesi London na tuendelee na mkataba ilhali ilishoaonekana kuwa Rochmond hawana uwezo?[/QUOTE]
hivi kwanini hakumshauri raisi kabla ya tukio? maana sioni busara yoyote ya kufanya kosa huku ukijua then useme alimshauri raisi tuvunje mkataba, unajua madhara ya kuvunja mkataba? nini maana ya kufanya evaluation kabla ya mkataba? si nikujua uezo wa huyo supplier etc na kupunguza kama sio kuondoa tatizo la mikataba tata?
 
Suala la kupatikana kwa umeme lilikuwa ni emmergency mpaka World bank na IMF waliona umuhimu huo na kukubaliana nalo ndiyo maana halikupata nafasi ya ku-flotishwa kwenye tenders kama ilivyo kawaida.

Alichofanya Lowasa ni kuona umeme unapatika kwa haraka na kwa gharama ndogo, ndiyo maana akawa anataka suala hilo liendeshwe haraka haraka. Yeye aliichagua Richmond kupewa kazi hiyo baada ya kupitia makabrasha mbali mbali mezani kwake yaliyoletwa na watendaji wake ambao ndiyo waliyoichagua na kuipendekeza Richmond kwa kigezo cha bei ndogo.

Kamati ya Mwakyembe kama ingelimuita Lowasa ili kupata maelezo kamili bila shaka wangeelewa kwanini Lowasa alifanya alichokifanya katika sakata zima la Richmond.

Lowasa ameonewa, hakupewa nafasi ya kujieleza. Katika hili suala Lowasa hana kosa. Mwakyembe na kamati yake wanatakiwa kuwa wakweli na bila kuwa na woga wowote, watupe ukweli na undani wa tatizo hili.

Lowasa ni kiongozi shupavu, asiye na woga wala haya, mwenye msimamo madhubuti, mfuatiliaji mzuri na mwenye uwezo wa kupambanua masula kiundani.
 
Suala la kupatikana kwa umeme lilikuwa ni emmergency mpaka World bank na IMF waliona umuhimu huo na kukubaliana nalo ndiyo maana halikupata nafasi ya ku-flotishwa kwenye tenders kama ilivyo kawaida.

Alichofanya Lowasa ni kuona umeme unapatika kwa haraka na kwa gharama ndogo, ndiyo maana akawa anataka suala hilo liendeshwe haraka haraka. Yeye aliichagua Richmond kupewa kazi hiyo baada ya kupitia makabrasha mbali mbali mezani kwake yaliyoletwa na watendaji wake ambao ndiyo waliyoichagua na kuipendekeza Richmond kwa kigezo cha bei ndogo.

Kamati ya Mwakyembe kama ingelimuita Lowasa ili kupata maelezo kamili bila shaka wangeelewa kwanini Lowasa alifanya alichokifanya katika sakata zima la Richmond.

Lowasa ameonewa, hakupewa nafasi ya kujieleza. Katika hili suala Lowasa hana kosa. Mwakyembe na kamati yake wanatakiwa kuwa wakweli na bila kuwa na woga wowote, watupe ukweli na undani wa tatizo hili.

Lowasa ni kiongozi shupavu, asiye na woga wala haya, mwenye msimamo madhubuti, mfuatiliaji mzuri na mwenye uwezo wa kupambanua masula kiundani.

Mkuu unatushangaza sana.World Bank na IMF ni nani hapa nchini?
Wenye nchi ndo thithi wenyewe, wasikilize hao jamaa at your own peril.
Mara kadhaa WB na IMF wamejulikana kuwa kichaka au a front for big multinational businesses.
Wanabadilika kama kinyonga hao,hawatakuja kumtetea sasa mzee EL.
EL Kujitetea or not, ukikamatwa na fundo la nyama mdomoni na ukalitema kabla ya kulimeza hakuondoi dhamira iliyokuwepo ya kuiba , mbaya zaidi kuiibia jamii ya Watanzania masikini waliokudhamini na kukuamini katika uongozi.
 
Aliyeandika makala hii akitegemea itaonesha ubaya wa EL kushiriki mchakato wa Rdc amechemsha. Makala inaonesha EL akiwa on top of his game. Ndiyo tatizo la kupigana vita wasiyojua adui ni nani. Oh well.
 
Tanzania tunahitaji kutumia nguvu..

Nguvu na uwezo uliotumika kumtoa Nduli IDD amin DADAA ndio vitumike ktk kuwatoa hawa nyoka wenye sumu kali katika maendeleo ya watanzania.

Umshini wam, mshini wam / Khawuleth'umshini wam
 
Kuna watu wanaotaka tuamini kuwa hakukuwa na mchakato wa tenda katika namna ya kumpata muuzaji wa mitambo ya kuzalisha umeme ambayo ilisababisha kupatikana kwa Richmond baadae. Nadhani kututaka tuamini hivyo ni kutufanya wote kuwa hatunazo. Kuna makampuni mengi ya kutosha ambayo yalipeleka bids zao na wakatupiliwa mbali, na Richmond akapewa tenda hiyo bila kufuata kanuni za manunuzi ya umma (PPRA). Na hapo ndipo kosa kubwa lilipoanza. Kwani wangemalizia taratibu kwa mujibu wa sheria ingewadhuru nini?

EL kama walivyo akina Msabaha, Nazir Karamagi na wengine, alihusika moja kwa moja kuvunja sheria za nchi na kuiingiza nchi kwenye hasara ambayo pia ilimsababishia kuachia ngazi ya u-PM. Kama angekuwa na imani kuwa alikuwa safi, na kuwa uamuzi aliouchukua ulikuwa ni wa lazima na wenye manufaa ya nchi, angeutetea kwa uwezo wake wote. Ila aliona ataumbuka, na hakujua njia ya kujiokoa kuepukana na kuumbuka huko. Ndio maana akakubali kung'oka katika wadhifa wake.

Hivi sasa amejipanga na yuko tayari kubadilisha mawazo ya watu bila kutumia mdomo wake. Angekuwa kweli yuko sahihi na hana kosa, angesimama hata wakati huu na kusema jinsi gani alivyotekeleza wajibu wa kuokoa nchi kutokana na tatizo la umeme, na ni ulazima gani uliosababisha kuchukua uamuzi aliouchukua katiak hatua zote za utekelezaji wa mkataba wa Richmond.

Haiwezekani akapitia mlango wa nyuma kujitetea. Kama mwanasiasa, asimame, aseme ukweli na aonyeshe kuwa kweli hakukuwa na njia nyingine. Hilo ninauhakika hawezi kulithibitisha. Na kadri anavyochelewa ndivyo inavyozidi kuwa ngumu kubadilisha imani ya watu. Wanaojaribu kumtetea waache unafiki. EL hawezi kushitakiwa kwa kuwa analindwa, basi hiyo na iwe bahati pekee aliyonayo.
 
Wana JF,
Tokana na maada hii inaonesha wazi kwamba Lowasa hana kosa na alijiuzulu ili kuepusha mengi na makubwa zaidi.

Alipogundua kosa alimpa mkulu taarifa ili mkataba usitishwe, lakini mkulu alikataa kwa kuogopa kesi. Nani wa kulaumiwa kati ya hawa wawili?.
...hakuna kati ya hao wawili anaye stahili lawama mkuu,ni SISI tulio wengi ndo wakujilaumu.
Tuliambiwa,hata kuonywa kwamba "hawatufai!!!"hawa.sasa tulimweka mmoja naye akampachika mwenziye,ndani ya miaka 5 jibu tunalo wenyewe!!
 
Mchungaji

Nakubaliana na reasoning yako.. logically ni sahihi kabisa kwa kuchangia zaidi labda tujibu maswali yafuatayo, sio kwa kumsafisha EL Lakini tu kuhakikisha haki inatendeka.

Nipashe wanaonyesha kusisitiza kuwa ofisi ya waziri mkuu ilihusika kila hatua: Hii sio ajabu kwa sababu ya unyeti wa suala lenyewe yani nchi iko gizani ni wazi ungetegemea waziri mkuu afuatilie kwa karibu, kama alivyosema mwenyewe kwenye barua anataka repoti kila siku bila kukosa- Hapo hana kosa kufuatiliwa kwa karibu ni wajibu wa Waziri mkuu na pia ni utekelezaji wa maagizo ya Rais kuhakikisha umeme unapatikana. Sasa angefuatilia nani kama sio Waziri mkuu.

Kukiukwa kwa taratibu za tenda: Hili pia lilisababishwa na unyeti wa suala lenyewe na sio lazima iwe ni ufisadi. na kubwa hapa ni kwamba IMF/Worl bank walijua,yaani haikuwa siri kuwa watafast track issue nzima ili umeme uje mapema.

Barua za Waziri mkuu: Waziri mkuu katika barua inayotajwa na nipashe anasema wazi Waziri Msabaha afuatilie na kama kuna mashaka basi atoe taarifa ili hatua zichukuliwe mara moja (nahisi ni pamoja na kuvunja mkataba ikibidi). kama ni kweli JK alikataa kwa kuogopa kesi kama mchungaji anavyosema mimi sijui, lakini hapa kwa barua ile ya kwenda kwa Msabaha kutoka kwa Waziri mkuu , naomba nimclear Lowasa kwa nini aliweka wazi kama kuna utata apewe taarifa hatua zichukuliwe.

Kwa kusema ukweli barua hizi zinamsafisha zaidi Lowasa kuliko kumkandamiza.Inawezekana Lowasa aliwaamini Richmond na wakamtapeli. Kwa hiyo Richmond ametapeli serikali , sasa kama kuibiwa ndio tumeibiwa wote sisi na Lowasa.. kwa hiyo tunaweza kumhukumu LA kwa uzembe wa kutapeliwa na Richmond , kwa kuwaamini Richmond lakini si kwa UFISADI,aliposema anajiuzulu kwa makosa ya kiutendaji nakubaliana nae, kwamba angekuwa makini zaidi asingewaamini RICHMOND kiasi kile.. na uzuri aliposhtuka kwamba sasa hawa jamaa ni wahuni aligeuka na akataka wachukuliwe hatua. katika suala hili kwa kusema ukweli .. ni haraka ndio iliponza.. na kama waswahili wasemavyo Hararka haraka haina baraka. Umakini ulikosekana.

Hatua zilizochukuliwa: Richmond wameshtakiwa mahakamani, na kama Gire sio mmiliki cha msingi abanwe ataje wamiliki .. vinginevyo jamani itakuwa ni kumwonea Waziri mkuu mstaaafu .. bila ushahidi.. tuweke jazba pembeni na tureason logically bila jazba.

Kosa la Lowasa katika sakata hili: kwa maoni yangu Lowasa alikosea kureact kwa jazba mara baada ya Mwakyembe kusoma report. Kuzira uwaziri mkuu haukuwa uamuzi kwa busara. Angeweza kuelezea ilivyokuwa akaleta na barua alizoandika na kueleza kwa nini aliamua kulivalia njuga suala hili kama alivyokuwa akifanya kwa masuala mengine na kwamba ile ni staili yake ya utendaji na kwamba waheshimiwa wabunge wasiwe na shaka ya yeye kuhusika kwa karibu kwani alikuwa akitekeleza majukumu ya kikazi kama alivyoagizwa na Raisi, kisha angeliachia bunge liamue. Alikosea kuleta jaza na kujiweka kwenye Victim position na yeye kuanza kublame na kucomplain... badala ya kuweka facts mezani na kuacha wabunge wachambue. Ninaamini bunge lingegawanyika na labda kumsamehe au kumwajibisha kwa uzembe na kisha kuigiza serikali imkamate mmiliki wa Richmond achukule hatua kwa kutapeli .. Lowasa angekuwa bado Waziri mkuu hadi leo ... Hasira hasara.. naomba tujadili kwa hoja tafadhali bila jazba.. kwani ukiwa na jazba uwezo wa kureason vitu unapungua na unaanza kuapply logical falacies kibao.. mwenye ushahidi na mwazo tofauti tuendelee kujadili....Na kwa taarifa mimi sio fisadi wala mwanamtandao ni mchambuzi tu wa mambo.. manake watu wengine wanaweza kuja na majibu mafupi na kusema .. ahah wale wale mafisadi hao ... mmmmmh hapana leta hoja mezani.. nawakilisha.
 
Mkuu unatushangaza sana.World Bank na IMF ni nani hapa nchini?
Wenye nchi ndo thithi wenyewe, wasikilize hao jamaa at your own peril.
Mara kadhaa WB na IMF wamejulikana kuwa kichaka au a front for big multinational businesses.
Wanabadilika kama kinyonga hao,hawatakuja kumtetea sasa mzee EL.
EL Kujitetea or not, ukikamatwa na fundo la nyama mdomoni na ukalitema kabla ya kulimeza hakuondoi dhamira iliyokuwepo ya kuiba , mbaya zaidi kuiibia jamii ya Watanzania masikini waliokudhamini na kukuamini katika uongozi.

Lole wa Gwakisa,

Serikali ilibidi iombe pesa kwa wahisani kuhusiana na suala hili la umeme wa dharura. Pesa ambazo tulisamehewa kulipia madeni na IMF/WB ndio tulizoruhusiwa kuzitumia kuingia mkataba huu.

Kwa upande mmoja, kwa kuwa hiyo psa ilishapangiwa matumizi, kilichofanyika Serikalini ni kile cha mazoea cha kutokujali tena alimradi fedha hii si yetu ni ya mhisani.

IMF/WB walisema badala ya sisi kulipa riba na mkopo, hiyo pesa tuipeleke kwenye umeme wa dharura!

Sasa kama unadai IMF/WB ni nani, mbona huulizi kuhusu zile sera za ERP, Ubinafsishaji na nyingine nyingi ambazo IMF/WB na donor countries wameilazimisha Serikali yetu ifuate wanachotaka?

Je unafikiri Mkapa kutamba sisi kusamehewa madeni Paris Club ili kuwa ni kutokana na Good Governance au kuongezeka uzalishaji? Jibu ni nope, nil, zilch big no na hapana.

Jibu la sisi kusamehewa madeni na Paris Club wakati wa Mkapa ni kuuzwa kwa NMB, Sheria mpya ya madini 1998, kubinafsishwa holela kwa mashirika na kuuzwa kwa bei chee huku tukitii amri za wakubwa.

Kama tulikuwa na ujasiri na uzalendo wa kukataa kushinikizwa na IMF/WB kama tulivyofanya wakati wa IPTL, tusingeuza basi hayo mashirika yetu ambayo mengine yalikuwa hayana matatizo yeyote!
 
Lukule2009,
Hivi kwa nini Wadanganyika siku zote hutafuta mchawi mwingine hata kama ukweli ni wazi kabisa.. Mkuu nakuomba uniwekee hapa sheria za ununuzi zinavyosema na imekuwaje Lowassa asisitize tender wapewe Richmond..Kama ni shida hata sasa hivi tunayo mbona simsikii Pinda akilazimisha kitu chochote! na tena mmefikia kusema kwa nini Waziri wa Nishati haku suggest kuwashwa kwa mitambo ya IPTL isipokuwa ushauri umetoka kwa Zitto..

Ikiwa serikali imeshapitisha tender zitolewe haiwezekani kabisa mtu mmoja atoe amri ya nani akubaliwe licha ya hivyo inaonyesha wazi Lowassa alimjua mwenye mali hiyo (meaning (Mohammed Gire), jambo ambalo linazidi kumfunga zaidi kisha inaonyesha pia alikuwa mbioni kuwatoa timu Aggreko kama mpango wa kwanza ungefanikiwa wakati hao Agreeko wana uzoefu na walikuwa wakifua umeme pasipo matatizo, leo uje kuwaondoa na kumweka mtu ambaye hana hata waya acha mbali mitambo na bado ilikuwa haijafika nchini.

Haya maneno ya Kikwete ati ndiye alikataa ni mazungumzo baada ya habari, tabia halisi ya mdanganyika...tunaweza sema hata Kikwete alihusika na mkataba wa Buzwagi, Kikwete alihusika na wizi wa EPA, kikwete alihusika na kila kitu kwa sababu yeye ndiye mkuu wa Kaya..
Lakini wakuu zangu ni muhimu sana tunapopanga mashataka ni lazima tufahamu pia majukumu ya wahusika na ndio maana halisi ya maneno Responsible and Accountable..someone has to be nasio kila mtu aliyeko juu basi tuwahukumu.. Imekuwa utawala wa Wagagagigikoko!
 
Mairo,

Je mnajua mchakato mzima wa uzabuni wa Serikali ulivyofanyika? Ukisoma hii taarifa, hakuna chochote kigeni ambacho ni cha kustaajabisha au usema kukiukwa kwa taratibu.

Suala la umeme ambalo lilileta Richmond lilitokana na kuhitajika kwa umeme wa dharura. Serikali kwa kupitia IMF/WB walikubaliana kuwa kwa kuwa hii ni emergency, zile protocal za ku-float tender kupitia zabuni na kadhalika ziachwe na kufanyike hiyo GNT.

Waziri Mkuu alipewa jukumu hili na Rasi na hakujichukulia uamuzi binafsi.

Kama mnakumbuka Kikwete alijitapa na kusema Richmond walipewa mkataba kutokana na kuwa na fees ndogo kuliko wengine, na ndipo tukahoji je mliangalia uwezo, lakini Serikali haikujibu.

Ukisoma hii habari, unaona ni mtiririko wa utekelezaji wa maamuzi ya Serikali na hakuna lolote lile.

Tena mbaya kuna TAHADHARI kijana wetu Eddo ametoa kuwa ikidhihirika yanayosemwa ni kweli, basi mkataba usitishwe na zaidi akasema itumike ile mbinu ya kutumia Letter of Credit kuwalipa hawa jamaa na si vingine!

Sasa kama mnajua L/C zinavyofanya kazi, mngejua kuwa Richmond walipaswa kuleta mitambo kwanza kabla ya kulipwa na kama wangeshindwa kuleta mitambo, wasingelipwa na mkataba ungekaa mguu pande!

Swali ni kwa nini Msabaha alikwenda kwa Meghji na Kikwete akiomba jama wapewe advance?

Ukisoma matendo ya Lowassa, hayana tofauti na ya Mramba au Yona ambao leo wanashitakiwa eti kwa uzembe ilhali kila walichokifanya kina Yona na Mramba kilikuwa na baraka za Serikali na kuchapwa kama agizo katika gazeti la Serikali.

Suala la kujiuliza tuhuma hizi za kusema alishiriki, je alishiriki kuhujumu au alishiriki kiutendaji kama alivyopewa jukumu hilo la kuhakikisha tunapata umeme wa haraka?

Mbona gazeti hili halichapi au kueleza jinsi Lowassa alivyokimbia Ikulu na kumwambia Rais wasitishe mkataba na Rais akakataa akasema anaogopa kesi London na tuendelee na mkataba ilhali ilishoaonekana kuwa Rochmond hawana uwezo?

Mchungaji

Nakubaliana na reasoning yako.. logically ni sahihi kabisa kwa kuchangia zaidi labda tujibu maswali yafuatayo, sio kwa kumsafisha EL Lakini tu kuhakikisha haki inatendeka.

Nipashe wanaonyesha kusisitiza kuwa ofisi ya waziri mkuu ilihusika kila hatua: Hii sio ajabu kwa sababu ya unyeti wa suala lenyewe yani nchi iko gizani ni wazi ungetegemea waziri mkuu afuatilie kwa karibu, kama alivyosema mwenyewe kwenye barua anataka repoti kila siku bila kukosa- Hapo hana kosa kufuatiliwa kwa karibu ni wajibu wa Waziri mkuu na pia ni utekelezaji wa maagizo ya Rais kuhakikisha umeme unapatikana. Sasa angefuatilia nani kama sio Waziri mkuu.

Kukiukwa kwa taratibu za tenda: Hili pia lilisababishwa na unyeti wa suala lenyewe na sio lazima iwe ni ufisadi. na kubwa hapa ni kwamba IMF/Worl bank walijua,yaani haikuwa siri kuwa watafast track issue nzima ili umeme uje mapema.

Barua za Waziri mkuu: Waziri mkuu katika barua inayotajwa na nipashe anasema wazi Waziri Msabaha afuatilie na kama kuna mashaka basi atoe taarifa ili hatua zichukuliwe mara moja (nahisi ni pamoja na kuvunja mkataba ikibidi). kama ni kweli JK alikataa kwa kuogopa kesi kama mchungaji anavyosema mimi sijui, lakini hapa kwa barua ile ya kwenda kwa Msabaha kutoka kwa Waziri mkuu , naomba nimclear Lowasa kwa nini aliweka wazi kama kuna utata apewe taarifa hatua zichukuliwe.

Kwa kusema ukweli barua hizi zinamsafisha zaidi Lowasa kuliko kumkandamiza.Inawezekana Lowasa aliwaamini Richmond na wakamtapeli. Kwa hiyo Richmond ametapeli serikali , sasa kama kuibiwa ndio tumeibiwa wote sisi na Lowasa.. kwa hiyo tunaweza kumhukumu LA kwa uzembe wa kutapeliwa na Richmond , kwa kuwaamini Richmond lakini si kwa UFISADI,aliposema anajiuzulu kwa makosa ya kiutendaji nakubaliana nae, kwamba angekuwa makini zaidi asingewaamini RICHMOND kiasi kile.. na uzuri aliposhtuka kwamba sasa hawa jamaa ni wahuni aligeuka na akataka wachukuliwe hatua. katika suala hili kwa kusema ukweli .. ni haraka ndio iliponza.. na kama waswahili wasemavyo Hararka haraka haina baraka. Umakini ulikosekana.

Hatua zilizochukuliwa: Richmond wameshtakiwa mahakamani, na kama Gire sio mmiliki cha msingi abanwe ataje wamiliki .. vinginevyo jamani itakuwa ni kumwonea Waziri mkuu mstaaafu .. bila ushahidi.. tuweke jazba pembeni na tureason logically bila jazba.

Kosa la Lowasa katika sakata hili: kwa maoni yangu Lowasa alikosea kureact kwa jazba mara baada ya Mwakyembe kusoma report. Kuzira uwaziri mkuu haukuwa uamuzi kwa busara. Angeweza kuelezea ilivyokuwa akaleta na barua alizoandika na kueleza kwa nini aliamua kulivalia njuga suala hili kama alivyokuwa akifanya kwa masuala mengine na kwamba ile ni staili yake ya utendaji na kwamba waheshimiwa wabunge wasiwe na shaka ya yeye kuhusika kwa karibu kwani alikuwa akitekeleza majukumu ya kikazi kama alivyoagizwa na Raisi, kisha angeliachia bunge liamue. Alikosea kuleta jaza na kujiweka kwenye Victim position na yeye kuanza kublame na kucomplain... badala ya kuweka facts mezani na kuacha wabunge wachambue. Ninaamini bunge lingegawanyika na labda kumsamehe au kumwajibisha kwa uzembe na kisha kuigiza serikali imkamate mmiliki wa Richmond achukule hatua kwa kutapeli .. Lowasa angekuwa bado Waziri mkuu hadi leo ... Hasira hasara.. naomba tujadili kwa hoja tafadhali bila jazba.. kwani ukiwa na jazba uwezo wa kureason vitu unapungua na unaanza kuapply logical falacies kibao.. mwenye ushahidi na mwazo tofauti tuendelee kujadili....Na kwa taarifa mimi sio fisadi wala mwanamtandao ni mchambuzi tu wa mambo.. manake watu wengine wanaweza kuja na majibu mafupi na kusema .. ahah wale wale mafisadi hao ... mmmmmh hapana leta hoja mezani.. nawakilisha.
Ukiwa hujui taratibu za manunuzi na due deligence utajibu kama ulivyo jibu, lakini ukiwa unajua utapingana na majibu ya lowasa.
kwanza unatakiwa ujue kwanini kunafanyika due deligence, hii inafanyika ilikuepuka kupata mkandarasi asiye faa, iwe mkurugenzi wake au hiyo kampuni, na hivi vitu vipo, sio kwamba mimi ninatunga leo, pili mkandarasi kutakiwa kutoa mahesabu yalio kaguliwa, bank statement, wasifu wake kwa kazi alizokwisha fanya etc etc, sasa hili lilifanyika kwa ufanisi? nini yalikuwa mapendekezo ya wataalamu kuhusiana na hili?
Humu JF watu na kwenye magazeti yaliisha anza minongono, Gire nk wakatupa web site na kudai wameweka bomba la mafuta Costa rica etc etc, lakini licha ya huo uongo wao watu waliliona hilo, tena wasio kuwa na resource, je serikali inayo ongozwa na waziri mkuu walishindwa kuliona hilo?
Nini matumizi ya balozi zetu zilizo nje ya nchi? si ni kuisaidia serikali kwa shughuli zilizo nje ya nchi?
Nini matumizi ya AG office ikiwa mshauri mwenyewe wa sheria naye haisaidi serikali.
Jingine unatakiwa ujue wajibu wa kazi za waziri mkuu, nazo ni kumsaidia Raisi, sasa hapa nitakupa mfano aliotoa Warioba , kwamba nyerere alitaka kumchagua kiongozi aliyehukumiwa kwa sheria za uchaguzi, warioba akmwambia mzee utakuwa unavunja katiba, nyerere akawa mbishi kidogo, lakini warioba alikwenda kwa waziri mkuu Sokoinne akampiga shule akaelewa, kesho yake warioba na sokoinne walienda kwa mwalimu, mwalimu nae akasema unajua jana sikulala, nilikuwa nafikiria lile jambo, pia unatakiwa uelewe kwanini nyerere alimlaumu malecela waziri mkuu na makamu wa Raisi? na kolimba katibu wa ccm, raisi Alhaji Ali na mwenyekiti wa CCm, sababu alivyo taka kuingiza mchi OIC, hawa jamaa kwa sababu zao mwenyewe walishindwa kumwambia au kumshauri Raisi na Mwenyekiti wao kwamba hiyo itakuwa ni kinyume cha katiba yetu na Sera ya Chama.
Sasa kwa hili hata kama Raisi alitaka iwe hivyo waziri mkuu alikuwa anatakiwa kulisisitizia hayo mapungufu ambayo aliyaona kama mtu mwerevu angeamua hakubalina na hili kwa maandishi au kwa kujiuzulu, lakini kuonyesha kwamba ni kiongozi dhaifu, hakufanya hivyo , bali nae akashiriki kuingia mkataba tata.
Zaidi ya hapo richmond alianza kusua sua kuleta mitambo kwa kukosa mtaji, na minongono ilikuwepo, sasa hapa ilikuwa ni wakati muuafaka wa kuvunja mkataba for non delivery as per agreement, badala yake wakaridhia kuwauzia huo mkataba Dowans.
 
Aliyeandika makala hii akitegemea itaonesha ubaya wa EL kushiriki mchakato wa Rdc amechemsha. Makala inaonesha EL akiwa on top of his game. Ndiyo tatizo la kupigana vita wasiyojua adui ni nani. Oh well.

Mzee Mwanakijiji dont take waTanzania for granted!
They know the right side of the coin.
EL may be, but only a piece in the whole game .
No wonder he has lasted for so long!
 
Lole wa Gwakisa,

Serikali ilibidi iombe pesa kwa wahisani kuhusiana na suala hili la umeme wa dharura. Pesa ambazo tulisamehewa kulipia madeni na IMF/WB ndio tulizoruhusiwa kuzitumia kuingia mkataba huu.

Kwa upande mmoja, kwa kuwa hiyo psa ilishapangiwa matumizi, kilichofanyika Serikalini ni kile cha mazoea cha kutokujali tena alimradi fedha hii si yetu ni ya mhisani.

IMF/WB walisema badala ya sisi kulipa riba na mkopo, hiyo pesa tuipeleke kwenye umeme wa dharura!

Sasa kama unadai IMF/WB ni nani, mbona huulizi kuhusu zile sera za ERP, Ubinafsishaji na nyingine nyingi ambazo IMF/WB na donor countries wameilazimisha Serikali yetu ifuate wanachotaka?

Je unafikiri Mkapa kutamba sisi kusamehewa madeni Paris Club ili kuwa ni kutokana na Good Governance au kuongezeka uzalishaji? Jibu ni nope, nil, zilch big no na hapana.

Jibu la sisi kusamehewa madeni na Paris Club wakati wa Mkapa ni kuuzwa kwa NMB, Sheria mpya ya madini 1998, kubinafsishwa holela kwa mashirika na kuuzwa kwa bei chee huku tukitii amri za wakubwa.

Kama tulikuwa na ujasiri na uzalendo wa kukataa kushinikizwa na IMF/WB kama tulivyofanya wakati wa IPTL, tusingeuza basi hayo mashirika yetu ambayo mengine yalikuwa hayana matatizo yeyote!

Mkuu Rev Kishoka , kwa mara ya kwanza katika wiki hii nakubaliana na wewe.
WB na IMF bado ni kichaka cha matapeli wa kimataifa.Wachangiaji wakuu wa mashirika hayo wanafahamika.
Pressure groups zinazoelekeza matumizi ya pesa zao vile vile zinafahamika.
Ni ndoto ya alinacha kutegemea kuwa tunaweza kuneemeka kwa mikopo ya hawa wakubwa sisi tukilala usingizi.
Hata hivyo matumizi ya fedha za mkopo toka IMF/WB kwa ajili ya umeme wa dharura bado ni deni ambalo watoto wetu watalilipa kwa kukabwa koo.
Hili haliondoi uwajibikaji wa viongozi wetu kwa wananchi wa Tanzania.
Matumizi mabaya ya mkopo, utakaolipwa kwa kodi zetu ni sawa na kuhujumu mapato yetu ya baadaye na kutuweka katika utumwa wa madeni.
Haya ndiyo makosa aliyofanya "mwenzetu" EL.
Yeye aliweka tamaa yake mbele na kusajili kunufaika kwake kabla ya maslahi ya wa Tanzania.
 
Mairo,

Je mnajua mchakato mzima wa uzabuni wa Serikali ulivyofanyika? Ukisoma hii taarifa, hakuna chochote kigeni ambacho ni cha kustaajabisha au usema kukiukwa kwa taratibu.

Suala la umeme ambalo lilileta Richmond lilitokana na kuhitajika kwa umeme wa dharura. Serikali kwa kupitia IMF/WB walikubaliana kuwa kwa kuwa hii ni emergency, zile protocal za ku-float tender kupitia zabuni na kadhalika ziachwe na kufanyike hiyo GNT.

Waziri Mkuu alipewa jukumu hili na Rasi na hakujichukulia uamuzi binafsi.

Kama mnakumbuka Kikwete alijitapa na kusema Richmond walipewa mkataba kutokana na kuwa na fees ndogo kuliko wengine, na ndipo tukahoji je mliangalia uwezo, lakini Serikali haikujibu.

Ukisoma hii habari, unaona ni mtiririko wa utekelezaji wa maamuzi ya Serikali na hakuna lolote lile.

Tena mbaya kuna TAHADHARI kijana wetu Eddo ametoa kuwa ikidhihirika yanayosemwa ni kweli, basi mkataba usitishwe na zaidi akasema itumike ile mbinu ya kutumia Letter of Credit kuwalipa hawa jamaa na si vingine!

Sasa kama mnajua L/C zinavyofanya kazi, mngejua kuwa Richmond walipaswa kuleta mitambo kwanza kabla ya kulipwa na kama wangeshindwa kuleta mitambo, wasingelipwa na mkataba ungekaa mguu pande!

Swali ni kwa nini Msabaha alikwenda kwa Meghji na Kikwete akiomba jama wapewe advance?

Ukisoma matendo ya Lowassa, hayana tofauti na ya Mramba au Yona ambao leo wanashitakiwa eti kwa uzembe ilhali kila walichokifanya kina Yona na Mramba kilikuwa na baraka za Serikali na kuchapwa kama agizo katika gazeti la Serikali.

Suala la kujiuliza tuhuma hizi za kusema alishiriki, je alishiriki kuhujumu au alishiriki kiutendaji kama alivyopewa jukumu hilo la kuhakikisha tunapata umeme wa haraka?

Mbona gazeti hili halichapi au kueleza jinsi Lowassa alivyokimbia Ikulu na kumwambia Rais wasitishe mkataba na Rais akakataa akasema anaogopa kesi London na tuendelee na mkataba ilhali ilishoaonekana kuwa Rochmond hawana uwezo?
Mkuu wangu kila siku unakuja na mambo jambo..
Hii habari ya kumsafisha Lowassa umeianza lini?.. maanake ktk mada nyingine unamwonyesha Lowassa kama ni mtu wa maamuzi mazito, anaweza fanya vitu ambavyo rais JK wala kiongozi mwingine yeyote hawezi..Lakini tulipokuja hapa, unaonyesha wazi Lowassa ni mnyonge, mtu anayefuata amri ya JK, kaonewa wakati sii kweli kabisa kwa watu wanaomfahamu Lowassa na hata maamuzi mengi alokwisha yafanya kabla ya hili..
Na sidhani hata zile mvua za kisayansi aliambiwa na JK maanake huyu mtu hawezi fanya makosa kama hayo.
Huyu Huyu Lowassa alifukuza mashirika kama Citywater na kusema kama wakishtaki wakashtaki, huyu Lowassa alifukuza watu kazi hata kabla ya kupewa report ya sababu za matukio wala kuachia vyombo vya usalama wafanye kazi yao.. kafukuza mtu kazi ktk shirika binafsi wakati jengo la ghorofa lilipoanguka bila kusubiri uchunguzi..
Labda niongezee ziadi... ndiye aliyemfungia Dimond Remtulia mwenye kiwanda cha sangara Mwanza kwa kushiriki ktk sinema ile, ndiye aliyetoa amri kuwekwa ndani Raphael Wagara (mlinzi wa kiwanda hicho) na hata mwandishi wa habari Cleopa Kaijage ambaye hadi leo hii sijui hatma yake. Na hakuna mdanganyika hata mmoja alosimama kuwalinda watu hawa..

Kila sifa mbovu ya Uongozi na ubabe alikuwa nayo Lowassa, leo anavikwa taji na kuonekana mtu mmoja alosingiziwa.. Ukisoma habari hii kwa makini na ukairudia ile ya Mwakyembe utaelewa vizuri zaidi ya ya kudandia bus..
Kwa taarifa zenu Kikwete yuko karibu sana na Msabah kuliko Lowassa mwenyewe na nina hakika JK angetaka Richmond waingie nchini hakuwa na haja ya kupitia kwa Lowassa hata kidogo kwanza sii kazi yake. Pili Kikwete asingeruhusu uchunguzi wa Richmond, hiyo kama ti isingeundwa haytta kidogo..nitarudia kusema Kikwete anaweza kuwa mjinga lakini sii Mjinga hivyo babu!
Tunaporudi kuhoji kwa nini Msabah na Meghji walikwenda omba fedha kwa JK, sijui kama tumejiuliza pia kwa nini viongozi wote waliochaguliwa na Lowassa walikwenda apishwa na JK..

Jamani Lowassa was a PRIME MINISTER! hivi kweli mnasahau nguvu ya Waziri mkuu kama alivyokuwa Sokoine!
 
Mairo,

Je mnajua mchakato mzima wa uzabuni wa Serikali ulivyofanyika? Ukisoma hii taarifa, hakuna chochote kigeni ambacho ni cha kustaajabisha au usema kukiukwa kwa taratibu.

Suala la umeme ambalo lilileta Richmond lilitokana na kuhitajika kwa umeme wa dharura. Serikali kwa kupitia IMF/WB walikubaliana kuwa kwa kuwa hii ni emergency, zile protocal za ku-float tender kupitia zabuni na kadhalika ziachwe na kufanyike hiyo GNT.

Waziri Mkuu alipewa jukumu hili na Rasi na hakujichukulia uamuzi binafsi.

Kama mnakumbuka Kikwete alijitapa na kusema Richmond walipewa mkataba kutokana na kuwa na fees ndogo kuliko wengine, na ndipo tukahoji je mliangalia uwezo, lakini Serikali haikujibu.

Ukisoma hii habari, unaona ni mtiririko wa utekelezaji wa maamuzi ya Serikali na hakuna lolote lile.

Tena mbaya kuna TAHADHARI kijana wetu Eddo ametoa kuwa ikidhihirika yanayosemwa ni kweli, basi mkataba usitishwe na zaidi akasema itumike ile mbinu ya kutumia Letter of Credit kuwalipa hawa jamaa na si vingine!

Sasa kama mnajua L/C zinavyofanya kazi, mngejua kuwa Richmond walipaswa kuleta mitambo kwanza kabla ya kulipwa na kama wangeshindwa kuleta mitambo, wasingelipwa na mkataba ungekaa mguu pande!

Swali ni kwa nini Msabaha alikwenda kwa Meghji na Kikwete akiomba jama wapewe advance?

Ukisoma matendo ya Lowassa, hayana tofauti na ya Mramba au Yona ambao leo wanashitakiwa eti kwa uzembe ilhali kila walichokifanya kina Yona na Mramba kilikuwa na baraka za Serikali na kuchapwa kama agizo katika gazeti la Serikali.

Suala la kujiuliza tuhuma hizi za kusema alishiriki, je alishiriki kuhujumu au alishiriki kiutendaji kama alivyopewa jukumu hilo la kuhakikisha tunapata umeme wa haraka?

Mbona gazeti hili halichapi au kueleza jinsi Lowassa alivyokimbia Ikulu na kumwambia Rais wasitishe mkataba na Rais akakataa akasema anaogopa kesi London na tuendelee na mkataba ilhali ilishoaonekana kuwa Rochmond hawana uwezo?

- Naona kuna watu humu mmekamia sana kumsafisha Lowassa kwa udi na uvumba, lakini tunawaambieni kwamba we know better, kwamba Lowassa ndiye aliyekua kiongozi wa wizi wa Richimonduli. Ni Lowassa ndiye aliyevunja kanuni za serikali na zabuni kwa kuingilia kati utafutaji wa zabuni kwa kuwamuru wajumbe wa ile kamati kujadili kampuni moja tu ya Richimonduli, badala ya zingine zote zilizoomba tenda.

- Lowassa ndiye aliyemtuma bangusile, awazuie wanakamati ya zabuni wasiende Texas, kuangalia kwa macho yao Richimonduli na ofisi zake zilipo, mkuu ninazo documents zote nilizopewa na mshiriki mmoja wa kamati, ambaye nilimuonya mapema kwamba he was about to be taken down as a sacrifice ili akishikwa nimwage ukweli, na baadhi yake nilizimwaga kidogo hapa huko nyuma. Alipoitwa Takukuru, huyu mkuu aliwaabisha na ukweli mpaka wakaishia kumuacha kama alivyo

- Lowassa alijichukulia maamuzi yote on his own bila kum-consult Rais, ndio maana moto ulipowaka Rais naye alimuachia abebe msalaba wake, Yona na Mramba, walitimiza sheria ya serikali ya kuruhusu kusamehe kodi, lakini tatizo ni kwamba hawakuwahusisha kamati ya bunge na bunge zima kama sheria inavyosema, ndilo tatizo la wezi wote duniani huwa wanajaribu sana kufuata sheria, lakini wanapindisha kiufundi sana wasijulikane.

- Rais alijua kuhusu kuwepo kwa mchakato wa umeme, one thing hakujua kwamba kuna ujanja unatendeka, alipohisi alimuita Masha na kumtukana sana kwamba kwa nini hakumuarifu mapema, ndipo kwa mara ya kwanza alipopata the glimpse ya the deal ya Lowassa, Lowassa pekee yake ndiye mchawi wa Richimonduli, ndio maana alikimbia bila kufukuzwa, the hero alikuwa Rutabanzibwa peke yake ndiye hakuhusika na ule wizi, wengine wote wakiongozwa na Lowassa walihusika.

- Ya Lowassa kusitisha mkataba ni another myth, kama ni kweli kwa nini Lowassa alitumia Billioni mbili kujaribu kuizima hii ripoti isiende bungeni? Kwa nini Hosea aliudanganya umma kwamba hakuna makosa Richimonduli? alitumwa na nani? Na kwa nini Lowassa alikuwa anamlilia Rais kwamba ni jm ndiye anayeleta fujo za Richimonduli, lakini ishu haina tatizo lakini mwishoni akakimbia mwenyewe bila kufukuzwa? Kama Rais alihusika kwa nini aliruhusu ripoti kwenda bungeni bila kuisoma kwanza, pamoja na kwamba aliambiwa mapema inawahusu marafiki zake wengi wa karibu?

- Jamani kama mnataka kuongozwa na Lowassa, msaidieni na kampeni zenu kama tunavyoziona hapa, lakini msitudanganye kwamba hakuhusika na Richimonduli wakati wengine on the record ndio mliokuwa mstari wa mbele sana kwenye kumsaidia Mwakyembe na ripoti, inatia kinyaa sana!

Lowassa ni mwizi tu, hata mumsafishe vipi ni kazi ya bure, yeye ndiye chanzo cha Richimonduli, bila ya yeye kusingetokea ule wizi, kama hamuridhiki na uongozi wa Rais wa sasa, yasemeni mapungufu yake kama yalivyo, lakini sio kujaribu kumuhusisha na asiyohusika nayo! Kwamba mnaweza kulikomboa taifa kwa kuwagombanisha Rais na Lowassa, kwangu sounds very low kwa sababu hili taifa linapaswa kuwa bigger than hawa viongozi wawili, kama we are running out of ideas za kulikomboa taifa letu basi tusubiri watoto wetu!

Respect.

FMEs!
 
Rev.Kishoka heshima mbele,

Ninaona hoja ya msingi hapa ambayo Mh.EL ataitumia kujisafisha.unless kama ni yeye aliyetoa maagizo ya maandishi kwa Mh.Msabaha kufukuzia advance Hazina tofauti na maelekezo yake mwenyewe ya awali ya kufungua Letter of Credit (LC).

Mpaka kwenye hatua ya kuagiza ifunguliwe LC naona Mh.Lowassa alikuwa sahihi sana,na kwa mazingira ya dharura ilikuwa ni sahihi kuwanyang'anya kazi TANESCO waliokuwa wanasuasua kufanya maamuzi.

Mhh! Nahisi EL ataponyoka kwenye hili la Richmond na hapo ndipo mbio zake za ikulu zitakapochukua kasi ya ajabu.Na hapo ndipo akina yakhe waliokuwa wanampiga vita watakapotafuta nchi ya kwenda kujificha.

Let's wait and see,sinema hii itakavyomalizikia. Je,Starring EL atauawa?
Sidhani kama Lowasa atakuwa na Uso wa kukimbilia Ikulu, Lowasa ni la kuvunda halisikii Udi wala Ubani.
Na hao kina yakhe wanaompinga (sidhani kama kuna anaempiga vita) kwa nini watafute nchi za kujificha? Wakati wa kutishana umepita.
Hata kama atafika Ikulu kama Rais Atwajibika kufanya kazi kwa mujibu wa Katiba ya nchi. Na kumbuka kufika Ikulu Unahitaji akina Yakhe kwa Mamilioni.
 
Back
Top Bottom