Hivi kwanini Mungu ana wivu?

Hivi kwanini Mungu ana wivu?

Kutokuwepo ni nini? Unaposema kisiwepo unamaanisha nini? Nadhani tatizo lipo hapa kwenye tafsiri ya kuwepo na kutokuwepo. Tuanzie hapa. Ni nini maana ya kutokuwepo?
Kinyume Cha kuwepo
 
S
Wewe akili zako zimekuwezesha kutengeneza uhai hata wa kifaranga cha kuku? Hizo nyota unazoziona kila siku umeshawahi hata kuisogelea nyota ya karibu zaidi? Kwa hiyo kwa akili zako hizo unamhoji aliyeset na kuweka hiyo mifumo?
Swali ni una uhakika gani au unathibitisha vipi madai yako ayo? Nyota zimewekwa/zimesetiwa?
 
Mtu hajawahi hata kuvuka nje ya solar syatem yake, achilia mbali hata kusogelea kwenye nyota ya karibu zaidi na jua, añatumia akili hizo hizo kuhoji utendaji wa Mungu 😄

images - 2024-04-09T150147.052.jpeg
 
Kinyume Cha kuwepo
OK, sifa za kuwepo ni matokeo, Yaani uwepo wako utagusa mwingine kimawazo, kiutendaji, kihisia n.k. Ili tuseme upo lazima kuwe na matokeo ya uwepo wako either kiutendaji, kifikra au kihisia na hayo matokeo yatagusa uwepo wa mtu/vitu vingine. Sahihi?
 
Sasa wewe umeyajuaje wakati wewe pia una ufaham na akili za kibinadam tu. Tena unapambania kabisa kama vile una uhakika
Unajua wewe ni kama mjinga ambaye yupo shimoni unaambiwa kule juu hauwezi kufika sehemu yetu ni huku, alafu unaanza kufoka "wewe umejuaje kama kule hakufikiki, umejuaje kama hapa tupo shimoni" khaa! Sasa unauliza wakati unaona kwamba upo shimoni! Akili na ufahamu wa kibinadamu ndiyo unaokufahamisha kwamba wewe utabaki kuwa mwanadamu na kamwe akili zako haziwezi kulingana na Mungu. Usilazimishe akili zako kuchunguza akili za Mungu.
 
Unaamini usicho kijua na ambacho hakipo , ila mkuu sio mbaya kwa sababu ni haki yako kuamini chochote wewe toy wa Mungu.
Mbona tunapangiana kwamba naamini nisichokijua! Namjua Mungu lakini natambua akili zake hazichunguziki! Usipende kuforce mambo, kama hauelewi jambo tulia uelekezwe ujifunze na mwisho wa siku ukubali na uongeze hekima.
 
Wataalamu wa bibilia, nakumbuka kuna siku nilisoma hicho kitabu nikaona historia ya mnara wa babeli Mungu aliposhuka na kuwakuta binadamu wanatengeza ule mnara alishtuka na kuwatenganisha kwa lugha pamoja na maeneo ndiyo yakazaliwa mataifa mengine.

Tukio la pili kwenye sura ya mwanzo Mungu baada ya adamu kula ule mti ambao alikatazwa inaonekana ibilisi alikuwa anajua siri ya mti huo wa uzima japo hakuufahamu haswa ni upi ila baada ya Mungu kuona binadamu na jeshi lake watapanga kuutafuta ndiyo akauficha, nimesahau exactly ni wapi.

Case ya tatu, baada ya kuwatoa Wanaisraeli kupitia Mtume wake Musa aliwaambia kuwa yeye ni Mungu mkuu na anawivu hivyo wasiabudu mwengine isipoikuwa yeye.

Je, kwa kauli ya kusema kuna miungu mengine anafahamu kuwa kuna nguvu nyengine tofauti na yeye?

Je, hajiamini na nguvu zake?

Je, Mungu huyu ni tunayemuabudia wakristo na waislamu?

Je, ni binadamu wa mwanzo ambaye aliwahi kutambua siri za ulimwengu na akajitahidi kuzificha na hatimaye akajitolea taji la uungu?

Nawasilisha.
Mungu hayupo mkuu.

Hizo ni hadithi za kutungwa na watu tu.
 
Mbona tunapangiana kwamba naamini nisichokijua! Namjua Mungu lakini natambua akili zake hazichunguziki! Usipende kuforce mambo, kama hauelewi jambo tulia uelekezwe ujifunze na mwisho wa siku ukubali na uongeze hekima.
Alie kupangia ni nani ? Amini unacho amini ni haki yako kikatiba, ila wewe na wenzako hakuna mtakacho nifundisha kuhusu hizo hadithi za abunuasi mpka siku nakufa.
 
Back
Top Bottom