Hili la Cleopa ni kama TUSI kwa Jakaya

Angalau hakuwa mwizi kama hawa waliopo sasa madarakani.

aliwahi kutuhumiwa kuhujumu uchumi miaka ya 80. na anatuhumiwa kuhusika kwa namna moja ama nyingine katika kifo Sokoine, kwakuwa Sokoine alikuwa mstari wa mbele kuwashughulikia wahujumu uchumi wakati ule
 
Angalau hakuwa mwizi kama hawa waliopo sasa madarakani.

Angalau alidhibiti mfumuko wa bei. Huyu mzee yuko smart sana hasa anapozungumza, hakurupuki kama mawaziri wetu wa sasa ambao wakiona swali limewashinda wanaamua kupayuka tu eti "SERIKALI IKO KWENYE MCHAKATO"
 
Huyu aliwahi kuwa pm na waziri wa pesa yeye alifanya nini cha mno?

Huwezi kulinganisha uwezo wa mawaziri wa Nyerere na JK. Wakati ule kazi ilifanyika basi tu mfumo wa uchumi wa dunia ulikuwa tofauti. Mashirika yote yaliyouzwa na akina Mkapa na JK yalianzishwa na wale jamaa.
 
Kule kwake ana miliki shamba kubwa. Anahamisha watu kizembe. Naye pia ni gamba.
 
Msuya mimi namwona kama ni wale wale tu. Sawa kamkosoa JK (Ila matusi sijayaona), kama ambavyo mtu yeyote anapaswa kufanya hivyo kwa maendeleo ya Taifa. Ila haya yote ni kwa sababu hayuko tena kwenye system (hana meno). Kumbukeni enzi za uhai wake ni mojawapo wa mafisadi wa enzi zake, tatizo habari zilikuwa haziwi wazi kama ilivyo sasa. Angalia miradi alivyoielekeza huko Mwanga, na malengo yake yalikuwa ni kupata mkoa mwingine wenye wilaya za Same na Mwanga - ingawa ilishindikana. Angekuwa rais wa Nchi siamini kama angefanya la ajabu sana, ni wale wale tu.

Ila nashukuru amemshauri Jk maeneo ya kuangalia. Ushauri wake ni mzuri ila na yeye pia ni wale wale.
 
Jana ITV nimesikiliza mdahalo uliokuwa ukiilenga Tanzania katika miaka 50 ijayo mmoja wa wageni waaliikwa alikuwa waziri mkuu wa zamani ndg Cleopa Msuya. Katika moja ya hoja zake ilionekana ni kama anauponda waziwazi utawala wa JK, hii ni baadhi ya michango yake;

i. Tz ya miaka 50 ijayo inahitaji Strong leader atakayeweza kusimama na kusema hiki kifanyike na hiki kisifanyike na ambaye ataweza kusimama katika maamuzi magumu (rejea JK kushindwa kuwa na msimamo juu ya matatizo yanayowakabili wa-tz likiwamo umeme)

ii. Tz inakabiliwa na ugonjwa hatari wa malaria, suluhisho sio kwenda kuomba msaada wa vyandarua suluhisho ni kukabili vyanzo vinavyozalisha mbu na vimelea vyake (msaada kutoka serikali ya marekani)

iii. Siku hizi hatuna wataalam wa kutosha katika masuala mbalimbali nchini mfano wa kina Prof. Benno Ndulu na wengine wa miaka ile, leo hii badala ya serikali kupeleka vijana kwa wingi nje ya nchi na kupata wataalam kama vile china na hata kenya, viongozi wamebaki kubuni mbinu mbalimbali zitakazowapeleka nje ili wapate posho kutunisha mifuko yao na kununua magari, nchi haina wataalam wa kutosha kuweza kuleta mabadiliko tunapoingia miaka 50 ijayo.(safari za JK nje ya nchi)

kwa maoni yangu nadhani mzee msuya kaamua kuponda wazi wazi utawala wa JK

Ni sawa kumwambia kiongozi udhaifu wake, lakin tujifunze kuona matatizo kwa kuangakia vyanzo na si matokeo.. kikwete si chanzo cha tatizo TATIZO NI 1.CCM 2.WATANZANIA WENYEWE
 
Hakuna jambo jema kama kuambiwa ukweli japokuwa unauma ila kama mtu ni mweledi atajirekebisha!
 
aliwahi kutuhumiwa kuhujumu uchumi miaka ya 80. na anatuhumiwa kuhusika kwa namna moja ama nyingine katika kifo Sokoine, kwakuwa Sokoine alikuwa mstari wa mbele kuwashughulikia wahujumu uchumi wakati ule
<br />
<br />
Ni ule usemi ya wahenga ndiyo inafaa kwa huyu Cleopa Msuya: SHETANI AKIZEEKA ANAKUWA MALAIKA.
 
"kwa maoni yangu nadhani mzee msuya kaamua kuponda wazi wazi utawala wa JK!" - quimby_joey

Bro, naanza kwa kukiri kuwa sikumsikia Msuya akiongea katika hiyo debate lakini kwa maoni yangu mtu yeyote akijaribu kuongea vitu ambavyo ni "logic" utagundua automatically kwamba anamponda the so called "mbayuwayu" this is simply because the guy is illogic!! If you want to prove my theory just try to do any intelligent conversation regarding a country by choosing any topic - at the end of the day u'll realize that what you discuss(problems,priorities and eventual solutions) is exactly opposite from what kikwete does!!! Mimi sala/dua zangu ni kuona akiwa na mwisho wa Ghedaffi yeye pamoja na familia yake God forbid bila hata damu ya watazania kumwagika maana kama ni cha moto tayari watanzania wamekiona - we have already paid our price!!!!
 
Katika hali ya kawaida macho yote yanatakiwa kuangalia mbele, ukiona kila jicho linaangalia upande wake au macho yanaangaliana (makengeza) ujue mwenye macho haoni mbele, Tanzania..!
 
Sioni mahali alipouponda utawala wa mk we re zaidi ya kuelezea nini kinapaswa kufanywa maana haya yamesemwa sana na watu wengi hata humu jamvini tumekuwa tukisema sana tatizo ni kuwa hakuna msikilizaji wa kujua afanyie nini yanayosemwa!!
 
JK anaingia madarakani mwaka 2000 sukari kilo ilikuwa sh 700 leo sh 2500,na viwanda vipo 4 tanzania.Hata siku moja hajakaa na wenye viwanda vya sukari kuuliza tatizo nini tusijitosheleze kwa soko la ndani?matokeo yake kiwanda kama kagera sugar kina export sukari yote njee,na ile nyeupe ya kilombero yote inapelekwa nje why?hapo utasema una rais wa nchi?
 
.. I real loved the Honesty shown by the former PM Cleopa Msuya... simple and plain spoken truth ..we should all learn from him and do what must be done!!
 
Mzee cleopa ametumia nafasi yake kikatiba ya kutoa maoni yake kama raia wengine wanavyoweza kufanya na wala hakumtukana mkuu wa kaya. aliamua kuongea ukweli kwa kuweka wazi ili kuwa na tz yenye maziwa na asali nini kifanyike tangu sasa.
 
mimi siamini kama tuna serikali wala rais,
ngoja niende majukwaa mengine. Hapa ni kujadili vitu ambavyo ktk real world havipo....
Ooh serikali ifanye hivi..ooh ifanye vile...kila nikiangalia serikali yenyewe siioni!
 
Huwezi kulinganisha uwezo wa mawaziri wa Nyerere na JK. Wakati ule kazi ilifanyika basi tu mfumo wa uchumi wa dunia ulikuwa tofauti. Mashirika yote yaliyouzwa na akina Mkapa na JK yalianzishwa na wale jamaa.
<br />
<br />
yeah,alifanya kazi nzuri katika kipindi hicho ugali wa mtama ama yanga kwa mgagani ilikua diet.makatambuga na kaunguza ilkua fashion
 
Back
Top Bottom