Hivi kuna uhusiano gani kati ya mvua na foleni za barabarani Dar es Salaam?

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
Moja ya jambo ambalo inawezekana changamoto ni miundombinu au labda ni vyombo vyetu vya usafiri, bado huwa nashindwa kuelewa vizuri, yaani ikitokea mvua imenyesha kidogo tu kwenye Jiji la Dar es Salaam hasa maeneo ya town, lazima foleni barabarani ziibuke kwa kasi.

Najiuliza, hivi tatizo ni miundombinu yetu kuwa haina uwezo au vyombo tunavyotumia kusafiria ndiyo vibovu, kiasi kwamba mvua ikinyesha vinavuja au vinaharibika, mfano leo imenyesha mvua kidogo tu lakini foleni hadi watu wanachelewa kwenye mishe zao.

Huu mji kuna vitu inabidi vifanyike, hili siyo jambo zuri kiuchumi na siyo kitu kizuri kwa faida ya Taifa.

Nasema hivyo kwa kuwa Dar ndio Mji mkubwa kibiashara, sasa kunapokuwa na foleni za kinomanoma kama hivyo, unadhani inamaanisha nini kiuchumi? Tunafeli wapi?
 
Barabara mbovu, fumba macho then fungua mara waaaa, kuna fly over kutoka msimbazi road hadi ubungo, kuna fly over kutoka kamata hadi mtoni, kuna fly over kutoka muhimbili hospital hadi mwenge, fly over kutoka posta ya zamani hadi mji mwema,na kuna fly over kutoka uhuru mchanganyiko hadi 603kj, mmmm hii ndio Dar mpya, nyesha mvua hakuna kabisa traffic jams
 
Mvua ikinyesha watu hawapiti njia za mkato (vichochoro) kutokana na kutokuwa na hali nzuri.

Pili kuna wale wenye magari ya kuegesha (yamechoka/lina hitilafu) au wengine hawapendi kutumia/kuendesha magari siku mvua ikidondoka yote haya yanatoka hata anaeogopa kuweka mafuta siku hiyo anapiga kidebe chake saaafi ili mradi asisote
 
miundo mbinu ni mibovu na imepitwa na wakati, mvua kidogo tu maji yanafurika barabarani badala ya kupita mitaroni, the result ni slow speed
 
Hata mimi huw na jiulza Mvua inauhusiano gan na folen

Labda mvua ikinyesha watu wengi gafla wanatumia magar
 
Back
Top Bottom