Hii ngumu kumeza

Hii ngumu kumeza

Status
Not open for further replies.
Daaah pepo la kuoa oa linipitie mbali "... maybe nitaoa tu if nikiwa masikini maana ili niweze kuwa na uhakika wa kugegeda itanibidi ni tafute wakumfunga speed gavana " ila kama Niko mcharo " Aisee ndoa naomba niishie kuisikia kwa radio ".... huwa hatuambiani ukweli " lakini ndoa ni moja ya sababu zinazo changia wanaume kufa mapema mnoo achilia mbali kwenda Jela
 
Mkuu piga chini huyo " mtu " atakuletea Magonjwa " ama utakuja kulea Mtoto ambaye sio wako
 
We chepuka tu ili kuondoa stress, ila muulize mkeo akueleze ukweli na ikibidi andaa fimbo umchape usimpige na ngumi utamuumiza
Ni miezi kama miwili imepita tangu nimalize chuo na kurudi nyumbani.....lakini hata hivyo nilikuwa narudi kipindi cha likizo kuonana na familia.

Kwanza niseme tu wazi,,,sina desturi ya kukagua simu ya mkewangu lakini baada ya kumtilia mashaka ilibidi nifanye hivyo.

Nikweli nilichokikuta inbox ya Facebook ni hiyo conversation kati ya wife(chati ya bluu)

na jamaa ambae namjua na ni mfanyakazi mwenzangu pia na nlikuwa namheshim sana.
Hiyo conversation inaonesha watu hawa ni wapenzi wala haihitaji nguvu ya ziada kugundua hilo.

Wadau hii kitu nilikuwa nasikia tu kwa watu kumbe ni kweli aisee inauma sana usiombe yakukute....

Imagine mtu tuko nae over ten years sasa pamoja na watoto wawili Leo hii ananifanyia hichi kitu..

Afadhali hata ningekuwa na tabia ya kuchepuka nisingeumia sana.....ningejisemea tu moyoni kwamba malipo ni hapahapa duniani , muosha huoshwa.

Lakini kinachoniuma Mimi nimekuwa mwaminifu tangu nilipomuoa sijawahi msaliti hata Siku moja.

Wakuu embu nisaidieni experience kwa wale mliopata maswahibu kama haya au hata kama hayajakupata nishauri tu kabla sijaharibu Niko na hasira sio ya kawaida ingawa sijionyeshi kwake.....View attachment 897325
 
Huyo jamaa yako naye yumo humu na ameuona uzi wako. Ameanza kutafuta ushauri naye
 
Kwanza kabisa napingana na hao wanaokataa kuchunguza simu au mawasiliano ya wenza wao, huyo ni mkeo /mumeo wa ndoa,hivyo kufuatilia chochote kile kwake ni 'wajibu'... 'sio wawili tena bali ni mwili mmoja',maana athari zozote zikitokea, ni shared.

Mimi ilikuwa ni msg, nadhani zilisahaulika kufutwa,nikachukulia poa tu kwa ule ujinga eti tusifuatilie simu zitatuvunjia ndoa. Baadye nikaamua kufuatilia karibu mawasiliano ya ile namba, nililenga kujua muda anaopigiwa na how long wanazungumza.

Nikaja kuthibitisha pasipo shaka kuwa waliwahi kuwa katika wahusiano pindi nikiwa masomoni ila wakaja tengana miezi 5 kabla ya mie kurejea masomoni. Uchunguzi huu ulichukua takribani miezi 3 tangu kustukia mawasiliano hayo.

Nilipothibitisha, nikamwomba MUNGU anipe subra, maana ni 'NGUMU KUMESA'. Cha kwanza nikawa tayari kumsamehe, ila nikaweka nadhili kwa muumba wake kuwa, nitamuhoji mara 3 kwa vipindi ni siku tofauti, akikana zote mara 3,ndio ungekuwa mwisho.

Nikaandaa Questionnaire zangu kwa ustadi wa hali ya juu sana na umakini mkubwa kuepuka kuhisi kuwa kuna kitu akistukie, ila swali la mwisho nakumbuka lilimbabaisha na 'akapoteana'.

Ile ya mwisho alikili na akaeleza yote tangu siku ya kwanza hadi walipoamua ku break up, na sababu.

Nilimwambia ampigie jamaa simu na amuite aje nyumbani kwangu, jamaa akazingua, nikampigia nikwambie ndani ya masaa 4 aje kwangu, lasivyo......!! Jamaa alikubali kuja.

Yeye alilia na kueleza kila kitu... Aliomba msamaha nikawasamehe wote. Japo mgoni wangu aliogopa sana baada ya kutoka kwangu alienda kuomba likizo na baadaye uhamisho, nasikia alirudi mkoani kwao maana roho ya hatia ilikuwa ikimwandama. Mke nae kabadilika ajabu, hakutarajia kilichotokea.

Nadhani ndugu yangu huenda ukapata cha kujifunza hapo, japo sikushauri ufuate ufuate njia niliyoifuata, maana kila mtu ni wa pekee. Kuacha nalo wazo zuri, tatizo utayemleta naye hauna uhakika naye. Huo ndio uzoefu nilioupitia.
Asee pole mkuu.


Nikuulize , vp wewe uliwahi Ku cheat tangu ulivyooa?
 
Zamani nilikuwa najiuliza kwa nini watu wanaoa ma-polygon;kumbe jibu lake ndio hili,hutokuwa na presha kwa sababu watu hawamtongozi na wana mapenzi ya kweli kwa sababu vishawishi hawana.
 
hilo kuendelea nae litakuuma maishan milele,,,, kila ukikumbuka au kumuona jamaa lazma utaumia tu,, la maana maliza uhusiano anza maisha mengne,, hao hawaachani watapotezea kwa mda baadae wataendelea kupeana,,,,,,,,,,,,, kumbuka mwanaume huwa haachi mwanamke
 
kama mna miaka Zaidi ya kumi ktk ndoa ,na jamaa kamchukua mke kwa mwezi tuu ,usijali endelea tuu na mkeo miaka 10 sio sawa na miezi ,ila mwambie mkeo aende kwa jamaa mara ya mwisho then AKOME abaki na wewe
Mmhh
 
Baadhi yetu tumekuwa tunaishi tu. Hatuna mpenzi. Hatujaribu umalaya. Hatumpendi mtu. Hakuna anayetupenda. Tunajishughulisha tu na kazi zetu, tunakula, tunalala, na kuishi maisha yanasonga kiulaiiini.
 
Mkuu tupe mrejesho umeamuaje? siku zinakimbia...na hasira zinapungua hasa pale atakapokuambia karibu baby tupumzike.
 
Pole sana...

Kinachokuuma hapo ni kipi? Mbona hakuna kibaya... au kumwambia ana hamu mwezi wa pili?


Cc: mahondaw
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom