Hii Mikoa Nani Kailoga?

Hii Mikoa Nani Kailoga?

Hakuna mji wenye sida ya maji kama Arusha,...Khaaa!!!

Hapana mkuu!! Unalinganisha na wapi? Kwenye suala la maji arusha ina nafuu kidogo kuliko hata dar, ingawa hawana bahari wala ziwa kubwa.
 
usiongopee watu mikoa yote ina maskin na hali mbaya sana,kariakoo nyumba za udongo ni juz tu zmeondoka, hyo kagera yako haina lolote mm naishi huko kagera biharamulo nyabusozi,muleba ndo ucseme khaaa misifa ya bure na roho mbaya mbaya tu. naconclude kuwa; MJINI NI NYuMbani KWako si kwa jirani,inawezekana ukawa unishi Dar na mm singida au lindi na kiuchumi usifue dafu.

Makazi ya kuridhisha yapi kwani hiyo mikoa iliyobaki hawana makazi ya kuridhisha labda umuulize mtoa mada katumia vigezo vipi maana hali ya mikoa hiyo kimaisha ni sawa tu. Na nilijua kusudi watu watapinga uwepo wa Kagera kwa kuwachukulia wahaya wanavyoishi nao mjini nendeni mkaishi nao kule ndo mtawajua vizuri na kama unazungumzia huduma za jamii ndo sababu hata mikoa mnayosema imeendelea nenda Arusha, Mbeya n.k kuna maeneo mengine huduma za jamii ni kitendawili huko vijijini lakini bado utakuta hicho kijiji kipo kwenye mkoa ambao makao makuu yake yanahadhi ya jiji.

Katika post yangu nimesema "majority" labda ndiyo ambalo haikueleweka kwa baadhi yenu. Katika hili ni kweli mikoa yote ni maskini lakini kuna kuzidiana. Kwa bahati nzuri nimetembelea mikoa karibu yote ya nchi hadi vijijini na hilo ndilo linaloniongoza kusema hayo niliyoyasema. Kuna baadhi ya wananchi wenzetu wanapatashida kweli na kuna wakati hata chakula wakati mwingine inakuwa ni shida kweli.

Nilienda sehemu inaitwa Mayamaya Dodoma hali niliyoikuta kule na vijiji vya jirani wakati wa Kiangazi ilikuwa ngumu kweli, wananchi wanaaamka saa kumi usiku kwenda kuhemea maji na wakati huo huo kuna hatari ya simba, maji yenyewe tope tupu. Hali niliyoikuta kule uwezi kulinganisha na kijiji chochote cha Mkoa wa Kagera ama Ruvuma. Hata hewa yenyewe kwenye nyumba za tembe wanapolala ni mgogoro. Zao la biashara ni zabibu lakini wao hawana kwani linahitaji mtaji mkubwa hivyo hali ya umaskini ni ya juu kabisa. Hata mavazi asilimia 98% wamevaa kaniki full mwenyekiti wa kijiji na mtu mwingine mmoja ndo waliokuwa wamevaa kaniki (mtandio) na shati angalau. Nimeyasema haya si kwa nia ya kukandia bali kujipanga kutafuta suluhisho, ktk migao ya fedha za maendeleo baadhi ya sehemu zipendelewe kwani ziko nyuma sana
 
umasikini wa mikoa hiyo umepima kwa kutumia kigezo gani? kwa ujumla maeneo mengi tz bado ni masikini
 
Mikoa masikini na isiyoendelea Tanzania hii japo kuna mingine wanatokea wapenda sifa.

1. Kagera
2. Lindi
3. Rukwa
4. Kigoma
5. Singida
6. Tabora
7. Mara
8. Ruvuma
9. Pwani
Mikoa hiyo nichoka mbaya kuliko hata huu

10. Mtwara.

Na hizo ni takwimu sahihi! Mimi namshukuru Mungu nimetembea mikoa mingi Tanzania isipokuwa Kigoma. Lakini makao makuu ya wilaya nyingi almost zinafana. Wilaya ambazo miji yake ni mikubwa ni Tarime-Mara, Masasi- Mtwara, Njombe- Iringa( kwa wakati ule), Korogwe- Tanga, Nzega-Tabora, Kahama-Shinyanga. Nyingi ya zilizobaki ni ndogo kabisa.
Mikoa ambayo makao makuu yake ni miji mikubwa kwa maana ya Level ya Jiji, Manispaa na Miji ni kama ifuatayo:-
Mwanza
Arusha
Mbeya
Tanga
Moshi
Morogoro
Dodoma
Tabora
Mtwara
Musoma
Iringa
Kigoma. Mingine yote ni miji midogo sana japokuwa ni Manispaa pia. Lakini pia fungua website ya TRA halafu google: Tanzania Domestic Revenue Collection Regionalwise, Mtwara bado iko juu kimaendeleo! Wilaya ya Tandahimba kwa mfano, moja ya wilaya tajiri kabisa nchini Tanzania. Mkoa wa Mtwara kila kitu kitakwimu ni duni sana katika wilaya moja, nayo ni Mtwara Vijijini, ni.duni kielimu, kiuchumi, kimiundombinu, vifo vya watoto na akinamama, na hii ndo pekee hushusha hadhi ya mkoa mzima, lakini kwingineko, Mtwara ni bora sana ukilinganisha na maeneo mengi ya Tanzania
 
Mtwara inakuja kwa speed kubwa sana,siyo ya siku zile tena...itafunika mikoa mingi tu muda si mref...just a matter of time.

usihau na ruvuma pia.
uranium,makaa ya mawe,mafuta/gesi,ktk mwambao wa ziwa nyasa,madini nk vitaufanya mkoa huu kuwa tishio kimaendeleo.
isipokuwa tu kama raia watajitambua kutokuichagua tena wanaccm ktk ngazi zote za maamuzi ya kisiasa.
 
Watu tu wajitume kufanya kazi ndo tutaendelea kusini yetu. Hasa Gas ambayo imepatikana Mtwara tusiposhikana mashati kipindi hiki tutabaki hivo hivo.

baba hataki muifaidi peke yenu.na wakwere wa bwagamoyo wanaitamani hiyo gesi.
 
mchwi wa maendeleo ya mikoa tajwa hapo juu ukiongeza na singida, rukwa, katavi, mara na pwani ni wazawa asilia wa maeneo hayo kutokuwa wa hurka ya kujituma kwa bidii ( hasa wakazi wa kusini mashariki mwa nchi) na matatizo ya uoto wa asili katika maeneo hayo mfano singida sehemu kubwa imetawaliwa na ukame, lakini pia ugumu wa kufikika kwa urahisi kwa maeneo mengi ya mikoa hiyo ni chanzo cha kudidimiza maendeleo ya mikioa hiyo mafano rukwa na katavi.
 
usiongopee watu mikoa yote ina maskin na hali mbaya sana,kariakoo nyumba za udongo ni juz tu zmeondoka, hyo kagera yako haina lolote mm naishi huko kagera biharamulo nyabusozi,muleba ndo ucseme khaaa misifa ya bure na roho mbaya mbaya tu. naconclude kuwa; MJINI NI NYuMbani KWako si kwa jirani,inawezekana ukawa unishi Dar na mm singida au lindi na kiuchumi usifue dafu.
heko kweli unajua maendeleo yanaanzia kwako.wangapi dar wanaishi kama kambini hatusemi na ilihali baadhi ya watu kigoma au mtwara wanaishi kwenye nyumba nzuri tubadilike umaskini unatuhusu wote xo cha mxingi ni kujipanga ili tusonge mbele
 
Nashangaa wazanzibar wanavyolalamika muungano unawanyonya au unapendelea bara,wakati hata mikoa hii mi 3 bado nayo iko nyuma kutokana na kero za muungano lakin haijawah kudai tanganyika yao.
Nadhani wazanzibar wana haki, maana nilkikuwa zanzibar december, ule uwanja wa ndege umechoka sana, yaqani mabegi uatafikiri yamewekwa kwenye karo, halafu kuna tundu ndio jamaa wanawake mabegi yote abiria ndio mnachagua.

Hivi ile kama ni nchi, si aibu sana? Pale forodhani jioni utakuta hata teenage boys wanatembea peku, yaani downtown wanakimbiakimbia peku kabisa bila viatu. Aibu!
 
mie nadhani hakuna aliewaloga zaidi ya kujiloga wenyewe na uvivu wao wa kuchagua maendeleo, maendeleo ya mmoja mmoja ndiyo maendeleo ya kitongoji, kijiji, mkoa na nchi, wewe kutwa nzima umekaa kwenye kipambaza unacheza bao wakati wenzio wanaingiza hela kwa ajili ya maendeleo yao hivi mtalingana kweli, shilingi ya leo sio ya kesho bana, ndio maana ya utofauti huo ktk maeno na vijiji na mikoa yetu, fuatilia utajua ukweli.
 
Back
Top Bottom