Mimi nimesema pale mwanzo kuwa "majina ya Makweta" ilikuwa jambo la kawaida sana enzi za mwalimu. Na ninajua wengi tu waliorudia na bado hawakupata nafasi za sekondari za serikali. Na unapaswa ukumbuke hapa kuwa tatizo hapa halikuwa ujinga wa repeater, lilikuwa uhaba wa nafasi za sekondari na utaratibu wa wakati ule wa mgao wa nafasi hizo. Ndiyo sababu neno lililokuwa likitumika ni "kuchaguliwa", na si "kufaulu". Na ndiyo sababu hata wale wengine ambao hawakuchaguliwa, kama pesa ilikuwepo walienda shule za private na huko walifaulu vizuri na kusonga mbele.
Labda mumseme huyu mheshimiwa kwa 'umaskini' aliokuwa nao wakati huo, maana hii ya kurudia ndiyo iliyokuwa njia pekee ya kumwezesha maskini kubahatisha elimu ya sekondari maana private zilikuwa hazishikiki. Na hiyo system ya mgao ilikuwa muflisi kabisa. Kule upareni watoto walikuwa wanafaulu kwa maksi za juu lakini hawachaguliwi kisa tu mkoa wa Kilimanjaro share yake ilikuwa fixed, hawawezi kupita zaidi ya waliopangwa. Kwa hiyo watu wakishakosa wanaenda Babati, Shinyanga, Tanga, Rufiji na kwingineko ambako wahusika walikuwa hawamalizi quota zao, yaani huko hata ukipata maksi nusu ya zile "ulizofeli" Same bado unachaguliwa. Na ndiko walikopatia watu majina tofauti na asili zao na wengine hata tofauti na dini zao. Na waliendelea kuonesha uwezo wao darasani hadi wakafika mbali tu, na wapo wengi.
Siku hizi hakuna justification ya kufanya hivyo maana nafasi za kusoma zinapatikana sana, na pia hakuna faida ya kung'ang'ania kupata shule ya serikali maana hizi za serikali siku hizi ni duni kuliko za private (enzi zetu kusoma shule ya serikali ndiyo ubingwa, haikutokea mtu kuacha shule ya serikali akasome private. Siku hizi shule za serikali zinakimbiwa kama vile zina *****!)
Hoja inayojadiliwa kuhusu mheshimiwa huyu kusomea jina la mtu mwingine haina tija yoyote, hasa ukizingatia mazingira ya wakati huo. Ingekuwa ameghushi cheti, au ingekuwa yule mwingine ndiye aliyefaulu halafu huyu bosi akapora, hapo kungekuwa na mjadala. Lakini wenyewe mnasema mtu aliacha shule, sasa kipi bora; nafasi ile ingepotea au mheshimiwa huyu alipoitumia na ikamfikisha hapo alipo? Hoja naiona ina sura ya kimajungu zaidi, haina tija.