Hii ndoa inapumulia mashine, ushauri tafadhali

Hii ndoa inapumulia mashine, ushauri tafadhali

kila mtu abebe mzigo wake hapo hakuna kulipa tena tena akinifuata fuata anakula na vitasa juu....😕😕😕
 
Nina rafiki/ndugu ambaye nilisimamia harusi yake (best man) miaka mitano iliyopita,kwa sasa wana watoto wawili.Tatizo lilianza pale mume alipogundua mke ana madeni sana anadaiwa na watu mbalimbali (wanaume kwa wanawake) jumla shilingi million 14 ambazo alikuwa anaweka dhamana kadi ya gar nk na analipa kwa riba. Iligundulika baada ya wadai kumpeleka polisi.Katika kufuatilia mke akasema hajui pesa imefanya nn,jamaa akaamua kulipa deni ili kuondoa hiyo Aibu ndipo afuatilie akiwa ktk mchakato wa kulipa amegundua mke alimdanganya na kuna sehemu nyingine anadaiwa million 6 na bado anaendelea kukopa kwa kificho hivo madeni yanaongezeka,jamaa kachanganyikiwa na mm nimekosa cha kumshauri kwa kweli,humu kuna watu wanapitia changamoto mbalimbali za ndoa naomba tumshauri tafadharini.

Sent using Jamii Forums mobile app
mbona kama namfahamu vile si wa pale kati hivi
 
Isije kuwa huyo mwanamke anatengeneza vitegea uchumi kimyakimya afu mwisho wa siku anakuja anadai talaka anamwacha mme wake katika hali duni aiseee.....
 
Isije kuwa huyo mwanamke anatengeneza vitegea uchumi kimyakimya afu mwisho wa siku anakuja anadai talaka anamwacha mme wake katika hali duni aiseee.....
Huenda ikawa pia mana mpaka muda huu haijajulikana hela zote hizo alikuwa anazifanyia nini?
 
Mkuu utakubali mkeo apelekwe polisi wakati weww mume wake upo?
It depends na situation mkuu.... haiwezekani mtu akope zaidi ya milioni ishirini afu mwisho wa siku nisijue kaifanyia nini? bado haitaniingia akilini labda tyu nijue maybe yuko na asset mahali ndio naweza msaidia tofouti na hapo itabidi apelekwe hakuna namna mimi nitaendelea na ulezi wa watoto bila shida
 
Huenda ikawa pia mana mpaka muda huu haijajulikana hela zote hizo alikuwa anazifanyia nini?
Ukiona hivyo ujue huyo mwanamke kamzidi kete mumewe ndio maana kila kukicha anaibuka na madeni mapya.... kuna shughuli ya siri huyo mwanamke anaifanya and hataki mume wake ajue.... mkuu
 
Pamoja na kwamba haitakiwi kutoa siri za familia nje, hiyo ni "NEWS" lazima itoke. Huyo mke siyo binadamu atakuwa pepo,, milioni 16 ni ndefu sana. Labda kama ana mabiashara makubwa yenye uhakika wa kurudisha.
 
Shost mmoja ameolewa lakini tamaa ya kujionyesha inamghrimu sana. Anaweza afungue mlango wa duka ili tu watu wajue na yeye anabiashara mambo safi lakini mtaji wote ni wa kukopa
Akope sawa, azalishe na arudishe mkopo itakuwa sawa ila kama ndo zinaishia kwenye vitenge na gold mwisho wake ni mbaya sana.
 
Mwambie arudishe kwao mpaka aseme izo pesa alikuwa anafanyia nini?aiwezekani m14 zisiwe na kitu kilichofanyika,basi mume si angeona hata mavazi ya gharama zaidi ndani angeshituka,juzi nimeona mchezo kwenye tv wanawake wameanzisha iyo tabia wanakuja watu wakati uko nae wanasema wanamdai na wanangangania kubeba vitu kwa lengo la kujua mwanaume utaona aibu ulipe kumbe ni utapeli wanaenda kugawana mbele uko na mwanamke akiwepo ilo nalo alijue
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
It depends na situation mkuu.... haiwezekani mtu akope zaidi ya milioni ishirini afu mwisho wa siku nisijue kaifanyia nini? bado haitaniingia akilini labda tyu nijue maybe yuko na asset mahali ndio naweza msaidia tofouti na hapo itabidi apelekwe hakuna namna mimi nitaendelea na ulezi wa watoto bila shida

Yataka moyo mkuu hiyo ya kusema umuache aende watoto utalea. Hata kama uwezo unao huwezi msaidia kulipa?

Ikifikiaga hatua hii huwa naona ndani ya familia kuna baadhi ya mambo yakiwa na uwazi na kushirikishana kabla ya kuyafanya inakuwa bora zaidi.
 
Yataka moyo mkuu hiyo ya kusema umuache aende watoto utalea. Hata kama uwezo unao huwezi msaidia kulipa?

Ikifikiaga hatua hii huwa naona ndani ya familia kuna baadhi ya mambo yakiwa na uwazi na kushirikishana kabla ya kuyafanya inakuwa bora zaidi.
Mkuu hapo ni kuwa muwazi usaidiwe and vice versa is true.... na inaonekana mwanamke keshajua jamaaa anamkwanja so anafanya kukopa kimakusudi ili jamaa alipe then hapo jamaa inabid abadilike kidogo awe kauzu then kama ni mwanamke anaejielewa itabidi afunguke ukweli tofouti na hapo ashitakiwe tu..... ili next time asirudie alichokifanya

Mkuu hata kama uwezo upo? kuna vitu vingine vya kufanya kutumia hiyo pesa na si kulipia madeni ya kile kisichoonekana....
 
Mleta mada
Kwanza ulitakiwa kumuuliza rafiki yako je mkewe hizo hela ana peleka wapi? Maana haiwezekani ulipe deni bila kujua hizo pesa ana peleka wapi?
Na kama anaendelea kukopa je anakopa ana fanyia nini?
Na kama mke ana shindwa kumueleza nini ana fanya na hizo pesa basi hapo hakuna ndoa ni ndoano maana kasha Kuwa mume atalipa tu!
Kati ya yafuatayo huyo mke ana weza kuwa na fanya
1. Ana jenga kwa siri
2. Ana mwanaume mwingine naye ana muhonga
3. Ana tamaa na maisha asiyo weza
Solution
Akaae chini na mke wazungumze kinaga ubaga akishindwa basi aite watu ana ona ni wakaribu, kama inashindikana basi ashilikishe viongozi wa dini
Km hivyo vyote havifui dafu basi Mungu atamuelewa tu akimuacha Dunia imfundishe ....


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waendelee tu mkuu kwa kuwa mke wake hapendi maisha bila madeni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom