totopack
Member
- Mar 4, 2015
- 52
- 10
Nina rafiki/ ndugu ambaye nilisimamia harusi yake(best man) miaka mitano iliyopita, kwa sasa wana watoto wawili.
Tatizo lilianza pale mume alipogundua mke ana madeni sana, anadaiwa na watu mbalimbali (wanaume kwa wanawake) jumla shilingi million 14 ambazo alikuwa anaweka dhamana kadi ya gari nk na analipa kwa riba. Iligundulika baada ya wadai kumpeleka polisi.
Katika kufuatilia mke akasema hajui pesa imefanya nini, jamaa akaamua kulipa deni ili kuondoa hiyo aibu ndipo afuatilie akiwa katikamchakato wa kulipa amegundua mke alimdanganya na kuna sehemu nyingine anadaiwa million 6 na bado anaendelea kukopa kwa kificho hivyo madeni yanaongezeka, jamaa kachanganyikiwa na mimi nimekosa cha kumshauri kwa kweli, humu kuna watu wanapitia changamoto mbalimbali za ndoa naomba tumshauri tafadhalini.
Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo lilianza pale mume alipogundua mke ana madeni sana, anadaiwa na watu mbalimbali (wanaume kwa wanawake) jumla shilingi million 14 ambazo alikuwa anaweka dhamana kadi ya gari nk na analipa kwa riba. Iligundulika baada ya wadai kumpeleka polisi.
Katika kufuatilia mke akasema hajui pesa imefanya nini, jamaa akaamua kulipa deni ili kuondoa hiyo aibu ndipo afuatilie akiwa katikamchakato wa kulipa amegundua mke alimdanganya na kuna sehemu nyingine anadaiwa million 6 na bado anaendelea kukopa kwa kificho hivyo madeni yanaongezeka, jamaa kachanganyikiwa na mimi nimekosa cha kumshauri kwa kweli, humu kuna watu wanapitia changamoto mbalimbali za ndoa naomba tumshauri tafadhalini.
Sent using Jamii Forums mobile app