Hivi dini ni imani au ni jina?

Hivi dini ni imani au ni jina?

Sio lazima kwa aliyesilimu kubadili jina lake anaweza kubaki na jina lake la kabla ya kusilimu, ila inapendeza zaidi akachagua katika majina mazuri ya Kiislam.

Vile vile kuna kuna majina mtu hatakiwi kujiita au kuitwa katika Uislam. Mifano nimetoa katika comment yangu hapo juu. Sasa kama mtu amesilimu na kabla ya kusilimu alikuwa akiitwa jina ambalo katika Uislam halifai analazimika kubadilisha. Na hata kama ni Muislam aliyepewa jina ambalo halifai na wazazi au walezi wake mfano lina shirki ndani yake, analazimika kujibadilisha akijua hilo.

Nikakupa na mifano mfano mmoja ni wa Swahaba Abu Hurayrah (Radhiya Allahu 'Anhu), kabla ya kusilimu alikuwa akiitwa 'Abdush-Shams (Mja wa Jua). Aliposilimu, Mtume ( Swalla Allahu 'Alayhi Wa Sallam) akambadilisha akamuita 'Abdur-Rahmaan (Mja wa Mwingi wa Rahma).

Nadhani hapo utakuwa umenielewa kidogo dada yangu.

Allah akubariki na azidi kukuongoza katika Haqq wewe na sisi sote.
Umesema kweli kabisa.
 
Sawa tunatakiwa.kuwa na majina mazuri..Sasa nikuulize jina Ben Ni baya?..

Mtu kubadili dini Natakiwa nianze kuap.kwa wanasheria kubadili vyeti vyangu vyote na documents ?

Mnasema Dini Ni nyepesi..huoni.huu.mchakato.mzima.wa kuaapa na nk... Inafanya Mambo yawe magumu..

Kabadili jina Inafaida gani katika dini ya Uislamu?...Je nikibadili jina ndo napendwa na Allah...Au Ni matendo yangu na bidii yangu ya kujifunza Dini na kufanyia kazi Elimu yangu?

Mnafanya mamabo magumu..wakati dini Ni nyepesi.

mtu.kuwa mchamungu haina uhusiano na Jina lake...Ndo maana.mimi watoto Wangu nawapa.majina ya.kikabila...sioni sababu ya kuwaita hayo.majina ya Kiarabu eti ndo watakuwa wachamungu.
Unayajuaje majina ya Kiarabu bibie ?

Naomba nikuulize swali, jina la "Ben" lina maana gani ?

Dini nyepesi na wewe nilivyokuona katika mada hii unaifanya dini iwe ngumu, ndiyo maana hili limekushinda. Mangapi magumu na yana mlolongo mrefu lakini mnayafanya ila hili la Dini unaliona gumu wakati si gumu. Fata utaratibu kisha kuwa na subira.

Mtume alisema "Dini ni nyepesi na atakaye ifanya kuwa ngumu, basi itamshinda" (Au kama alivyosema Rasul). Sasa angalia isije kukushinda.

Ngoja nikupe faida tu kidogo, majina yote ya mitume si ya Kiarabu isipokuwa majina manne tu (Hayazidi hapo).
 
Nimeitikia wito kaka.

Hadithi imekuja, inatuhimiza ya kuwa tuwape watoto wetu majina mazuri, na mtume akataja majina kama vile "Abdillah na Abdulrahman". Jina Abdulrahman ni zuri sana kuliko majina ya kikabila, sababu lina maana.

Kuna majina mazuri na kuna majina mabaya,mtume wa Allah alikuwa anawabadilisha watu majina ambayo yalikuwa mabaya na yenye shirki ndani yake.

Ila kama jina lina maana nzuri halina haja ya kulibadili, na wapo watu wengi walikuwa Wakristo walipo ingia katika Uislamu hawakubadili majina ya wazazi wao. Hapa wapo watu walikuwa wakiingia Uislamu wanabadili mpaka majina ya wazazi wao na hili ni kosa, ila jina la mwanzo unaruhusiwa kubadili. Sababu mzazi wako habadiliki. Mfano kuna brothers kobao unamkuta anaitwa "Bilal Davis" au "Musa Richardson" na mfano wake.

Utaratibu mzuri wa kuwapa watoto majina ukisoma kitabu kiitwacho "Tasmiyaat al Mawluud" ameelekeza umpe mtoto wako majina ya mitume, wake zao, watoto zao, ukikosa huko wape majina ya maswahaba au walio wafata maswahaba yaani kwa ujumla majina ya wajawema. Huu ndiyo utaratibu mzuri, na huwezi kukosa majina mazuri huko.

Mimi watoto wangu siwezi kuwapa majina ya kikabila sababu mengi hayana maana, na majina mazuri yako mengi.
Minaitwa Kagemlo..manayake nzuri TU..Sasa nilibadili niitwe Hafsa..ndo ili iwe Nini..au Aisha mke wa mtume..Au Khadija
Yaaani kwajina Hilo ndo Dini yangu itakuwa imekamilika..
 
Unayajuaje majina ya Kiarabu bibie ?

Naomba nikuulize swali, jina la "Ben" lina maana gani ?

Dini nyepesi na wewe nilivyokuona katika mada hii unaifanya dini iwe ngumu, ndiyo maana hili limekushinda. Mangapi magumu na yana mlolongo mrefu lakini mnayafanya ila hili la Dini unaliona gumu wakati si gumu. Fata utaratibu kisha kuwa na subira.

Mtume alisema "Dini ni nyepesi na atakaye ifanya kuwa ngumu, basi itamshinda" (Au kama alivyosema Rasul). Sasa angalia isije kukushinda.

Ngoja nikupe faida tu kidogo, majina yote ya mitume si ya Kiarabu isipokuwa majina manne tu (Hayazidi hapo).
Mi naona nyie ndo mnaifanya ngumu kwa kulazimishana kubadilisha majina.

jina Kama nizuri na liachwe...Focus na kumfundisha huyu aliesilimu Dini..aijue na ikamfae...Sio kubadilishana majina eti Ndo ukamilifu wa Dini.

Ben linaweza kuwa jina la mtu mwema pia...kwani mtu mwema lazima awe mtume?
 
Minaotwa Kagemlo..manayake nzuri TU..Sasa nilibadili niitwe Hafsa..ndo ili iwe Nini..au Aisha mke wa mtume..Au Khadija
Yaaani kwajina Hilo ndo Dini yangu itakuwa imekamilika..
Nipe maana ya hilo jina lako, la kwanza na la pili.

Pili, watu wenye akili timamu huwa wanapenda vizuri bila kuangalia umimi. Mathalani wewe hapo huna hoja ya kielimu ya kuyakataa majina ya waja wema, zaidi ya umimi.

Tatu, Hafsa ni jina zuri na lina historia nzuri, na halikuongezei chochote wala kukupunguzia chochote, ila utapata thawabu kwa kumtii mtume wa Allah aliye juu.

Nne, uzuri ulioje kujiita jina la mtu ambaye ametabiriwa pepo na jina la mke wa mtume ? Majina yao ni mazuri na ni watu wa kheri na utalipwa kwa ajili ya kumtii mtume.

Kuna ujinga fulani waislamu wengi wako nao, unakuta wanaogopa kuwaita watoto wao majina ya Kiislamu wakihofia maisha wengine wakihofia watoto wao kuonekana Waislamu, basi ndiyo udhalili unawakuta.
 
Nipe maana ya hilo jina lako, la kwanza na la pili.

Pili, watu wenye akili timamu huwa wanapenda vizuri bila kuangalia umimi. Mathalani wewe hapo huna hoja ya kielimu ya kuyakataa majina ya waja wema, zaidi ya umimi.

Tatu, Hafsa ni jina zuri na lina historia nzuri, na halikuongezei chochote wala kukupunguzia chochote, ila utapata thawabu kwa kumtii mtume wa Allah aliye juu.

Nne, uzuri ulioje kujiita jina la mtu ambaye ametabiriwa pepo na jina la mke wa mtume ? Majina yao ni mazuri na ni watu wa kheri na utalipwa kwa ajili ya kumtii mtume.

Kuna ujinga fulani waislamu wengi wako nao, unakuta wanaogopa kuwaita watoto wao majina ya Kiislamu wakihofia maisha wengine wakihofia watoto wao kuonekana Waislamu, basi ndiyo udhalili unawakuta.
Sijasema hayo Ni majina mabaya.. lakini haimzuii mtu kumuita mwanaye. ..kwa mfano mamayangu Mimi namuona Ni mtu mwema nikimuita Mwanangu Karen... Sio lakiislamu Kama mnavyodai.. je ntakuwa na kosea Hadi nimuite Hidaya..au Sakina?
 
Ukienda kule mbeya ambako asilimia kubwa wakristo wametawala, mambo yapo tofauti kidogo. watu wamepewa majina sio kwa itifaki ya kidini ni basi tu mzazi alikua na feeling nalo akapenda mwanae aitwe hivyo.

Wapo wakristo wengi wamepewa majina na wazazi wao toka utotoni ambayo yanatafsirika kama ni majina ya muumini wa kislam. mfano zuberi hadija, ramadhani, hamisi, bakari, masudi, abdala, iddi nk.
 
Mi naona nyie ndo mnaifanya ngumu kwa kulazimishana kubadilisha majina.

jina Kama nizuri na liachwe...Focus na kumfundisha huyu aliesilimu Dini..aijue na ikamfae...Sio kubadilishana majina eti Ndo ukamilifu wa Dini.

Ben linaweza kuwa jina la mtu mwema pia...kwani mtu mwema lazima awe mtume?
Hakuna sehemu mtu amelazimishwa kubadili jina au majina, ila kuna zuri na zuri zaidi, na mtu makini huwa anafata lile zuri zaidi.

Na hata ukimfundisha dini akajua, lazima ipo siku tu atabadilisha jina. Historia ina badili sana mitazamo ya watu na kuwafanya watu wawapende waja wema. Hili tunaliona, na wengi wao huishia kubadili majina yao na kutumia majina ya waja wema.

Nimekuuliza swali nini maana ya jina "Ben" ? Unaniuliza tena swali, swali lako linaonyesha ya kuwa hujui maana ya jina hilo. Kadhalika hakuna sehemu niliyo kwambia mtu mwema ni mtume peke yake, laiti kama ungekuwa umesoma nilichokiandika, hili usingeliandika.
 
Hauwezi ukawa muislam alafu ukaitwa Paulo.
Au ukawa mkristo ukaitwa Hassan.
Yaani hainogi.unaweza siku ukapata matatizo watu wakashindaa kukusaidia.
Au unaweza ukaenda sehemu ukafa.
Watu wanakuja una jina la kikristo kumbe muislam.
Mwisho wa siku utazikwa kikristo wakati ni muislam
Utakua unakosea, nje ya eneo lako mambo hayako hivyo
 
Sijasema hayo Ni majina mabaya.. lakini haimzuii mtu kumuita mwanaye. ..kwa mfano mamayangu Mimi namuona Ni mtu mwema nikimuita Mwanangu Karen... Sio lakiislamu Kama mnavyodai.. je ntakuwa na kosea Hadi nimuite Hidaya..au Sakina?
Kuna vitu huvielewi, hapa nakupa udhuru sababu ya kutokujua kwako.

Mtu ambaye yuko hai wema si wa "guarentee", maana yake anaweza kuamka mwema akalala muovu, akaamka muovu akalala mwema, yaani watu wanabadilika badilika. Kwa hoja ya kumuita mwanao jina la mama yako kisa ni mwema na bado yuko hai hii si sahihi, labda useme unamuita mwanao kwa ajili ya kumuenzi mama yako tu.

Utakuwa unakosea sababu unaenda kinyume na mtume.
 
Hakuna sehemu mtu amelazimishwa kubadili jina au majina, ila kuna zuri na zuri zaidi, na mtu makini huwa anafata lile zuri zaidi.

Na hata ukimfundisha dini akajua, lazima ipo siku tu atabadilisha jina. Historia ina badili sana mitazamo ya watu na kuwafanya watu wawapende waja wema. Hili tunaliona, na wengi wao huishia kubadili majina yao na kutumia majina ya waja wema.

Nimekuuliza swali nini maana ya jina "Ben" ? Unaniuliza tena swali, swali lako linaonyesha ya kuwa hujui maana ya jina hilo. Kadhalika hakuna sehemu niliyo kwambia mtu mwema ni mtume peke yake, laiti kama ungekuwa umesoma nilichokiandika, hili usingeliandika.
Dini Sio jina...TAFUTA kuijua Dini na kuielewa na kuiishi kwa vitendo.. hakuna sehem wanasema wanaoitwa Mohammed wataingia peponi kwa majina yao..japo Sio mbaya kumuita mtoto hivyo.

Nawanaoitwa Shida, Fitina au Masumbuko ..wataingia motoni.. japokuwa Hawa wenye hayo Majina wanaweza yabadili kwani si mazuri.

Nimemaliza
 
Karen... Sio lakiislamu Kama mnavyodai.. je ntakuwa na kosea Hadi nimuite Hidaya..au Sakina?
Karen maana yake nini ?

Ila haya majina mawili ya chini uliyo yataja yote yana maana tena maana zake ni nzuri, jina "Hidaya" maana yake ni "Uongofu" na jina "Sakina" maana yake ni "Utulivu".
 
Dini Sio jina...TAFUTA kuijua Dini na kuielewa na kuiishi kwa vitendo.. hakuna sehem wanasema wanaoitwa Mohammed wataingia peponi kwa majina yao..japo Sio mbaya kumuita mtoto hivyo.

Nawanaoitwa Shida, Fitina au Masumbuko ..wataingia motoni.. japokuwa Hawa wenye hayo Majina wanaweza yabadili kwani si mazuri.

Nimemaliza
Dini yetu imemaliza kila kitu, dini ni jina,kauli na vitendo.

Kwanza tamko lenyewe tu "Dini" ni jina. Shida yako bibie una umakini mdogo na uchachefu wa kung'amua hoja, unarudia kosa lile lile, hakuna aliyesema hayo unayo yasema, nalukosoa kila muda lakini unarudia kosa lile lile.

Shida, masumbuko na kadhalika ni katika majina mabaya, na hata walio waita majina hayo hukiri waliwaita watoto zao ka ujinga. Mwanadamu hupenda vizuri, sasa usirudie kosa hili, nimekwambia lazima ufanye mambo kwa kumtii mtume na ukimtii mtume ndiyo kufaulu, sasa wewe huelewi unarudia kosa lile lile.

Ahsante kwa kumaliza kwako, ila nakusihi ukiwa unasoma hoja ielewe na unapokosolewa kubali kukosea, kwani hupungukiwi na kitu zaidi ya kujifunza na kuonyesha utimamu.

Nilikuwepo...
 
Napataga kigugumizi sana nikisikia mtu kabadili dini kisha anabadilisha na jina,eti jina la kiislam au la kikristo.

Kwani ukibaki na jina lako na kuendelea na ibada za kumuabudu Mungu kwani haikubaliki? Nimebahatika kwenda Japan,China na Russia. Nimekuta kuna waislaam wengi na wakristo, ila sijakuta mtu anaitwa Muhammad au William.

Kumjua mtu dini yake hadi umuulize lakini sio kwa jina. Sasa tunaomini hivyo tunakwama wapi?
Dini ni mfumo wa kuamini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Napataga kigugumizi sana nikisikia mtu kabadili dini kisha anabadilisha na jina,eti jina la kiislam au la kikristo.

Kwani ukibaki na jina lako na kuendelea na ibada za kumuabudu Mungu kwani haikubaliki? Nimebahatika kwenda Japan,China na Russia. Nimekuta kuna waislaam wengi na wakristo, ila sijakuta mtu anaitwa Muhammad au William.

Kumjua mtu dini yake hadi umuulize lakini sio kwa jina. Sasa tunaomini hivyo tunakwama wapi?
Dini ni vyote hivyo.
 
Dada yangu, ni vizuri kwa mtu aliyesilimu kuchagua jina la Kiislam kwa ajili ya utambulisho wake lakini pia tumeambiwa tuchague majina mazuri.

Pia kuna wakati mtu atalazimika kubadili jina mfano mtu anayetumia jina katika majina ambayo ni maalum kwa Allah tu. Mfano mtu kuitwa Al-Khaaliq (Muumba) au Ar Razzaq (Mwenye Kuruzuku). Hii haifai.

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimbadilisha mtu aliyesilimu aliyekuwa akiitwa Abul-Hakam (baba wa Hukumu) akimwambia kuwa Allaah Pekee Ndiye Mwenye sifa hiyo ya Al-Hakam, na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamuuliza kama ana watoto na majina yao, yule mtu akataja wanawe watatu, Shurayh, Muslim na 'Abdullaah. Basi Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: “Kuanzia leo wewe ni Abuu Shurayh.” [Abu Daawuwd].

Ni vyema kuwaita watoto au kuwaita watu (mfano aliyesilimu) kwa majina ya Allah kwa kufuatanisha na neno 'Abd (Mja). Mfano kumuita mtu 'Abdur-Razzaaq (Mja wa Mwenye Kuruzuku) au 'Abdu-Allah (Mja wa Allah).

Inafaa kwa mtu kutumia majina ambayo ni sifa za Allah lakini pia ya WanaAdamu kama vile Maalik (Mfalme).

Haifai pia mtu kujiita au kuitwa 'Abdur-Rasul (Mja wa Mtume) au 'Abdun-Nabbiy (Mja wa Nabii) au 'Abdul-Hussain (Mja wa Hussain), kwa sababu uja ni wa Allah pekee na si wa kiumbe chochote. Majina yenye Shirki hayafai. Hata Swahaba Abu Hurayrah alikuwa akiitwa 'Abdush-Shams (Mja wa Jua) lakini aliposilimu Mtume alimbadilisha jina akamuita 'Abdur-Rahmaan (Mja wa Mwingi wa Rehma)


Mtu Mwenye jina lenye maana mbaya pia halifai. Na Uislam unamruhusu mtu kubadilisha jina lolote lenye maana mbaya hata kama alipewa na wazazi wake.

Mengi katika niliyoandika nimeyatoa Alhidaaya.com.


Soma pia yafuatayo kwa faida zaidi;


Fiqh Ya Kuwaita Majina Watoto

Jamii

Fiqh Ya Majina Ya Watoto



www.alhidaaya.com





Ni Sunnah kutunza jina zuri, na katika majina mazuri ni:



'Abdullaah (Mja wa Allaah Subhanahu wa Ta'aala)

na

'Abdur-Rahmaan (Mja wa Mwingi wa Rahmah);



na majina ya ki kweli hasa ni:



Al- Haarith (Anayezaa)

na

Humaam (Hodari);



na majina mabaya zaidi ni:



Harb (Vita)

na

Murrah (Chungu)





Hadiyth ifuatayo imethibitisha:



((Majina yanayopendezewa kwa Allaah (Subhaana wa Ta'aala) ni 'Abdullaah na Abdur-Rahmaan.)) [imeripotiwa na Muslim.





Kwa Abu Daawuud kuna nyongeza((Na majina ya ki kweli hasa ni Al-Haarith na Humaam, na mabaya zaidi ni Harb na Murrah)).





Na majina mabaya, na yale ambayo yanamaanisha vitu vibaya katika kutokuwepo kwao, ni makuruhu (Yasiyopendeza), kama vile:



Nujayh (fanikiwa),



Barakah (baraka),



Kulayb (kijimbwa),



Harb (vita),



Murrah (chungu),



Shihaab (kimondo),



Himaar (punda),



Aflah (fanikiwa sana),



Yasaar (wepesi),



Rabaah (faida), na



Naafi` (kunufaika)



na majina kama:



Sittun-nisaa (mwanamke wa wanawake wote) ni yanayogombezewa sana.



Na Mfalme wa Wafalme limekatazwa, kama ilivyokuwa:



'Shahenshaah',



na



Aqdhwaal-Qudhwaat (hakimu wa mahakimu).





Na inapendelewa kubadilisha majina mabaya na ambayo yanamaanisha vitu vibaya katika kutokuwepo kwao.





Na inapendelewa kwa mtoto wa kiume, mwanafunzi au mfanyakazi kutomwita kwa jina lake, na kwamba watu wazuri (wanaume na wanawake) wawe wana kun-yah, hata ikiwa hawana watoto wa kiume, na kun-yah huhusiana na mtoto wa kiume wa mwanzo.





Na imekatazwa kuwa na Kun-yah ya 'Abul-Qaasim kwa mtu ambaye jina lake ni Muhammad na vile vile kwa watu wengine, katika kipindi cha Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na vile vile baadae ya hapo.





Tanbihi:



Kuna khitilafu baina ya madhehebu juu katika nukta hii- wengine wameshika kwamba katazo lake (kutumia kun-yah ya Abul-Qaasim) liliwekwa katika kipindi cha uhai wa Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) tu na si baada ya kufariki.





Na aliyeruka mipaka (faasiq) au mzushi asipewe kun-yah mpaka kukiwepo hofu ya fitnah, au ikiwa kwa sababu ya utambulishi, (kama vile Abu Lahab).





Na inapendelewa kwamba mtu asitumie kun-yah yake pekee (yaani bila ya kutimiza jina lake pia), isipokuwa akiwa anajulikana kwa kun-yah yake na sio kwa jina lolote isipokuwa hilo.





Na pia imekatazwa (Haraam) kumtania mtu kwa jina ambalo halipendi. Kama ikiwa anajulikana kwa jina jengine (ambalo halimchukizi) na hata kama jina hilo lina dhamiria kitu ambacho kinamhusu yeye ambacho ni cha kweli.





Kun-yah (Lakabu au Jina la kupachika)

Ushahidi uliombwa wa kuchukuliwa kun-yah kuwa ni Sunnah. Kuna vidokezo mbali mbali juu ya hili katika Hadiyth.





Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa na kun-yah, na hakuna ushahidi wowote wa kuonyesha kwamba kuwa na kun-yah ilikuwa kwa yeye pekee, na hii ndio inayoamua ni Sunnah (kumfuata mtu katika kitu ambacho hakikua kwa ajili yake pekee (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).







Zaidi, kuna Hadiyth iliyoripotiwa na At-Tirmidhiy katika "Ash-Shamaail"





Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwita mvulana mdogo kwa kun-yah, kuonyesha kwamba si muhimu kuwa na mtoto kabla ya kutumia kun-yah.





Mazungumzo zaidi ya Hadiyth hizi yanapatikana katika Fat-h al-Baariy (maelezo ya Swahiyh Al-Bukhaariy).
Mkuu hivi uzuri wa jina upo wapi? ni kwenye maana au the way linapo tamkwa?

Mi naona kipimo cha uzuri au baya wa jina mi nadhani haupimwi kwa namna ambavyo linatamkwa au kwa kujenga dhana ya kuona kwamba jina lenye asili kutoka lugha fulani yenye watu ambao nchi yao inahistoria ya kukaliwa na mitume kua ni bora zaidi

Mfano kuna teacher kanifundisha alikua anaitwa "tuntufye" kwa mtazamo wako hilo jina ni lazima useme baya, lakini deeply lina maana nzuri tu ambayo inaweza kukushawishi hata wewe ukapendezewa nayo
 
God does not exist na kwakuwa Mungu hayupo watu wa jamii hisika wanaishi kulingana na tamaduni walizozoea nyinyi mnaita dini ukiwa muislam utafata tamaduni za warabu mpk majina na ukiwa mkristo utafata tamaduni za wazungu mpk majina kwakuwa mnafata tamaduni zao hivyo Dini ni utamaduni wa jamii fulani
 
nashukuru
Elimu yangu katika dini bado ni ndogo mno dada yangu. Ngoja nijaribu kuwaita baadhi ya watu ambao nawadhania kuwa ni wenye elimu kidogo ya dini wakufafanulie zaidi InshaAllah. Cc Jurjani Abuu Dharr Kazakh destroyer
nashukuru kwa kuniita mkuu......kaka jurjani amemaliza kila kitu hapo chini..
allah akubariki na akuingize firdaws siku ya qiyamah pamoja na manabii na wakweli na mashuhadaa na watu wema na uzuri ulioje wa marafiki hao..
 
Nimeitikia wito kaka.

Hadithi imekuja, inatuhimiza ya kuwa tuwape watoto wetu majina mazuri, na mtume akataja majina kama vile "Abdillah na Abdulrahman".

Kuna majina mazuri na kuna majina mabaya,mtume wa Allah alikuwa anawabadilisha watu majina ambayo yalikuwa mabaya na yenye shirki ndani yake.

Ila kama jina lina maana nzuri halina haja ya kulibadili, na wapo watu wengi walikuwa Wakristo walipo ingia katika Uislamu hawakubadili majina ya wazazi wao. Hapa wapo watu walikuwa wakiingia Uislamu wanabadili mpaka majina ya wazazi wao na hili ni kosa, ila jina la mwanzo unaruhusiwa kubadili. Sababu mzazi wako habadiliki. Mfano kuna brothers kobao unamkuta anaitwa "Bilal Davis" au "Musa Richardson" na mfano wake.

Utaratibu mzuri wa kuwapa watoto majina ukisoma kitabu kiitwacho "Tasmiyaat al Mawluud" ameelekeza umpe mtoto wako majina ya mitume, wake zao, watoto zao, ukikosa huko wape majina ya maswahaba au walio wafata maswahaba yaani kwa ujumla majina ya wajawema. Huu ndiyo utaratibu mzuri, na huwezi kukosa majina mazuri huko.

Mimi watoto wangu siwezi kuwapa majina ya kikabila sababu mengi hayana maana, na majina mazuri yako mengi

Uwe unaandika mambo ambayo ukiombwa ushahidi unaweza kutupa. Siyo unaandika huu ujinga ambao mpaka unakufa huwezi kuuthibitisha.
Issa alizaliwa chini ya mtende wakati Yesu alizaliwa katika banda la mifugo.
Issa hakufa wakati Yesu Kristo alikufa na kufufuka na kupaa mbinguni.
 
Sasa Kama wewe NI muislam lakini kwenye vitambulisho vyako umeandika majina ya kikristo.
Unaweza ukaanguka sehemu ukafa na haujulikani .watu wakakuokota kuangalia vitambulisho vyako umeandika majina ya kikristo kumbe wewe ni muislam. HAUONI KAMA UTAZIKWA KIKRISTO?.
pili unaweza ukaenda kutembelea sehemu kuna wakristo wakapika kitimoto Ila kwa kuwa jina ulilowatajia ni la kikristo wakaona NI mwenzao kumbe umeshabadili DINI unaletewa kitimoto UNAKULA kumbe wewe ni muislam.
Lakini ukibadili dini na jina unawapa watu nafuu ya kukufahamu zikitokea emergency Kama hizi NI RAHIS KUSAIDIWA.
Utakua unakosea, nje ya eneo lako mambo hayako hivyo
 
Back
Top Bottom