Hivi Magufuli atagombea tena?

Hivi Magufuli atagombea tena?

Katiba ya JMT (1977) inamruhusu, na kanuni za chama chake zinamruhusu. Lakini ikitokea baadhi ya mawaziri wakajitenga kati ya sasa na 2020 kwa kuona kwamba hawaendani na kasi yake, hivyo kupisha wenye uwezo, watavurugana sana ndani ya chama chao, na sio kwa uchaguzi wa 2020 tu bali hata uchaguzi wa Mwenyekiti taifa baadae mwaka huu.
Mkuu Mchambuzi kwa maoni yako kwenye hii lineup ya hawa panya, unaona kweli kuna panya yoyote mwenye uwezo wa kumfunga paka kengele? .

Nimenote hata wale watu wa Nyerere waliokuwa very vocal wakati wa JK kina Butiku, Kaduma, Kitine, Warioba and the like wameisha soma alama za nyakati na kujua saa hizi ni nyakati nyingine hivyo wamekaa chonjo saa mbaya.

Ila kuna kigogo mmoja tuliongea off the record akasema atamtafuta na kumkabili, haiwezekani wote tuendelee tuu kumchekea nyani, tutayavuna mabua ilhali shamba ni letu sote.

Paskali
 
Nakumbuka wakati wa kampeni alivyopata shida kujinadi, ikafika mahali mzee wa watu akaanza kupiga push ups, akaongea kila lugha ili raia wamuelewe haikutosha akaacha na chama chake akaanza kukiponda na kusema wao ndio wameifikisha hii nchi hapa.

Maswali pekee ambalo najiuliza mpaka sasa huyu mtu atagombea tena? Hakumbuki yaliyompata kipindi kile, hivi atawaeleza nini watanzania wamuelewe au ndio anasubiri 2019 awasaulishe, atarudi Kagera kuomba kura? Kule simiyu ataenda? Watumishi wa umma atawaomba kura? Wanafunzi wa vyuo vikuu je?, wahitimu wa vyuo vikuu atawambia nini? Atajiteteaje kuhusu Tanzania ya viwanda, nakumbuka alisema serikali yake ni viwanda hivyo viwanda vimefika vingapi? Au ndio vile anavyozindua vilivyo anza kufanya kazi kipindi cha Kikwete.

Vijijini huko atawaeleza nini kuhusu milioni 50 alizoahidi, ataenda huko kweli kuomba kura zao. Wafanyabiashara ambao wamefunga biashara zao kutokana na hali mbaya kiuchumi atawaambia nini? Kuna msemo unasema "usitukane mambo kabla hujavuka mto" nakumbuka Mhe alianza kwa mbwembwe na dhihaka nyingi kwa watangulizi wake, nadhani hivi sasa anajionea.
Labda swali la nyongeza. Je CCM watamkubali tena?.
Ama atakuwa na WAPINZANI chamani?
 
Labda swali la nyongeza. Je CCM watamkubali tena?.
Ama atakuwa na WAPINZANI chamani?
hili pia sio swali kwa sababu ni utaratibu wa CCM, aliyepo anasimama vipindi viwili bila kupingwa. Mwana CCM yoyote haruhusiwi kujaza fomu kumpinga, ila hii sio sheria wala sio kanuni bali ni taratibu yao CCM.

P.
 
Katiba ya JMT (1977) inamruhusu, na kanuni za chama chake zinamruhusu. Lakini ikitokea baadhi ya mawaziri wakajitenga kati ya sasa na 2020 kwa kuona kwamba hawaendani na kasi yake, hivyo kupisha wenye uwezo, watavurugana sana ndani ya chama chao, na sio kwa uchaguzi wa 2020 tu bali hata uchaguzi wa Mwenyekiti taifa baadae mwaka huu.
Hiyo Afrika bado sana mkuu. Waziri ajitenge eti kisa haendani na kasi ya rais! Wanakomaa kama luba hadi wang'olewe.
 
Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania wananchi tunasubiri uchaguzi kwa hamu miaka mitatu badae kutokana na kuchoshwa na Uongozi wa aliyepo madarakani.
 
hili pia sio swali kwa sababu ni utaratibu wa CCM, aliyepo anasimama vipindi viwili bila kupingwa. Mwana CCM yoyote haruhusiwi kujaza fomu kumpinga, ila hii sio sheria wala sio kanuni bali ni taratibu yao CCM.

P.
Mkuu, ni kweli ni taratibu zao kichama ziko hivyo.
Ila ukiangalia katika jicho la uchambuzi wa kisiasa, unabaki na maswali yasiyojibika kirahisi.
Hata hivyo Pascal uko SAHIHI.
Yetu macho
 
Back
Top Bottom