mwanalumango
JF-Expert Member
- Dec 13, 2010
- 232
- 280
Wengi tulipata wazo la kujenga vyumba viwili vya haraka na kuamia kwasababu ya manyanyaso ya wenye nyumba, sijutii kwakuwa ilinisaidia sana na kuhamia kwangu. Sasa wewe take it in a positive way, binadamu ndivyo tulivyo haiwezekani uje uniombe msaada siku ya kwanza nikupe, unakuja tena siku ya pili na ya tatu, unadhani nitakaa kimya. Ilikupasa wewe mwenyewe uone aibu kwanza, huwezi kuwa unapanda lift ya mtu bure tu kila siku huchangii hata kidogo, ilikupasa ujue jinsi ya kula na kipofu. Hata unapoanza maisha na kuwa kwa ndugu yake wa aina yeyote yule ingawa ndugu yako anafinance kila kitu basi ingawa kipato chako kidogo yakupasa siku za mwisho wa mwezi japo kununua kilo kadhaa za mchele na kigereni cha korie sio wewe upo tu. Hiyo barabara, ulistahili kuwatreate that way kwakuwa akili zako hazina akili za kufikiria kuwa unaweza ukachangia japo lita 5 kwa mwezi akili zako zinakueleza kuwa huyo jamaa ni tajiri na anaweza afford kila kitu huo ni wehu.
Jamani leo naona jirani yangu niliyezoea kumuomba 'lift',
nadhani huenda baada ya 'kunichoka' kutokana na katabia
kangu ka kumuomba lifti wakati wa kwenda kazini.
Huenda aliamua kunitolea uvivu, au pengine nilikuwa namboa, au pengine
kwa mtazamo wake, anadhani ninao uwezo au labda ni ubahili
wangu.......hata sijui why....ila kifupi mara baada ya kupanda, akionekana
hana furaha, neno lake la kwanza likawa 'Hivi jirani kwa nini hununui
gari likusaidie usafiri wa kwenda na kurudi ofisini? Abiria wengine wawili walokuwa
ndani ya gari walibaki kuangaliana tu, maana nao kama wasaidiwa
huenda walihis hilo 'dongo' linawahusu pia
Kwa kuhisi huenda jamaa kanichoka, nililoweza kufanya ni
kuguna tu, mhhhhhh bila kujibu kitu huku nikiwa na aibu tele usoni.
Baada ya kwenda kama mita 70 hivi, nikajidai nimesahau simu na kumuomba jamaa
anishushe niirudie simu yangu nyumbani. Baada ya kushuka
nikapanda zangu daladala na kuelekea job.
Hapa kazini hii stori imekuwa gumzo kwani abiria wale wengine waliifikisha
hii skendo ofisini na imekuwa gumzo la siku. Kila mtu 'ananitania' kwa kurudia
kauli ya mshikaji, 'Hivi jirani kwa nini hununui gari'? Nabaki nacheka tu hapa
ofisini!