Hivi hili penzi linachakachuliwa ? advice pls

Inawezekana mama wa kwanza!Binafsi sidhani kama ni rahisi hivyo kuchanganya majina katika maongezi...tena sio na rafiki mpya useme umesahau jina lake kwahiyo unabahatisha ila mchumba wako kabisa?Ni ngumu kidogo kuamini!

Unakosea mara ya kwanza unaambia bado katika ya maongezi unakosea tena unakanya ukitaka kusema Basi Samahani Lizzy unasema samahani Rose how is it kam kam ?
 
hana chake hapo, ameshaachakachuliwa mwambien msimfiche,huyo dada naona kama vile anahairisha msiba kuzika ila kama kifo tayari kilishatokea. (ajaribu kujirudi lini huyo bf alianza hako kajina ajue kama kuna jambo alimkwazaga ajirekebishe otherwise he has gone):sick:
 
Pole yake huyo dada, lakini jamani hakuna kitu kibaya kama kukosa uaminifu,
na kwa bahati mbaya mtu kama sio mwaminifu ni sio mwaminifu tu.
Labda mpaka atakapokutana na neema ya Mungu imuokoe.

Mi namshauri huyo dada asiingalie sana ndoa amuangalie zaidi huyo kaka, apime moyo wake
kama kweli unaweza kubeba hilo basi aamue kufunga ndoa, kama moyo wake hauwezi bora aachane nae tu,

Afadhali maumivu atakayoyapata sasa yatapona kuliko kidonda ambacho atakipata akiwa kwenye ndoa, hakiishi na hakiponi milele.
Afadhali kuacha mchumba, kuliko aje kuitwa mwanamke aliyeachika!!

Mungu amsaidie katika yote.


Asante LD kwa ushairi murua be blessed na utafanyiwa kazi ipasavyo
 
Ila kuna watu wana siri unaweza maliza hata mwaka lakini yote hayo usiyaone ,
Asante kwa ushauri mzuri
Huchoki kucheza wewe?

asante FL1
wajua ule ukaribu utamsaidia kunote vitu vidogodogo ambavyo huyu mtu wake lazima hata afiche vipi atajisahau tu kama ana mambo ya konakona
tukumbuke kuwa inauma sana unapokuwa na hisia hizo na pia kuacha au kuachwa ni maumivu zaidi,ajaribu kujiridhisha aona kama still wana future ama kiza kinene!!
sichoki kucheza,nahofia kitambi nisijekosa kilicho chema!
 
Ni takribani miezi miwili sasa ,mpenzi ,mchumba ,husband to be wake amekuwa kila mara akimpigia simu katikati ya maongezi yao kila anapotaka kuita jina la huyo dada F,amekuwa akiita jina la dada mwingine kabisa ,Huyu binti kila anapohoji maswali anapewa lugha nzuri

"..Mapenzi yamekwisha siku hizi..." - Banana Zoro
 
asante FL1
wajua ule ukaribu utamsaidia kunote vitu vidogodogo ambavyo huyu mtu wake lazima hata afiche vipi atajisahau tu kama ana mambo ya konakona
tukumbuke kuwa inauma sana unapokuwa na hisia hizo na pia kuacha au kuachwa ni maumivu zaidi,ajaribu kujiridhisha aona kama still wana future ama kiza kinene!!
sichoki kucheza,nahofia kitambi nisijekosa kilicho chema!

Nilishajifunza kutokana na makosa ,
 
Hivi kwanini watu tunashindwa kujituliza mpaka unaelekea kwenye hatua muhimu kama hii bado tu unahangaika kudodosa nje???????????????????????????????????????????????????????????????????????????
 
Mbu ......I think you are right ....ajaribu kukosea jina naye aone reaction ikoje...........
Haya Mapenzi haya..................duh aloyavumbua kweli amejua kututenda
 
Labda anamtaka kaka na anashinda kutwa kucha kwa wahanga!U neva kno!

KM NINGEKUWA nasar ndo ningefikiria ivo lakin kwa ivi sasa nipo la kwanza B so siwez fikiri ivo

uyo kaka ana mahusiano tena mapenzi makali yale na uyo dada anayemtaja jina ata akiongea na mamake mzazi...mi hapana..pangechimbika mwaya...ahhh daily anikosee?
so kichwani mwake folda zote zpo full kwa uyo mdada?ndo mana ukimklik tu znafunguka folda zake tu....ningemnyanyua nakwambia aaakkk badoooooooooooooo!!!!!
kwanza ningesepa..wakat anajileta sasa ningemwambia anyoshe maelezo juu ya uyo ndondocha wake anayehemwa hemwa nae kila nukta...maelezo yangekuwa mafup bas ningemwambia aende kwanza akamalizane nae akimaliza aje..na iyo ndo ingekuwa mwshooooo
SAA INGINE MUNGU ANAJARIBU KUKUONYESHA WEEEEI HATARI LAKIN WAPPP UMENG'ANG'ANA TU...
 
Wanaume wana mambo DA hapa mie nimeshindwa la klusema nikaona nileta hapa mmsaidie huyu mdada

Hakuna mapenzi hapo mwaya mie niliwahi kuwa na rafiki yangu mmoja akawa ananiambia mie sijui yule mwanamke kaniroga maana kila nikitaka kudo na my wife mpaka nivute hisia kwake ndo naweza bila hivyo hakuna ila alimtenda yule mdada ndo maana wakaachana kumbe jamaa bado linampenda
 
Huyo kuna jambo Mungu anamuonyesha au huyo mwanaume anafnaya makusudi au kalogwa na bidada wa kando......hiyo ndoa na isubiri,waelewane kwanza la sivyo ndo yale yale ya vilio kila siku while ulijua.....ogopa sana mwanaume amtaje mwanamke mwingine kila mara that shows anampenda,wanawasiliana kila saa na the guy is into the other gal kiasi kwamba mind ime-corrupt hata anajisahau......ndoa kama ipo ipo kama hakuna na huyo mtu usilazimishe.......
 
mkaka anaye alyeijaza moyo na akili yake
so apo ajiandae ata kat kat ya game anaweza akakosea jna....wewe asha sogea uku bwana ahh kumbe shost anaitwa magdalena...teh teh!!!
...ata wakipafom dzain jamaa atakuwa anaVUTA HISIA ZA ASHA ILI APATE STIMU ...akuna kitu bla sababu...angekuwa anakosewa majina tofaut ningeelewa bt daily uyo uyo ahhh pole yake

Dah Rose we mtata kweli kweli. Umefikaje huko?
Au una kapiriensi na hii maneno?!
 
Mwambie hivi..... UKIONA MANYOYA....UJUE KALIWA.......
Hapo kaishaingizwa mjini....mwenzie kuna mtu kamkaa rohoni.....aendelee kusoma alama za nyakati
 
Hivi kwanini watu tunashindwa kujituliza mpaka unaelekea kwenye hatua muhimu kama hii bado tu unahangaika kudodosa nje???????????????????????????????????????????????????????????????????????????

unajua kuna watu wanapata msukumo wa ndoa kutoka nje,sio nafsi zao,labda ni mpenzi wake ndo anataka waoane ama kuna msukumo wa wazazi ama umri na majukumu ya kazi
Ndoa ni hatua ambayo inahitaji uamuzi na ni hatua nyingine ya mabadiliko ya maisha ambayo ambayo utaingia kuishi kwa maisha yako ya mbeleni,hivyo kutafakari na kujiweka tayari ni muhimu.
ni uamuzi tu kuondokana na vishawishi
 
asante FL1
wajua ule ukaribu utamsaidia kunote vitu vidogodogo ambavyo huyu mtu wake lazima hata afiche vipi atajisahau tu kama ana mambo ya konakona
tukumbuke kuwa inauma sana unapokuwa na hisia hizo na pia kuacha au kuachwa ni maumivu zaidi,ajaribu kujiridhisha aona kama still wana future ama kiza kinene!!
sichoki kucheza,nahofia kitambi nisijekosa kilicho chema!


asante Inkoskaz noted with thanks
 
Huyu dada siyo mpenzi halali wa kijana huyu. Ameingilia penzi la mtu hapo. La pili hapa ni kwamba huyo dada hajui mambo, anapigwa bao na huyo anayetajwa!! Hawezi kumteka ili jamaa amsahau Pdemu wake halali. Ameingilia penzi la mwenzie, na mbaya zaidi kazi haiwezi vizuri na siku akimfahamu basi patachimbika. Anayetajwa wakati wa mapozi ya kujivinjari mambo ya kitangatanga ... kama Rose1980 alivyofafanua hapo juu, basi huyo ndiye mlengwa. Na hiyo ndoa ikitangazwa ujue kutakuwa na pingamizi hapo. Ushauri, mwambie huyo rafiki yako amwache mara moja kijana huyo.
 
Huyo kuna jambo Mungu anamuonyesha au huyo mwanaume anafnaya makusudi au kalogwa na bidada wa kando......hiyo ndoa na isubiri,waelewane kwanza la sivyo ndo yale yale ya vilio kila siku while ulijua.....ogopa sana mwanaume amtaje mwanamke mwingine kila mara that shows anampenda,wanawasiliana kila saa na the guy is into the other gal kiasi kwamba mind ime-corrupt hata anajisahau......ndoa kama ipo ipo kama hakuna na huyo mtu usilazimishe.......

Huyo jamaa hana nia ya dhati ya kumuoa huyo shostito.
Kwa mtazamo wangu ameshindwa kuwa na ujasiri wa kumweleza kwamba hana nia ya kumuoa, so anatafuta mbinu mbadala.
Mbona wengi tu wana "multiple choice" lakini hawafanyi makosa ya kizembe kama huyo jamaa?
Huyo bi shotito inabidi amtafune jongoo, ampige chini mshikaji ili maisha yaendelee vizuri, vinginevyo atakuja kulizwa vibaya!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom