Hivi hawa Mipango Miji wana kazi gani?

Saidama

JF-Expert Member
Jun 10, 2022
500
942
Hawa jamaa bana ni miyeyusho yani sijui hata wanafanya vipi kazi. Ukiangalia kwa sasa kasi ya watu kujenga maeneo ya pembezoni mwa mji imekua kubwa lakini hawa jamaa siwaoni kabisa wakitimiza majukumu yao ya kupima viwanja kwa kasi ili watu wanapojenga, haya maeneo mapya angalau yawe na mpangilio mzuri sio kama mitaa ya zamani (mfano uswahilini).

Sasa hawa mipango miji bana, unaweza jitutumua ukajenga ka nyumba kako taratibu hata kwa miaka miwili huwaoni kuja kukwambia chochote ila ukisha kamilisha ndio wanakuja kukuwekea 'X bomoa'. Hivi mi nijenge nyumba yangu kwa biashara yangu ya miogo kwa kudunduliza kwa miaka hata miwili taratibu halafu nikamilishe we uje tu from nowhere uniambie nibomoe, haiingii akilini.

Sasa cha kushangaza kuna maeneo mengine hata hayapo mbali na mji, yani unakuta hata ni km20 tu kutoka katikati ya mji ila bado hayajapimwa na unakuta ni maeneo ambayo yameanza kuendelea tangu 2015. Sasa hawa jamaa hua wako wapi. Wanafanya vipi kazi!

Huu ujinga ndo hata haya maeneo mapya yataishia kua na mpangilio kama wa Manzese.
 
Hawa jamaa bana ni miyeyusho yani sijui hata wanafanya vipi kazi. Ukiangalia kwa sasa kasi ya watu kujenga maeneo ya pembezoni mwa mji imekua kubwa lakini hawa jamaa siwaoni kabisa wakitimiza majukumu yao ya kupima viwanja kwa kasi ili watu wanapojenga, haya maeneo mapya angalau yawe na mpangilio mzuri sio kama mitaa ya zamani (mfano uswahilini).

Sasa hawa mipango miji bana, unaweza jitutumua ukajenga ka nyumba kako taratibu hata kwa miaka miwili huwaoni kuja kukwambia chochote ila ukisha kamilisha ndio wanakuja kukuwekea 'X bomoa'. Hivi mi nijenge nyumba yangu kwa biashara yangu ya miogo kwa kudunduliza kwa miaka hata miwili taratibu halafu nikamilishe we uje tu from nowhere uniambie nibomoe, haiingii akilini.

Sasa cha kushangaza kuna maeneo mengine hata hayapo mbali na mji, yani unakuta hata ni km20 tu kutoka katikati ya mji ila bado hayajapimwa na unakuta ni maeneo ambayo yameanza kuendelea tangu 2015. Sasa hawa jamaa hua wako wapi. Wanafanya vipi kazi!

Huu ujinga ndo hata haya maeneo mapya yataishia kua na mpangilio kama wa Manzese.
WIZARA ya ARDHI kwa Asilimia 100 Imehusika na Uharibifu wa Miji yetu kutokana na Watalaamu wake kutowajibika
Jiji la Dar lolikuwa Makao makuu ya Nchi Wakubwa wote Walikuwepo Wizara ilikuwepo lakini Ujenzi holela kila sehemu hakuna wa Kukemea
 
WIZARA ya ARDHI kwa Asilimia 100 Imehusika na Uharibifu wa Miji yetu kutokana na Watalaamu wake kutowajibika
Jiji la Dar lolikuwa Makao makuu ya Nchi Wakubwa wote Walikuwepo Wizara ilikuwepo lakini Ujenzi holela kila sehemu hakuna wa Kukemea
Na cha kusikitisha ni kua bado wanaendelea kubweteka na hali ya uharibifu ikiwa bado inaendelea. Hii wizara ni bure
 
Unaambiwa ubomoe kwasababu hujakata kibali cha ujenzi,bado ukifwata taratibu zote zakukata kibali cha ujenzi hukipati kwa wakati ukiuliza sababu za kuchelewa kwa kibali hupati majibu yakuridhisha.Hii hali inakera sana na inachangia vitendo vya rushwa.
 
Mipango miji ni idara tu, na wanafanya kazi chini ya mkurugenzi wa jiji/manispaa/halmashauri.

Suluhisho hapa, ni kuwa na wakurugenzi wenye maono; ambao watashusha majukumu kwa idara inayohusika na mipango miji.

Na idara husika itafanya majukumu yake.​
 
Unaambiwa ubomoe kwasababu hujakata kibali cha ujenzi,bado ukifwata taratibu zote zakukata kibali cha ujenzi hukipati kwa wakati ukiuliza sababu za kuchelewa kwa kibali hupati majibu yakuridhisha.Hii hali inakera sana na inachangia vitendo vya rushwa.
Nilishawahi timua mmoja kidogo ale Tofali ya kichwa nipo site mafundi wanapiga ripu anapita tu kwenye matembezi yake nashitukia kaandika simamisha Ujenzi. Nilimtoa nduki Ile mbaya. Sitakagi ujinga. Nilimuuliza swali nani anawajibika kupima viwanja. Akasema ni yeye.

Swali la pili mbona hapa hamjapapima? Tuko kwenye mchakato.

Kosa la nani Sasa. Ilitakiwa niwe na kibali. Swali jingine mbona mmekaa hamjapima huku watu wanaendelea kujenga. Hamnuoni hayo ni makosa yenu. Akaanza kujikanyaga tu. Kilichofata hapo alikijua. Tangu siku hiyo sijawahi kumuona tena

Sent from my TECNO KG6 using JamiiForums mobile app
 
Bajeti yao ni ndogo, vitendea kazi na wataalamu hawatoshi kwa ajili ya kupima matumizi ya ardhi.

Waje na mipango endelevu ili kunusuru miji mingi kuwa na makazi yenye ujenzi holela.
 
Bajeti yao ni ndogo, vitendea kazi na wataalamu hawatoshi kwa ajili ya kupima matumizi ya ardhi.

Waje na mipango endelevu ili kunusuru miji mingi kuwa na makazi yenye ujenzi holela.
Sababu inaweza kuwa ni bajeti; ilakama nia ipo, wanaweza kuingia ubia na sekta binafsi katika upimaji, na mambo yakaenda vizuri na kwa haraka.
 
Shida Wananchi wanakimbia Serikali inatembea.

Mfano huku Mbeya ni maeneo machache sana yamepimwa huku mipango miji wakicheka
 
Halafu waambie na bei wanazopanga baada ya kupima sio halisi.

Wataje bei kulingana na uhalisia ila sio skyrocketing price zisizo na kichwa Wala kwa miguu.

Ili wananchi wengi waweze kumudu na kuondokana kwa makazi holela.

Yaani unakuta kiwanja kabla ya kupimwa kilikuwa na thamani ya shilingi 900,000.
Gharama ya kupima hata ikiwa asilimia 50% hakiwezi kuuzwa Milioni 6 au 7
 
Juzi kati hapa walipita mitaa ya madale, wazo, mashamba ya jeshi waliwawekea sana watu x...sjui simamisha ujenzi etc
Ila naona ni njia ya kujipatia pesa
Watu wafanye malipo kulipia fine

Ila mipango miji hawafanyi kazi ipasavyo maana licha ya watu kujenga
Lakini maeneo wanayojenga watu yanakuwa kama squatter sasa
Maana mipango miji haisimamiwi

Hii nchi ngumu kuanzia juu mpaka chini

Ova
 
Juzi kati hapa walipita mitaa ya madale, wazo, mashamba ya jeshi waliwawekea sana watu x...sjui simamisha ujenzi etc
Ila naona ni njia ya kujipatia pesa
Watu wafanye malipo kulipia fine

Ila mipango miji hawafanyi kazi ipasavyo maana licha ya watu kujenga
Lakini maeneo wanayojenga watu yanakuwa kama squatter sasa
Maana mipango miji haisimamiwi

Hii nchi ngumu kuanzia juu mpaka chini

Ova
Watu wa Wazo waliwekewa X kwenye nyumba zao kwa makosa gani mkuu?
 
Back
Top Bottom