Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Ukiwa hujui taratibu za manunuzi na due deligence utajibu kama ulivyo jibu, lakini ukiwa unajua utapingana na majibu ya lowasa.
kwanza unatakiwa ujue kwanini kunafanyika due deligence, hii inafanyika ilikuepuka kupata mkandarasi asiye faa, iwe mkurugenzi wake au hiyo kampuni, na hivi vitu vipo, sio kwamba mimi ninatunga leo, pili mkandarasi kutakiwa kutoa mahesabu yalio kaguliwa, bank statement, wasifu wake kwa kazi alizokwisha fanya etc etc, sasa hili lilifanyika kwa ufanisi? nini yalikuwa mapendekezo ya wataalamu kuhusiana na hili?
Humu JF watu na kwenye magazeti yaliisha anza minongono, Gire nk wakatupa web site na kudai wameweka bomba la mafuta Costa rica etc etc, lakini licha ya huo uongo wao watu waliliona hilo, tena wasio kuwa na resource, je serikali inayo ongozwa na waziri mkuu walishindwa kuliona hilo?
Nini matumizi ya balozi zetu zilizo nje ya nchi? si ni kuisaidia serikali kwa shughuli zilizo nje ya nchi?
Nini matumizi ya AG office ikiwa mshauri mwenyewe wa sheria naye haisaidi serikali.
Jingine unatakiwa ujue wajibu wa kazi za waziri mkuu, nazo ni kumsaidia Raisi, sasa hapa nitakupa mfano aliotoa Warioba , kwamba nyerere alitaka kumchagua kiongozi aliyehukumiwa kwa sheria za uchaguzi, warioba akmwambia mzee utakuwa unavunja katiba, nyerere akawa mbishi kidogo, lakini warioba alikwenda kwa waziri mkuu Sokoinne akampiga shule akaelewa, kesho yake warioba na sokoinne walienda kwa mwalimu, mwalimu nae akasema unajua jana sikulala, nilikuwa nafikiria lile jambo, pia unatakiwa uelewe kwanini nyerere alimlaumu malecela waziri mkuu na makamu wa Raisi? na kolimba katibu wa ccm, raisi Alhaji Ali na mwenyekiti wa CCm, sababu alivyo taka kuingiza mchi OIC, hawa jamaa kwa sababu zao mwenyewe walishindwa kumwambia au kumshauri Raisi na Mwenyekiti wao kwamba hiyo itakuwa ni kinyume cha katiba yetu na Sera ya Chama.
Sasa kwa hili hata kama Raisi alitaka iwe hivyo waziri mkuu alikuwa anatakiwa kulisisitizia hayo mapungufu ambayo aliyaona kama mtu mwerevu angeamua hakubalina na hili kwa maandishi au kwa kujiuzulu, lakini kuonyesha kwamba ni kiongozi dhaifu, hakufanya hivyo , bali nae akashiriki kuingia mkataba tata.
Zaidi ya hapo richmond alianza kusua sua kuleta mitambo kwa kukosa mtaji, na minongono ilikuwepo, sasa hapa ilikuwa ni wakati muuafaka wa kuvunja mkataba for non delivery as per agreement, badala yake wakaridhia kuwauzia huo mkataba Dowans.
August,
Kama Due Dilligence ingekuwa inafanyika Tanzania, leo hii tusingekuwa na IPTL, Rada, GulfStream, ATCL, TRL-Rites, EPA, CIS, Kiwira, Vhalambia, Nolan au Richmond!