Haya mambo mnayaexagerate sana, mbona wapo wengi tu, kwani akina mama Salma,Anna,Janeth walianza na waume zao wakiwa na kipato gani??
Hao hao unaodai wana hali za chini ndio kwa kiasi kikubwa sana wanaoa,kwani wanaoa wanawake wa nchi gani? Suala la mahusiano ni la wawili hivyo likifail basi ujue wote mmechangia kwenye kufail kwake.
Na wanaume wengi wa kitanzania waliofanikiwa basi wengi walianza chini sana na wake zao,ila wakishafanikiwa ndio mabalaa yanaibuka,but unakuta wake zao wapo nao tu, na wengine hudiriki kabisa hata kuacha wake zao maana wakati huo ndio wanakuwa hawafai bali dogodogo ndio wanafaa, hebu ifike hatua muwape credit zao muone na mazuri yao.
Tatizo letu watz ukikataliwa na mwanamke au ukiachwa basi unahukumu wanawake wooote,akikuacha basi shukuru,muache aende as maybe kubaki nawe ndio ingekuwa anguko lako,hakuwa wako huyo,wa kwako atabaki nawe katika hali zote.
Mpendwa natamani ningekuwa na pc hili nikujibu vizuri hii reply yako paragraph after paragraph lakini kwa bahati mbaya natumia simu, ila ntakujibu kama ifuatavyo naamini utanielewa tu.
Kwanza kabisa kama umelielewa vizuri bandiko langu hakuna exeggeration yoyote ile bali safari ya obama na Michelle ni ya kipekee sana kulingana mazingira yao, na hauwezi ukawalinganisha na hao uliotaja hapo.. Alafu huyo mama janeti magufuli hakustahili kabisa kumuorodhesha kwenye huo mfano wako, yaani huyu mama janeti aliyekataa kumpigia mumewe kampeni,... huyu mama janet ambae hakuna shughuli yoyote ya kijamii tunayomuona akifanya,...huyu mama janet ambae watanzania wengi hawajui kama yeye ndio first lady eti ndio unatupa kama mfano wa Michelle serious!? kwa context iliyopo hapa huyo jenet hayumo kabisa wanawake ambao ulitakiwa kuwa mention hapo regarding to the context labda mama Maria nyerere na mama Salma kikwete.
Unasema kwamba wanaume wenye kipato cha chini ndio wanaoa kwa kiasi kikubwa, sawa hili sikatai lakini je, wanaoa wanawake wa aina gani!!? Je wanaoa wanawake wanaolingana nao au kuwazidi vipato!? je wanaoa wanawake wanaowazidi kielimu!? na kama wapo ni wangapi kati ya hao wengi!?... The gospel truth ni kwamba wanaume wengi hao wenye vipato vya chini wanaoa ma low life wenzao na hili limechangiwa na pande zote mbili Yani wanaume na wanawake pia simaanishi kwamba mwanaume mwenye low status hawezi kumuoa mwanamke mwenye high status.
Ni kweli kuna wanaume wengi tu wa kitanzania walionzia chini sana na wake zao na walipofanikiwa wakageuka chatu kwa wake zao kwa kuwaachia maradhi ya moyo na wengine hata kuwauwa kabisa. Hakika ni ukweli usiopingika hakuna watu wanaojua kuvumilia wanawake na wanaongozwa kwa kunyanyaswa na mimi binafsi huwa namuheahimu sana mwanamke yoyote anayestahili kuheshimiwa haijalishi mahusiano yangu na yeye yako vipi.
Kuwahukumu wanawake wote kwa kosa la mwanamke mmoja huo ni upuuzi wa hali ya juu, lakini mimi binafsi naongelea hali halisi nnayoiona kwa hiyo usishangae kuona nikiinvolve majority. Wanawake wengi wa kipindi hiki hawana sifa za kuitwa wake, wengi wao ni wavivu kwanzia kufikiri na wana golddigging traits... The representative sampling suffices, angalia tu hata humu jamiiforum wanawake wanaokuja kutafuta partners style wanayoingia nayo..
eti mtu anakwambia asiwe mweusi sana awe maji ya kunde! serious hiv kweli una akili zako timamu hicho kinaweza kuwa ni kigezo cha kuangalia ukiwa unatafuta mume?
Haya sijui eti mara awe na degree pia na kazi nzuri..!! huu si ni upuuzi? je kama hana kazi nzuri kwa muda huo lakini kupitia wewe kwa network uliyonayo unaweza kumfanya akawa na kazi nzuri tu hapo tayari mkiwa kwenye mahusiano. Na sidhani kama hata huwa wanafikiria hili.
Kupitia hawa na hizi sababu zao chache unaweza kuona jinsi gani mabinti wengi wanavyokosa material ya kuitwa wife, na hawa ni reflection ya waliopo huko mitaani. Yaani wengi wanapenda mwanaume ambaye tayari yuko accomplished Najua hii sio kwa wanawake wote ila kwa hawa waliozaliwa miaka ya 80s kuja huku juu wengi wako hivyo. They are too selective and lazzy.
Wanaume tuna makosa yetu na tumechangia kwa kiasi kikubwa sana kuwaharibu hawa wanawake na sasa hatuna budi kuubebea huu msalaba.
Mwisho kabisa niseme kama Michelle wapo tanzania hii but finding one is like a needle in haystack.