Hili ni jaribio jingine kwa System/state au Kitengo!

Hili ni jaribio jingine kwa System/state au Kitengo!

Jackbauer

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2010
Posts
6,067
Reaction score
2,228
Mimi ni muunini wa kinachoitwa SYSTEM AU STATE AU KITENGO.

Ninaamini nchi hii kama zilivyo nyingine nyingi zina MFUMO AU SYSTEM na kazi yake ni moja tu kulinda maslahi ya nchi dhidi ya majaribio ovu kutoka ndani na nje ya mipaka yetu.

Ni 'system' pekee ndio inatufanya tuishi kwa amani hata kama ni kidogo!


System hailali wala kusinzia!

System inaachia uhuru wa kutosha sana mpaka pale ulevi wa uhuru unapoanza ndipo system inaingilia kati !

Sitaki kuongelea mengi pengine siyajui sana!

Naamini ni kazi ya kawaida kabisa ya System kuendelea kujilinda na kulinda values za kitanzania ili kuifanya Tanzania iendelee kuitwa Tanzania!

Hakuna aliye juu ya system awe masikini,kilema au tajiri au gaidi.ni system pekee ndio Alpha na Omega!

Mwaka 1992,1995,2010,2013 na labda miaka ya nyuma zaidi nikiwa mdogo SYSTEM ilipitia majaribio makubwa kadhaa na ikayashinda na sasa ni jaribio jingine tena ndani ya mwaka huu 2015.

Kwa hekima ya kipekee naamini system itashinda kiurahisi kuliko kila mmoja wetu anavyotarajia kwa kuwa ili-anticipate na hivyo imejipanga vilivyo.

UPDATES 1:
System au Kitengo imepata majaribu mapya na ya kipekee na imeyafanyia kazi kwa weledi.bado naendelea kuiita system ni ALPHA na OMEGA.
Tutulie ! #COVID 19

UPDATE 2:
SYSTEM ama KITENGO imepigwa kwa miaka miwili na inaendelea kupigwa sana lakini itakaa sawa.

UDATE 3:SEPTEMBA 2024
SYSTEM ipo kwenye jaribio jingine tena.Hebu tuendelee kushuhudia yanayojiri.

....Hatimaye System imeendeleza lile ililozoea kulifanya leo tena 23 septemba 2024.tusubiri tena ...other episode.

UPDATE 4:ni mwaka mwingine tena(Agosti 2025) na hususani katika mwezi huu wa 8 system inaendelea kupitia mfululizo wa changamoto lakini unaiona namna inavyojiweka salama....
Itaendelea.....

Mwaka huu tena leo mei 19 2025 System inapitia jaribio lengine hatarishi na muhimu.

KILA LA KHERI KWA SYSTEM KATIKA KUENDELEZA MAJUKUMU YAKE!

#Heshimakwakitengo
 
Haya kumekucha magambani...wanomba msaada wa sistimu sijui kitengo! hao nao ni watanzania... wana ndugu zao wanaopata shida kutokana mfumo kandamizi wa CCM nao sistimu wanataka ukombozi...wamechoka kutumiwa kama toilet paper.
 
Kitu kizuri mwaka Huu n kwamba wanapambana watu wawili ambao tayar wameshafanya kazi na hiyo system...inawezekana kila mtu ana watu wake kwenye system hivyo kazi ikawa rahisi kabisa
 
Mimi natamani hata System ikiona amani inatoweka wamkumbuke Lukuviii ...Jeshi lichukueeee....
 
Kitu kizuri mwaka Huu n kwamba wanapambana watu wawili ambao tayar wameshafanya kazi na hiyo system...inawezekana kila mtu ana watu wake kwenye system hivyo kazi ikawa rahisi kabisa
Umesahau Slaa alipambana huku akiwa na ripota kutoka kwenye system?
 
hii nchi kweli ya ajabu na ina watu wenye fikra za ajabu.
kwa hiyo kwenu nyie sisitimu kufanya kazi ni kulinda maslahi ya chama kimoja na mafisadi?
vyama vingine havichangii kodi ya kuendesha hivyo vitengo?

kwani akishinda mtu wa chama kingine imani itapotea au hawataweza kulinda hiyo amani?
ndio maana wananchi tunawachukia na ole wenu ccm tukishaitoa madarakani, mtarudi vijijini kulima viazi.

yaani badala ya kulinda amani ya nchi na mipaka yake wako busy kulinda wezi!!!
ndio maana nchi ina wahamiaji haramu wengi na wengine wamepewa vitambulisho vya kura na passport za tz.

Tatizo la kurecruit watu wenye IQ ndogo na kuwapa kazi nzito.
wanawaza matumbo yao tu
 
hii nchi kweli ya ajabu na ina watu wenye fikra za ajabu.
kwa hiyo kwenu nyie sisitimu kufanya kazi ni kulinda maslahi ya chama kimoja na mafisadi?
vyama vingine havichangii kodi ya kuendesha hivyo vitengo?

kwani akishinda mtu wa chama kingine imani itapotea au hawataweza kulinda hiyo amani?
ndio maana wananchi tunawachukia na ole wenu ccm tukishaitoa madarakani, mtarudi vijijini kulima viazi.

yaani badala ya kulinda amani ya nchi na mipaka yake wako busy kulinda wezi!!!
ndio maana nchi ina wahamiaji haramu wengi na wengine wamepewa vitambulisho vya kura na passport za tz.

Tatizo la kurecruit watu wenye IQ ndogo na kuwapa kazi nzito.
wanawaza matumbo yao tu

Mkuu napenda sana ujadili hoja hii bila jazba wala kuwa skewed kwa upande wa kisiasa!

Labda niseme kifupi tu...System haina maslahi juu ya chama flani bali Taifa!ndio kazi yake na ndio hukumu yake!

System itaitete accm kwa sababu flani!

System itaikuza Nccr kwa sababu flani

System itaibomoa Nccr kwa sababu flani

System itaiporomosha ccm na kuikuza chadema kwa sababu flani.

System itaendelea na kazi yake kwa sababu flani.

malengo ya system ni yale yale tu kuilinda Tanzania.

Yaani system ni kama Mungu...ataleta mafuriko kwa masikini wa kilosa na kuleta tsunami asia na kuipa baraka vatican!

Mwisho wa siku SYSTEM hutuvusha na sifa huchukua watu flani flani hivi!

System lazima ipate lawama tu kwani ndio kazi yake lakini mwisho wa siku system lazima ibakie kuwa system !

Confusing but thats the way it should be!
 
Back
Top Bottom