Hii itawauma wengi

Hii itawauma wengi

Yaani ni wachache sana kusaidia mafanikio ya wengine
Mtoa mada ni muungwana sana kwani unapondwa na hapohapo unapewa idea ya maisha.
Big up mkuu waambie maisha hayaendi hivyo
Wengi hawana kitu lakini ukisema ulichonacho wao ndio wa kwanza kukubeza ingawa hana lolote.

Mitandao mingine ya kimataifa unakuta watu wanajimwaga kwa hali zote na kusaidiana lakini mitandao yetu threads zetu nyingi ni hovyo kabisa
 
Yeye kukaa kwao na kula hela za Wazazi wake wewe unaumizwa na nini?

Waafrika tuache tabia za kimaskini za kuona anayeishi nyumbani kwao hana malengo yoyote.
Mleta mada anajaribu kukumbushia tu kuwa umri unakwenda, hii inaweza kusaidia kuwashtua watu na wakafanya mabadiliko. Hata wazazi wengine hawasemi, lkn hawapendi kiendelea kulea hao wababa wazima, na siku wazazi wakifa utahamia kwa mjomba?
Sioni ubaya wa hii mada kama sehemu ya kuendelea kukumbushana maisha tu!
 
pale unapopata pa kushika na kushiba baada ya kushikwa mkono,fikiria tu umemaliza chuo,hujapata kazi na mtaji huna...wahurumieni wenzenu,kama we mkali wa kuchakarika acha hiyo ajira halafu anza from the scratch kutafuta ingine tuone
 
Mkuu hata mimi imeniuma sana.

Lakini ukumbuke waandika proposal wengi hawazifanyii kazi na hawawezi kuzifanyia kazi proposal zao wanazoziandika wenyewe.

Sasa tueleze wewe binafsi umeitumiaje elimu yako ama taaluma yako katika kuinvest ama kutokea?

Maana isije kuwa muuaji wa mwizi kumbe naye ni mwizi vilevile.
 
Tatizo ni kuishi nyumbani au kuendesha Maisha yako?embu nenda Kariakoo na upanga ukacheki wahindi na Waarabu wanavyoishi na watoto wao watu wazima kabisa na Maisha yanasonga.
Mkuu ukisema wahindi na waarabu, tayari upo nje ya mada. Watu hao hatuishi tamaduni moja.
 
Hata humu JF wapo wengi mno. Hujifanya wajuzi, wachambuzi na wenye kasha nyingi mno.
Hii yote ni athari ya utandawazi wa teknolojia na haja ya walimwengu kuishi zaidi kwa kuridhisha waliowazunguka kuliko uhalisia wa maisha yao.
Ni mbaya kwa mtu kuwa muongo lakini ni mbaya zaidi kuamini uongo wako mwenyewe kuwa kweli. Mtu anajiaminisha kuwa ni 'star' wa kwenye mtandao kwa picha alizopiga kwenye gari ya mjomba huku akiishi sebuleni kwa shangazi kupelekea kutotaka chochote chini ya kile anachojinasibu juu yake kwa hofu ya 'mahaters' wa mtandaoni. Athari yake anachagua kazi ilhali hana uwezo wa maisha anayojifanya kumiliki.
Mkuu kuna mtu aliwahi kunieleza hii habari, wewe utakuwa wa pili.

Hivi ni kweli kuwa uongo wako unaweza kukuathiri kisaikolojia na baadaye akili zako zikayaamini unayojidanganya na kisha kuridhika?

Mfano unakuta mtu kila siku anadanganya wenziye kuwa "mimi nimejenga bw, sisi kwetu kuzuri" nk nk, kumbe mtu huyo hana lolote!

Baadaye mtu huyo unakuta karidhika sana, ananenepeana tu kwa kuuamini uongo wake kuwa ana kilakitu,wakati hana lolote!
Dunia ina mambo hii!
 
Jamani maisha magumu, Na sisi tulio thubutu vizinga aviishi kwa ndugu unatamani ata mpesa na tigo pesa visinge kuwepo.
 
Huwa nawahurumia sana wadada wanaotongozwa mitandaoni. Anawasiliana na jamaa huku kichwani anajenga picha ya kukutana na bonge la shefa. Siku anapokutana na huyo mtu sasa. Anatamani hata kutapika kwa hicho kituko alichokutana nacho.
CC. Mzigua90 Madame B Evelyn Salt Shunie
Umenikumbusha machungu, ngoja nilie nitarudi
 
Huwa nawahurumia sana wadada wanaotongozwa mitandaoni. Anawasiliana na jamaa huku kichwani anajenga picha ya kukutana na bonge la shefa. Siku anapokutana na huyo mtu sasa. Anatamani hata kutapika kwa hicho kituko alichokutana nacho.
CC. Mzigua90 Madame B Evelyn Salt Shunie
Hii ipi kote kote mkuu tena kwa wadada nadhani wamezidi, unamkuta mtu kila siku kakazana ku-post picha hata sio zake ukiziangalie mwenyewe unaona huyu malaika katokea wap sasa subirisiku ya kumuona live unaweza ukajificha chini ya mti halafu ukageuza tararibu kurudi ulikotokea!!!
 
Hii ipi kote kote mkuu tena kwa wadada nadhani wamezidi, unamkuta mtu kila siku kakazana ku-post picha hata sio zake ukiziangalie mwenyewe unaona huyu malaika katokea wap sasa subirisiku ya kumuona live unaweza ukajificha chini ya mti halafu ukageuza tararibu kurudi ulikotokea!!!
Na wanavyojua kujibebisha sasa...
 
Back
Top Bottom