Wana jamvi naamini mu wazima wa afya.
Nimeolewa miaka nane iliyopita na tumebahatika kupata watoto watatu,tangu nimeolewa hiyo miaka naweza sema nimeishi na mume wangu miaka mitatu,namaanisha ki-ndoa.Maisha ya ndoa yetu naweza sema ni ya ajabu sana kwa jinsi nionavyo mimi.
Mume wangu akinikosea huwa ninatabia ya kununa ili aniombe msamaha,na kwasababu mwanaume kuomba msamaha ni ngumu huwa nahitaji basi hata kutambua tu kosa lake. Lakini kwa mwenzangu imekua ni vigumu, nikinuna nae huwa ananuna.
Miaka mitano iliyobaki tumeishi maisha ya kununiana mpaka hivi leo hatuongei. Mnuno wa mwisho sababu yake nilimgundua anatembea na binti mmoja na kwa ushahidi, lakini hakujutia wala kuomba msamaha, badala yake nilinuna nae akanuna yapata mwaka mmoja sasa, tumelala kitanda kimoja hanigusi wala simgusi, mpaka sasa kakimbia nyumba, kaniacha mimi na watoto ikafikia hatua akakataa kutoa pesa ya chakula ikabidi nikamshitaki kwa wazee, ila ilishindikana, wazee wakaniambia nimpeleke mahakamani, hivi sasa anatoa ela ya chakula kwa amri ya mahakama ingawa hapendi.
Wanaume mkigombana na wake zenu muwahudumie watoto wenu maana ni wenu,baada ya kusema maneno haya kifua changu kimepumua na ninaamini kuanzia leo nitakula chakula vizuri na kuanza maisha mapya.
Usitukane wala usidharau maana ni dukuduku langu la muda sasa nitarudi kutumia id yangu ya siku zote.
Asanten