ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,653
Jamani leo naona jirani yangu niliyezoea kumuomba 'lift',
nadhani huenda baada ya 'kunichoka' kutokana na katabia
kangu ka kumuomba lifti wakati wa kwenda kazini.
Huenda aliamua kunitolea uvivu, au pengine nilikuwa namboa, au pengine
kwa mtazamo wake, anadhani ninao uwezo au labda ni ubahili
wangu.......hata sijui why....ila kifupi mara baada ya kupanda, akionekana
hana furaha, neno lake la kwanza likawa 'Hivi jirani kwa nini hununui
gari likusaidie usafiri wa kwenda na kurudi ofisini? Abiria wengine wawili walokuwa
ndani ya gari walibaki kuangaliana tu, maana nao kama wasaidiwa
huenda walihis hilo 'dongo' linawahusu pia
Kwa kuhisi huenda jamaa kanichoka, nililoweza kufanya ni
kuguna tu, mhhhhhh bila kujibu kitu huku nikiwa na aibu tele usoni.
Baada ya kwenda kama mita 70 hivi, nikajidai nimesahau simu na kumuomba jamaa
anishushe niirudie simu yangu nyumbani. Baada ya kushuka
nikapanda zangu daladala na kuelekea job.
Hapa kazini hii stori imekuwa gumzo kwani abiria wale wengine waliifikisha
hii skendo ofisini na imekuwa gumzo la siku. Kila mtu 'ananitania' kwa kurudia
kauli ya mshikaji, 'Hivi jirani kwa nini hununui gari'? Nabaki nacheka tu hapa
ofisini!
nadhani huenda baada ya 'kunichoka' kutokana na katabia
kangu ka kumuomba lifti wakati wa kwenda kazini.
Huenda aliamua kunitolea uvivu, au pengine nilikuwa namboa, au pengine
kwa mtazamo wake, anadhani ninao uwezo au labda ni ubahili
wangu.......hata sijui why....ila kifupi mara baada ya kupanda, akionekana
hana furaha, neno lake la kwanza likawa 'Hivi jirani kwa nini hununui
gari likusaidie usafiri wa kwenda na kurudi ofisini? Abiria wengine wawili walokuwa
ndani ya gari walibaki kuangaliana tu, maana nao kama wasaidiwa
huenda walihis hilo 'dongo' linawahusu pia
Kwa kuhisi huenda jamaa kanichoka, nililoweza kufanya ni
kuguna tu, mhhhhhh bila kujibu kitu huku nikiwa na aibu tele usoni.
Baada ya kwenda kama mita 70 hivi, nikajidai nimesahau simu na kumuomba jamaa
anishushe niirudie simu yangu nyumbani. Baada ya kushuka
nikapanda zangu daladala na kuelekea job.
Hapa kazini hii stori imekuwa gumzo kwani abiria wale wengine waliifikisha
hii skendo ofisini na imekuwa gumzo la siku. Kila mtu 'ananitania' kwa kurudia
kauli ya mshikaji, 'Hivi jirani kwa nini hununui gari'? Nabaki nacheka tu hapa
ofisini!