Ukichunguza sana haitakosa.
Ukimsoma Dr. Thomas Molony aliyeandika kitabu cha "Nyerere:The Early Years" anayezungumzia miaka ya mwanzo ya Kambarage Nyerere, utaona kwamba kumbe hata Burito Nyerere, baba yake Kambarage Nyerere, hakuwa Chifu wa kurithi utawala kutoka kwa baba yake, alikuja kuwa Chifu baada ya watu kumkataa Chifu aliyekuwepo kabla kwa sababu ya migogoro.
Kwa hiyo kuna mambo machache ya kuzingatia hapa.
1. Wakoloni katika jitihada za kurahisisaha utawala wao, walitumia dhana ya "kabila" kutatua matatizo ya utawala kwa kuwagawanya watu katika makabila tofauti, mengine ambayo hayakuwa well defined na mengine ya kutunga tu ambayo hayakuwepo kabisa. Hapo utakutana na habari za "divide and rule".
2. Hata kabla ya utawala wa wakoloni, uhamaji hamaji wa makabila ya Kibantu hususan Africa katika miaka 2000 iliyopita, na zaidi katika miaka 300 iliyopita, umesababisha habari nzima ya "kabila pure" kuwa ni kitu kisichoyumkinika. Hii habari iko hata kwa makabila yasiyo ya kibantu. Peter Firstbrook katika kitabu chake cha historia ya familia ya Obama "The Obamas: The Untold Story of An African Family" kaonyesha jinsi uhamaji hamaji wa watu kutoka kaskazini ulivyokwenda mpaka kuja kuzaliwa Barack Obama. Leo hii kuna Wasukuma wamehama makazi kutoka Mwanza wamefika mpaka Ufipa na wengine wako Zambia wamejichanganya huko. Habari nzima ya "kabila pure" ni hadithi zaidi ya ukweli