Hili ni jaribio jingine kwa System/state au Kitengo!

Hili ni jaribio jingine kwa System/state au Kitengo!

Neno Alpha and Omega ni (JINA)la Mungu..yaani Mungu Muumba wa mbingu na nchi..na halipaswi kutumiwa kwa namna yeyote zaidi yakusema Yeye ni ALPHA NA OMEGA=Mwanzo na Mwisho.

hivyo kulitumia kwa style yako yakibinadam haikupasi wala haipaswi.Mungu akuumbie moyo safi wakumjua yeye pasi kumchanganya..asante.
 
Sytem isio na malengo au mikakati ya kuweka maslahi ya wananchi na nchi kwa ujumla ni sytem mbovu.System huongozwa na watu,hao watu uweledi wao au upuuzi wao ndio jibu la system.Kwa hali ya sasa sijui kama kuna system yenye viwango vinavyokubalika au kuheshimika kwa umma wa watanzania.Ovehaul the system first.
 
ugumu wa safari hii system inaonekana kugawanyika..haifanyi kazi kwa umoja wake kama miaka hiyo uliiyoitaja.....uwezekano wa kufail ni mkubwa mno....kubwa zaidi ni kuhushuhudia vipande viwili vya system vikiwa na malengo tofauti...kimisingi ni tunashuhudia watu wawili wenye ushawishi wa dola wakigombana......yupo mwenye ushawishi binafs na yupo aisye na ushawishi binafs lakini analindwa na mfumo
 
Najaribu kufikiri hapa ukute lowasa, slaa, mbowe, marando, lipumba, wote ni system lengo lao nini? Wanatarajia kutoa kitu gani ndani ya siasa tanzania kuelekea uchaguzi? Je kuna system nyingine nje yao? Nao wanafanya nini wanatarajia kutoa nini kuelekea uchaguzi mwaka huu 2015?
 
System ya Tanzania imefeli siku nyingi sanaa . Kwanini imeshindwa kuzuia ufisadi, kwanini imekubali Balali afe kifo cha uongo ? Kwanini imekubali Riz 1 achague viongozi anaowataka, Kwanini haijahakikisha mchakato wa kila chama wa kupata viongozi wake haubakwii na wenye tamaa ya kupata dola ?

System ya Tanzani inahitaji overhaul . Shilingi kushuka thamani kwa kasi ni kushindwa kwa System pia !
 
Tatizo la muandishi ni moja tu kufananisha system na Mungu.Hapo ndipo nimeweka walakini maana system kuna kipindi inakorofisha au inafeli na matengenezo madogo au makubwa yanatokea ,,sasa sijui alikuwa anamaanisha Mungu naye anafeligi na anahitaji marekebisho madogo? Ok anyhow mwandishi amepepesa maneno sana kuitumia system kumzuia mamvi ,,,wala asihofu sio system itatumika ni wananchi wenyewe watamzuia bwana yule kwa kura za hapana dhidi yake. Ila system sio Mungu ,,na kuna kipindi inafeli na inafanyaga hata mabadiliko baada ya kugundua imefeligi wapi...
 
mbona hueleweki mkuu?!usipende kuishi kwa imagination na uwoga uwoga.......!
 
Amina! Umeonge kama mtanzania makini. System haitamwangalia mtu wala kikundi bali uhai na afya ya mama yetu tanzania! Mungu aipe system hekima na ujasiri
 
Kitengo kinakula kodi zetu bila kufanya kazi kwa umakini naweza sema kitengo kimelala sana kipo kwa ajili ya maslahi ya chama.
 
Lakini system haitavunja sheria hata kidogo kwa kujua kuwa historia itawahukumu.

System ya Kenya enzi za mwisho wa utawala wa Mzee Moi ilipoona wananchi wameamua kupata mabadiliko hawakuingilia kati harakati za kuuchagua upinzani.

Waliacha na mustakabali wa Kenya hatimaye umekuwa salama japo walikumbwa na shida na kusumbuka kidogo miaka ya hivi karibuni. Moi alishauriwa na system.

Marekani nao wakaruhusu mweusi atawale na wanamlinda vilivyo. Hivyo ndivyo system zilivyo tusizielewe vibaya. Fidel Castro akakubali kuachia ngazi na leo tunaona mabadiliko makubwa ya kimaendeleo na kisiasa Cuba. Alimruhusu mdogo wake asimamie mabadiliko ya lazima. Alishauriwa na System.

Tuiombee nchi yetu, viongozi wetu na vyombo vyote husika vilikumbuke hili kwani wanalijua; na sisi wananchi tuwaache wafanye kazi yao vizuri na kwa umahiri kulilinda Taifa letu.

Tunawaaminia.
 
Nadhani hujui kutofautisha kazi ya system na vyama vya siasa !!! System za nchi nyingine hufanya kazi zake kiutaaalamu na sio kisiasa nyie system ni ccm !!! POOR YOU
 
Back
Top Bottom