Hii itawauma wengi

Hii itawauma wengi

Kwaio tatizo ni mtu kukaa kwao wakati hawezi kulipa kodi ya miezi miwili daah aisee naona una gubu sana mzee daah
 

Huwa nashangazwa sana watu wanaokerwa na aina ya maisha ya wengine wakati hayawagusi kwa namna moja ama nyingine.
 
Huwa nawahurumia sana wadada wanaotongozwa mitandaoni. Anawasiliana na jamaa huku kichwani anajenga picha ya kukutana na bonge la shefa. Siku anapokutana na huyo mtu sasa. Anatamani hata kutapika kwa hicho kituko alichokutana nacho.
CC. Mzigua90 Madame B Evelyn Salt Shunie
Hahahahah
Usinikumbushe mie.
Nilipata danga kule Badoo, likanitumia laki 1 na nusu nauli ili nimfate Mwanza, ila kila nikimuomba picha yake anasema utakuja kuniona hukuhuku.
Nikasema potelea mbali, laki 1 na nusu kwenda hapo Mwanza tu, ngoja niende maana litakuwa bonge la shefa na lina mawe hatari.

Basi siku mbili kabla, akanitumia laki ya kuwaachia ndugu nyumbani.
Nikasema dah!...Mungu anipe nini mimi.
Laki na nusu + laki= laki 2 na nusu na hapo sijakutana nae uso kwa uso.

Siku ikafika, nikajifungasha.
Huyo mpaka Ubungo, ndaaaaa!!!! kwenda Mwanza.
Nikawa nawasiliana nae kila dk mpaka naingia Mwanza.
Akanielekeza kuwa amenichukulia chumba pale Victoria Palace. Nimefika pale kwa muhudumu wa hotel akasema kweli kuna jamaa kalipia hotel kwa wiki 2 na kampa muhudumu laki 2 anipe yeye atakuja kesho.
Basi muhudumu akanipa zile laki 2 akanielekeza na chumba kilipo.
Basi usiku kucha nawaza kuhusu huyo jamaa alivyo...mbona anajificha ficha.

Kesho yake asubuhi ya saa 4, muhudumu akaja na elfu 40 kasema inatoka kwa jamaa.
Nikaipokea.
Mchana nikashuka kwenda kula....(jamaa naendelea kuwasiliana nae siku zote hizo)
Nikafika restaurant ya hotel nikala na kunywa.
Nimekaa dk 10, akaja yule muhudumu na laki 2 tena zingine mkononi akasema jamaa kasema nikupe....nikazipokea.

Imefika jioni, jamaa ananipigia simu kuwa amepata udhuru hivo anaenda Dar kikazi kwa siku 4 ila akasema niende kwa yule muhudumu amemuachia laki 7 ili niendelee kubaki pale mpaka atakapokuja baada ya hizo siku 4.
Basi nikaanza kuzurura Mwanza, kula na kunywa sana kwa siku hizo 4.

Siku ya 5 asubuhi akaniambia yuko chini ya hotel nikampokee.
Nilichokutana nacho, sikuamini.

Ila mpaka leo huwa naukubali sana ule msemo wa kuwa, "pesa ndo mchawi wa mwanamke"
Anyway....nilikula bata ila ndo hivo.
Baadae saaaana nilivyorudi Dar yule muhudumu alinipigia simu baada ya miezi 6 kuwa yule jamaa alijiua.
Ila nilikuja kugundua kuwa wapo wanaume waaminifu na wastaarabu katika hii mitandao ya Kijamii.
Japo watu wanaponda ila mie nishafata sana wadau mikoano huko.
 
Sielewi kama mimi ndio nina matatizo ama vipi, maana hivi vitu watu wanafanya siku hizi vinanichanganya

Unakuta mtu ana miaka 25+ anaishi nyumbani kwao, hata rent ya miezi miwili hawezi kujilipia lkn ukija kwenye status yake unakuta yy ni bingwa wa kuandika historia ya mabilioni ya Jeff Bezos, Jack Ma na kina Patrice Motsepe

Mtu huyo huyo hafanyi chochote kbs, akishashiba chakula cha mama anakuja IG anaandika "Dear haters, the more you hate me the more I become successful" Ni kama vile kuwa na haters ni fashion inayoTrend

Watu wa aina hii ukimuuliza bruh mishe zinaendaje,kwanza lazima akujibu kwa kingereza,utasikia "Patience bruh, you know patience is bitter, but it's fruit is sweet". Sasa mimi najiuliza hivi tatizo ni kuwa na elimu au kutokuwa na elimu. Maana watu wa namna hii huwa wanasoma vitabu kweli kweli, cashflow quadrant yote ipo kichwani

Kukaa nyumbani kufikiria kuwa milionea ni utoto sana na hii michezo ya kujifanya wasomi na wachambuzi haitatufikisha popote pale. Mtu anajua matoleo yote ya Range Rover lkn bado nauli ya daladala mpk aombe kwa mtu

Sisemi kuwa watu wasiwe na ndoto kubwa, hapana! lkn kabla ya kutamani kuwa bilionea fikiria kwanza jinsi utakavyofanikisha kuhamia kwako. Kama una degree ya BaEd na hauna ajira, nunua mabenchi fundisha watoto twisheni jioni, 25,000 kwa mwezi, anza na watoto 10, hiyo ni 250,000... hapo unaweza kuanzisha baby care ya wanafunzi 40, kila mmoja ada 30,000 kwa mwezi una milioni yako. Asubuhi baby care, jioni twisheni, weekend mitihani

Muhimu sana ukaepuka kuwaambia watu shida zako, coz kila mtu ana shida zake kibao na hkn anayeshtushwa na shida zako. Km una ndoto sahau mtu kuinvest hela yake kwenye ndoto yako wkt ww haujainvest hata mia. Komaa invest hela yako then push, mtu akitaka kukujoin akukute kati kati, ht ukimwambia inahitajika mil 20 at least inaelezeka hiyo hela itatumika wapi. Sio uniombe mil 5 wkt unalala kwa mama'ko, hapo nitajua tu huyu jamaa hela yng atalipia kodi....#NIMEIKUTA MAHALI WADAU#
Imekaa sawa sana
 
Nimecheka sana, hii inaitwa necked truth, wanapita kimyakimya kwenye uzi huu.

Kama alivyosema mtoa mada, sisi tuliozoea kula ugali wa shikamoo huwa tunasoma sana vitabu... naomba nikurekebishe...
Sio necked truth.... ni naked truth.
 
Muhimu sana ukaepuka kuwaambia watu shida zako, coz kila mtu ana shida zake kibao na hkn anayeshtushwa na shida zako. Km una ndoto sahau mtu kuinvest hela yake kwenye ndoto yako wkt ww haujainvest hata mia. Komaa invest hela yako then push, mtu akitaka kukujoin akukute kati kati, ht ukimwambia inahitajika mil 20 at least inaelezeka hiyo hela itatumika wapi. Sio uniombe mil 5 wkt unalala kwa mama'ko, hapo nitajua tu huyu jamaa hela yng atalipia kodi....#NIMEIKUTA MAHALI WADAU#
Moja ya maneno yenye hekima sana kwa asie elewa anaitaji maombi !!
 
hii thread ina weakness kidogo ila kilichozungumzwa ni ukweli
 
Hapa naona vita kati ya watu waliohama makwao(wenye kazi)na ambao wapo makwao(wasio na kazi)some time huwa najiulizaga hivi wale wafanya mazingaombwe wanageuza makaratasi kuwa hela wako wapi maana huu ndo muda sahihi wa kufanya hivyo maana vy***** vimekaza.
Nb:kila mtu anamda wake wa kuondoka nyumbani japo wengine tulikimbia toka tukiwa na miaka 15
 
Back
Top Bottom