Ushauri wangu (japo wanaume hawataupenda) ni kuwa jipende kupita maelezo...
Kama mwili umebadilika sababu ya watoto fanya mazoezi...
Yani jipende kweli kweli...
Tafuta ela...kuwa independent..tena hata ela ya watoto usimuombe...lakini omba talaka ili uwe huru
Who knows unaweza pata partner wa kumalizia siku zilizobaki duniani...
Usikubali partner kijana (sharobaro)...wala mume wa mtu...tafuta alofiwa na mke...ila mkapime afya...
Wanaume wengi jeuri yao ni kuona wake zao wamezeeka sababu ya kuwa na watoto...
Kuwakomoa ni kuwaonyesha kuwa uzee mwisho Msata...
Hivi nani atakubali kuoa mwanamke na watoto watatu? Je, kama na huyo mwanaume ana watoto si muungano tata kama muungano wa Tanzania siku za usoni?
Mkuu labda huko kwenu... Huku kuna mwanaume alifunga ndoa na mwanamke ana watoto 6, tena wawili tu ndio wa baba mmoja na waliobaki kila.mtu na baba yake. Walipendezaje??
Ushauri wangu (japo wanaume hawataupenda) ni kuwa jipende kupita maelezo...
Kama mwili umebadilika sababu ya watoto fanya mazoezi...
Yani jipende kweli kweli...
Tafuta ela...kuwa independent..tena hata ela ya watoto usimuombe...lakini omba talaka ili uwe huru
Who knows unaweza pata partner wa kumalizia siku zilizobaki duniani...
Usikubali partner kijana (sharobaro)...wala mume wa mtu...tafuta alofiwa na mke...ila mkapime afya...
Wanaume wengi jeuri yao ni kuona wake zao wamezeeka sababu ya kuwa na watoto...
Kuwakomoa ni kuwaonyesha kuwa uzee mwisho Msata...
Duh...!!
Huna watu wa ukweli unaofahamiana nao ambao unaweza ukawaeleza masahibu ya ndoa yako hadi uje humu kwa mazimwi......
Wana jamvi naamini mu wazima wa afya.
Nimeolewa miaka nane iliyopita na tumebahatika kupata watoto watatu,tangu nimeolewa hiyo miaka naweza sema nimeishi na mume wangu miaka mitatu,namaanisha ki-ndoa.Maisha ya ndoa yetu naweza sema ni ya ajabu sana kwa jinsi nionavyo mimi.
Mume wangu akinikosea huwa ninatabia ya kununa ili aniombe msamaha,na kwasababu mwanaume kuomba msamaha ni ngumu huwa nahitaji basi hata kutambua tu kosa lake. Lakini kwa mwenzangu imekua ni vigumu, nikinuna nae huwa ananuna.
Miaka mitano iliyobaki tumeishi maisha ya kununiana mpaka hivi leo hatuongei. Mnuno wa mwisho sababu yake nilimgundua anatembea na binti mmoja na kwa ushahidi, lakini hakujutia wala kuomba msamaha, badala yake nilinuna nae akanuna yapata mwaka mmoja sasa, tumelala kitanda kimoja hanigusi wala simgusi, mpaka sasa kakimbia nyumba, kaniacha mimi na watoto ikafikia hatua akakataa kutoa pesa ya chakula ikabidi nikamshitaki kwa wazee, ila ilishindikana, wazee wakaniambia nimpeleke mahakamani, hivi sasa anatoa ela ya chakula kwa amri ya mahakama ingawa hapendi.
Wanaume mkigombana na wake zenu muwahudumie watoto wenu maana ni wenu,baada ya kusema maneno haya kifua changu kimepumua na ninaamini kuanzia leo nitakula chakula vizuri na kuanza maisha mapya.
Usitukane wala usidharau maana ni dukuduku langu la muda sasa nitarudi kutumia id yangu ya siku zote.
Asanten
INASIKITISHA JAMANI SOMA HII! Baba na
mama baada ya kurudi kazini pamoja wakakuta
BARUA iko mezani SEBULENI ikisema.... "Baba
na mama, ni matumaini yangu kuwa mtasoma
ujumbe wangu huu kwenye karatasi niliyoiweka
juu ya meza, naomba msishtuke maana ni
mambo ya kawaida kwenye maisha tunayoishi,
najua mtaumia kwa vile bado nasoma na ndo
nipo kidato cha kwanza..." Napenda
kuwajulisha kwamba sasa hivi mnaposoma hii
barua sipo nyumbani, nimetoroka maana
nimegundua nina uwezo wa kujitegemea kwa
sababu mimi ni kijana mwenyewe umri wa miaka
14 na ninajua kipi chema na kipi kibaya. Tangu
mwezi mmoja uliopita nilikuwa na uhusiano na
binti mmoja aliyeitwa Rachel, mwenye umri wa
miaka 27 na kwa sasa ndo naishi naye kwenye
chumba alichopanga. Nilipokuwa nyumbani
sikuwa napata hela za kutosha ila sasa
nimeanza kushika noti za shilingi 10,000...
Msichana niliyenaye ni mzuri sana wa umbo na
ninampenda sana, amenifundisha njia za
kutafuta hela. Amenipangia kazi ya kuuza
madawa ya kulevya na yeye ikifika usiku
anaenda kuuza mwili wake, basi kila siku
tunapata hela ya kutosha, huyu mchumba
wangu ni msichana mwenye bidii, kwa siku
analala masaa 6 tu maana mwanaume yeyote
akija lazima awe naye chumbani kwa muda wa
masaa 3. Msiwe na hofu, nipo salama kabisa
na nimeamua kumwoa Rachel mana ni kila kitu
kwangu. Pia amenunua gari la kubebea mbao
kwa hiyo biashara inakwenda vizuri, Rachel
amekwenda kupima afya na amekutwa na
upungufu wa kinga mwilini, mara nyingi
namridhisha anapotaka kitu fulani, iwe kufanya
naye mazoezi ya viungo au kufanya naye
mapenzi, si mnajua unapokuwa na mgonjwa
unatakiwa kuwa naye karibu, ila mimi pia
sijihisi vizuri
maana kila saa nakohoa tu na sina uhakika
kama nimeathirika. Tumepanga baada ya miaka
miwili tutawatembelea, nadhani mpaka miaka
miwili iishe atakuwa ameshajifungua, na ni
furaha yangu mtamwona mjukuu wenu. Wazazi
wangu sina la kuongeza kwaherini Mungu
akipenda tutaonana. N.B: "Baba na mama, mimi
nipo chumbani kwangu najisomea,
mnachokisoma ni home work ya mwalimu wa
kiswahili alituambia tutunge hadithi fupi ya
kusisimua, naomba muiangalie kama kuna
makosa!"
Kuolewa ni rahisi ila watoto wakikua hapo ndo muziki unogile.....Kila mtoto anajipambanua kwa ubini na Mama anaanza kuside na watoto aloolewa nao. Kukiwa na kidume ndicho kinaharibu mambo yote. Na kwa huyu mwanaume kama atakuwa na mtoto wa kike, akiwa mkubwa kunachimbika kwa mama wa kambo. Jamani angalia familia muungano zilivyo uzeeni. Unless Baba ana watoto wa kiume tu na mama ana wa kike tu (ingawa mbele ya safari si ajabu kukuta wajukuu wa ndani)wakati mie nina watoto 4 na natafuta mchumba
umenchekesha sana
tena huyo anao wa baba mmoja anaolewa kabisas
Nimeupenda ushauri
Ni kweli tena ni mzuri tu wa kuperuzi humu, anaweza akasema na yeye
Kwa hiyo na wewe ni mmoja wa mazimwi wa humu.Duh...!!
Huna watu wa ukweli unaofahamiana nao ambao unaweza ukawaeleza masahibu ya ndoa yako hadi uje humu kwa mazimwi?
Ila cha muhimu ni wewe kujiskia vizuri. Kwa hiyo kama umejisikia vizuri kwa kufunguka humu basi haina shida.