Hivi ndivyo Lowassa alishiriki Richmond

Hivi ndivyo Lowassa alishiriki Richmond

Nikikumbuka richmond naliaaaaa halafu natulizia na ga..........................
 
Makaayamawe,

Mengi hausiki na hiyo habari. Yeye ni mmiliki tu wa kile chombo na si mhariri na wala mwandishi wa habari.

tangu lini mwenye mali asihusike na madhara ya mali yake???

Umetumwa kumtetea mengi? Nani kamlaumu humu?!!!

Kasi yako ni ya ajabu katika utetezi hata hakimu hajasema kama ana kesi ya kujibu au la!!!
 
Pamoja na kuandikwa vizuri, barua iliyowekwa ukurasa wa mbele wa Nipashe ina walakini, inaweza kuwa imechomekwa kumsafisha!!!!!
 
Kwahiyo nipashe wanakaba penalty?!!! Hahahaaaaaaaaa!!

Ninadhani kuna untold stories za richmond ngoja tuone bungeni wakuu, lowasa siyo mtu mbaya wa kiasi tunachosomeshwa hapa lakini si kila baya la richmond ni lowasa wakuu, hebu tuone hatima huko bungeni huenda tukapata jipya hapa jamvini
 
afu kuna watu wanataka kumsafisha humu sebreni JF kweupee? HUYU MTU HATA WAKIMSAFISHA HATUKUBALI.
 
hii ni hatari sana, na inauma kuona watu ambao tunawapa nafasi ya kututumikia wanageuka watu wa kutuibia
 
Bonge la fisadi hilo. Ndiyo maana utekelezaji wa maazimio ya bung e ni mgumu Mshikaji wa JK ni nwizi mkubwa sana . sijui tutamokoaje kwenye kikao kinacho fuata cha Bunge .Lete vitu wanaJF.
 
Nipashe wamenusa taarifa ya serikali Bungeni wiki hii nini?
wana jembe pale linaitwa Jesse Kwayu hili ni balaa katika investigative journalism, sitashangaa kama wanataarifa zote...naona watakuwa wakitoa kama dose mpaka kikao kiishe...bravo Nipashe.
 
weka barua yote hapa tuisome yenye hayo maelezo otherwise ni walewale tu....
 
Bonge la fisadi hilo. Ndiyo maana utekelezaji wa maazimio ya bung e ni mgumu Mshikaji wa JK ni nwizi mkubwa sana . sijui tutamokoaje kwenye kikao kinacho fuata cha Bunge .Lete vitu wanaJF.

ushabiki maandazi huo...
 
Sasa mnangoja nini? Nauliza mnangoja nini kumpeleka Lowasa mahakamani? Naudihika sana, eti watajidai hakuna ushahidi, unataka ushahidi gani? Tatizo tunaoneana haya kwenye haya mambo ya kifisadi, nachukia mimi, sijui nihame nchi, utafikiri sio watanzania bwana
 
tangu lini mwenye mali asihusike na madhara ya mali yake???

Umetumwa kumtetea mengi? Nani kamlaumu humu?!!!

Kasi yako ni ya ajabu katika utetezi hata hakimu hajasema kama ana kesi ya kujibu au la!!!
FDR. Jr,

nimemuelimisha tu mwenzio Makaayamawe, na hata kama na wewe ulikuwa hujui, habari ndiyo hiyo.
 
Mkuu Mgongo heshima mbele,
Ni kweli kabisa akienda mahakamani ataumbuka. Swali ni kuwa je atakaa kimya baada ya kuwekwa wazi kiasi hiki na Mengi? Maana ingawa tulikuwa tunajua juu ya ushiriki wake, hajawahi kuropokewa hadharani na magazeti.

Akikaa kimya atakuwa amekubali ushiriki, akijitosa kujitetea atakuwa amejipalia makaa, kazi kwake.

....Juzi huyu 'mzalendo' alienda kulipia kadi yake ya ccm tawi la mkunguni....
makaayamawe, R U thinking what i'm thinking???
 
Hivi lowasa, chenge, JK, mkapa, n.k. wana damu kama yetu au?? Nafikiri wao hawata kufa eti??


Ili ujue kwamba hawa ni shetani wabaya..Mchezo wanao utumia ni kupeana deal. Nadhani Inapotokea serikali inahitaji kununua kitu kwa bei kubwa au kumilikisha mali hawa njoka wakali huambizana ...""" mkuu hii nikupe wewe au niendelee ? Au tumpe MK yeye hajapiga deal muda mrefu.. HAYO NDIO MAMBO AMBAYO LEO NA KESHO NA KESHO KUTWA hata upige kelele vipi hutaweza kuwashtaki kwani deal wamekuwa wakipiga pamoja..! Leo Rada chukua wewe, kesho Richmond niachie mimi, kesho kutwa Kagoda tumpe mzee.. Urais hamisheni fedha kwaajiri ya kampeni. Unategemea utamshtaki mtu hapo kweli ? Tanzania tunahitaji kutumia nguvu..

Nguvu na uwezo uliotumika kumtoa Nduli IDD amin DADAA ndio vitumike ktk kuwatoa hawa nyoka wenye sumu kali katika maendeleo ya watanzania. Kama alivyosema baba wa Taifa Mwl. Sababu za kuwatoa Tunazo, na Uwezo wa kuwatoa Tunao..tumechoka kunyanyasika kwenye ardhi yetu.! Silaha yetu ya mwisho ni katika uchaguzi mkuu. Hatuhitaji kutumia nguvu za kijeshi kwani hatuna uwezo nazo bali kura yako na yangu ndio uwezo wetu.
 
Hivi lowasa, chenge, JK, mkapa, n.k. wana damu kama yetu au?? Nafikiri wao hawata kufa eti??


Sio hao tu, kinachosikitisha zaidi ni hawa vibaraka wao kama akina Msabaha, Mwakapugi n.k. Wewe utapewaje maagizo huku ukijua kabisa hii ni dili chafu halafu usaini tu kisa eti umepewa na bosi?

Watanzania mlio kwenye vyeo lazima mbadilike. Fikirieni umma kwanza kabla ya interest binafsi. Najua ni ngumu sana kwenda kinyume na matakwa ya bosi lakini kama ni kwa maslahi ya taifa lazima tufanye hivyo. Unaogopa ukimkatalia atakufukuza kazi, kwani bila kazi utakufa? Mbona tukija gundua kama tulivyogundua la Richmond bado utafukuzwa kazi? Si bora ujiondoe with dignity??

Wote waliohusika na uchafu huo wachukuliwe hatua kila mmoja kwa nafasi yake. Eti mkuu wa nchi naye anasema hawezi kumfukuza Lowasa maana hana ushahidi. Pumbaf sana.
 
Mkuu Rev Upo? I would like to read your comments on this!

Mairo,

Je mnajua mchakato mzima wa uzabuni wa Serikali ulivyofanyika? Ukisoma hii taarifa, hakuna chochote kigeni ambacho ni cha kustaajabisha au usema kukiukwa kwa taratibu.

Suala la umeme ambalo lilileta Richmond lilitokana na kuhitajika kwa umeme wa dharura. Serikali kwa kupitia IMF/WB walikubaliana kuwa kwa kuwa hii ni emergency, zile protocal za ku-float tender kupitia zabuni na kadhalika ziachwe na kufanyike hiyo GNT.

Waziri Mkuu alipewa jukumu hili na Rasi na hakujichukulia uamuzi binafsi.

Kama mnakumbuka Kikwete alijitapa na kusema Richmond walipewa mkataba kutokana na kuwa na fees ndogo kuliko wengine, na ndipo tukahoji je mliangalia uwezo, lakini Serikali haikujibu.

Ukisoma hii habari, unaona ni mtiririko wa utekelezaji wa maamuzi ya Serikali na hakuna lolote lile.

Tena mbaya kuna TAHADHARI kijana wetu Eddo ametoa kuwa ikidhihirika yanayosemwa ni kweli, basi mkataba usitishwe na zaidi akasema itumike ile mbinu ya kutumia Letter of Credit kuwalipa hawa jamaa na si vingine!

Sasa kama mnajua L/C zinavyofanya kazi, mngejua kuwa Richmond walipaswa kuleta mitambo kwanza kabla ya kulipwa na kama wangeshindwa kuleta mitambo, wasingelipwa na mkataba ungekaa mguu pande!

Swali ni kwa nini Msabaha alikwenda kwa Meghji na Kikwete akiomba jama wapewe advance?

Ukisoma matendo ya Lowassa, hayana tofauti na ya Mramba au Yona ambao leo wanashitakiwa eti kwa uzembe ilhali kila walichokifanya kina Yona na Mramba kilikuwa na baraka za Serikali na kuchapwa kama agizo katika gazeti la Serikali.

Suala la kujiuliza tuhuma hizi za kusema alishiriki, je alishiriki kuhujumu au alishiriki kiutendaji kama alivyopewa jukumu hilo la kuhakikisha tunapata umeme wa haraka?

Mbona gazeti hili halichapi au kueleza jinsi Lowassa alivyokimbia Ikulu na kumwambia Rais wasitishe mkataba na Rais akakataa akasema anaogopa kesi London na tuendelee na mkataba ilhali ilishoaonekana kuwa Rochmond hawana uwezo?
 
Mairo,


Mbona gazeti hili halichapi au kueleza jinsi Lowassa alivyokimbia Ikulu na kumwambia Rais wasitishe mkataba na Rais akakataa akasema anaogopa kesi London na tuendelee na mkataba ilhali ilishoaonekana kuwa Rochmond hawana uwezo?
kwa nini Lowasa mwenyewe asiseme hivyo kuwa alimwambia kikwete na kikwete akakataaaaa, kwa nini lowasa asiitishe mkutano na waandishi wa habari akaeleza upande wake??
kama hawezi kufanya hivyo yeye ndiye richmond.
 
Mairo,

Je mnajua mchakato mzima wa uzabuni wa Serikali ulivyofanyika? Ukisoma hii taarifa, hakuna chochote kigeni ambacho ni cha kustaajabisha au usema kukiukwa kwa taratibu.

Suala la umeme ambalo lilileta Richmond lilitokana na kuhitajika kwa umeme wa dharura. Serikali kwa kupitia IMF/WB walikubaliana kuwa kwa kuwa hii ni emergency, zile protocal za ku-float tender kupitia zabuni na kadhalika ziachwe na kufanyike hiyo GNT.

Waziri Mkuu alipewa jukumu hili na Rasi na hakujichukulia uamuzi binafsi.

Kama mnakumbuka Kikwete alijitapa na kusema Richmond walipewa mkataba kutokana na kuwa na fees ndogo kuliko wengine, na ndipo tukahoji je mliangalia uwezo, lakini Serikali haikujibu.

Ukisoma hii habari, unaona ni mtiririko wa utekelezaji wa maamuzi ya Serikali na hakuna lolote lile.

Tena mbaya kuna TAHADHARI kijana wetu Eddo ametoa kuwa ikidhihirika yanayosemwa ni kweli, basi mkataba usitishwe na zaidi akasema itumike ile mbinu ya kutumia Letter of Credit kuwalipa hawa jamaa na si vingine!

Sasa kama mnajua L/C zinavyofanya kazi, mngejua kuwa Richmond walipaswa kuleta mitambo kwanza kabla ya kulipwa na kama wangeshindwa kuleta mitambo, wasingelipwa na mkataba ungekaa mguu pande!

Swali ni kwa nini Msabaha alikwenda kwa Meghji na Kikwete akiomba jama wapewe advance?

Ukisoma matendo ya Lowassa, hayana tofauti na ya Mramba au Yona ambao leo wanashitakiwa eti kwa uzembe ilhali kila walichokifanya kina Yona na Mramba kilikuwa na baraka za Serikali na kuchapwa kama agizo katika gazeti la Serikali.

Suala la kujiuliza tuhuma hizi za kusema alishiriki, je alishiriki kuhujumu au alishiriki kiutendaji kama alivyopewa jukumu hilo la kuhakikisha tunapata umeme wa haraka?

Mbona gazeti hili halichapi au kueleza jinsi Lowassa alivyokimbia Ikulu na kumwambia Rais wasitishe mkataba na Rais akakataa akasema anaogopa kesi London na tuendelee na mkataba ilhali ilishoaonekana kuwa Rochmond hawana uwezo?

Mchungaji kweli una roho ngumu.
 
Back
Top Bottom