Hii inapendeza sana kwa wapenzi

Hii inapendeza sana kwa wapenzi

Mpendwa natamani ningekuwa na pc hili nikujibu vizuri hii reply yako paragraph after paragraph lakini kwa bahati mbaya natumia simu, ila ntakujibu kama ifuatavyo naamini utanielewa tu.

Kwanza kabisa kama umelielewa vizuri bandiko langu hakuna exeggeration yoyote ile bali safari ya obama na Michelle ni ya kipekee sana kulingana mazingira yao, na hauwezi ukawalinganisha na hao uliotaja hapo.. Alafu huyo mama janeti magufuli hakustahili kabisa kumuorodhesha kwenye huo mfano wako, yaani huyu mama janeti aliyekataa kumpigia mumewe kampeni,... huyu mama janet ambae hakuna shughuli yoyote ya kijamii tunayomuona akifanya,...huyu mama janet ambae watanzania wengi hawajui kama yeye ndio first lady eti ndio unatupa kama mfano wa Michelle serious!? kwa context iliyopo hapa huyo jenet hayumo kabisa wanawake ambao ulitakiwa kuwa mention hapo regarding to the context labda mama Maria nyerere na mama Salma kikwete.

Unasema kwamba wanaume wenye kipato cha chini ndio wanaoa kwa kiasi kikubwa, sawa hili sikatai lakini je, wanaoa wanawake wa aina gani!!? Je wanaoa wanawake wanaolingana nao au kuwazidi vipato!? je wanaoa wanawake wanaowazidi kielimu!? na kama wapo ni wangapi kati ya hao wengi!?... The gospel truth ni kwamba wanaume wengi hao wenye vipato vya chini wanaoa ma low life wenzao na hili limechangiwa na pande zote mbili Yani wanaume na wanawake pia simaanishi kwamba mwanaume mwenye low status hawezi kumuoa mwanamke mwenye high status.

Ni kweli kuna wanaume wengi tu wa kitanzania walionzia chini sana na wake zao na walipofanikiwa wakageuka chatu kwa wake zao kwa kuwaachia maradhi ya moyo na wengine hata kuwauwa kabisa. Hakika ni ukweli usiopingika hakuna watu wanaojua kuvumilia wanawake na wanaongozwa kwa kunyanyaswa na mimi binafsi huwa namuheahimu sana mwanamke yoyote anayestahili kuheshimiwa haijalishi mahusiano yangu na yeye yako vipi.

Kuwahukumu wanawake wote kwa kosa la mwanamke mmoja huo ni upuuzi wa hali ya juu, lakini mimi binafsi naongelea hali halisi nnayoiona kwa hiyo usishangae kuona nikiinvolve majority. Wanawake wengi wa kipindi hiki hawana sifa za kuitwa wake, wengi wao ni wavivu kwanzia kufikiri na wana golddigging traits... The representative sampling suffices, angalia tu hata humu jamiiforum wanawake wanaokuja kutafuta partners style wanayoingia nayo..

eti mtu anakwambia asiwe mweusi sana awe maji ya kunde! serious hiv kweli una akili zako timamu hicho kinaweza kuwa ni kigezo cha kuangalia ukiwa unatafuta mume?

Haya sijui eti mara awe na degree pia na kazi nzuri..!! huu si ni upuuzi? je kama hana kazi nzuri kwa muda huo lakini kupitia wewe kwa network uliyonayo unaweza kumfanya akawa na kazi nzuri tu hapo tayari mkiwa kwenye mahusiano. Na sidhani kama hata huwa wanafikiria hili.

Kupitia hawa na hizi sababu zao chache unaweza kuona jinsi gani mabinti wengi wanavyokosa material ya kuitwa wife, na hawa ni reflection ya waliopo huko mitaani. Yaani wengi wanapenda mwanaume ambaye tayari yuko accomplished Najua hii sio kwa wanawake wote ila kwa hawa waliozaliwa miaka ya 80s kuja huku juu wengi wako hivyo. They are too selective and lazzy.

Wanaume tuna makosa yetu na tumechangia kwa kiasi kikubwa sana kuwaharibu hawa wanawake na sasa hatuna budi kuubebea huu msalaba.

Mwisho kabisa niseme kama Michelle wapo tanzania hii but finding one is like a needle in haystack.
Nilipomuongelea mama magufuli nilimuweka kwenye kundi la wanawake walioanzia chini na waume zao,unaweza usiuone mchango wake kwa muono wako kwasababu unataka kumlinganisha na mwingine lkn mchango wake anaujua mumewe. Kumbuka mke ni image ya mumewe kwahiyo michelle alikuwa image ya Obama, unapomsifia Michelle hauwezi ukaacha kumsifia Obama maana asingekuwa na Obama maybe asingekuwa Michelle tunaemfahamu.

Kuhusu wanawake wenye kipato kikubwa kuliko waume zao mie nawashuhudia wengi tu huku mitaani na maisha yanasonga vizuri tu.

Hao wanaotafuta waume kwa vigezo vya rangi hata wanaume wanachagua hivyo nashangaa kwanini umeegemea upande wa wanawake tu,maybe wanawake hawapaswi kuwa na choices bali anayekuja ye ajibebee tu, mtu anakuwa na yule aliyemridhia kama ambavyo michelle alimridhia obama maana alikidhi vigezo vyake.

Hii ya wanawake wa sasa kuangalia mwanaume ambae ana unafuu wa maisha ni kwakuwa maisha yamebadilika mpendwa,sio kama zamani mkikosa mboga utakwenda kuchuma hata kwenye shamba la jirani. hakuna anaependa shida ndio maana angalia hata thread za wanaume wanaotafuta wachumba utaona anahitaji alojiajiri au aloajiriwa,wengine mwenye elimu fulani,kwakuwa birds of the same feadhers flies together.

Vigezo vyako vinaweza visiwe vya yule, kwahiyo heshimu tu vigezo vya mwenzio. Hata wanaume wa sasa walio wengi hauwezi kuwalingalisha na baba/babu zetu kuna vingi wanakosa.

Itoshe kusema nyakati zimebadilika and alot hv changed, usitegemee mwanamke awe wa 50s wakati we ni wa 80s. Ila wanawake wema na wanaume wema still wapo wengi tu ni vile wewe unavyochanga karata zako kuwapata.
 
Hakuna kitu hapo alifanya usanii tu, inaonekana huwajui vizuri wazungu
Hebu wakati mwingine muwe positive jamani, mbona hamna jema. Au ndio ile mtu akiona kwake kunaungua basi anaamini na kwa wenzie ni vivyo hivyo na kama sio hivyo basi wanapretend!!!
 
Ndo hapo mtu anabaki kulalama hampati Michelle, sasa mtu anampataje Michelle wakati yeye si Obama bali Joseph Konyi

Maana unakuta akina Michelle wote wako kwa Obama zao. Yeye atabaki tu na wa size yake.... Hahaha

Na kumbuka Michelle hawezi kuwa Michelle bila Obama, na Obama hawezi kuwa Obama bila Michelle.... If u know what am talking about...
hilarious comment
 
Wanawake au wanaume wachache sana wanaweza kuchukua ndoto za wenzi wao na kuzifanya zao(as a team). Kuna tamthilia "House of Cards" Frank and Claire Underwood inatoa mwangaza fulani hivi wa maisha ya ndoa unapokua mtu maarufu au wadhifa mkubwa kwenye jamii.

House of cards ntaanza kuiangalia week ijayo. Nmeshaiweka kwenye list
 
Mnafiki tu huyo analia na Mengi akiwaza jinsi alivyoikuta Libya na jinsi alivyoiacha, mauaji na ubaguzi wa waziwazi kwa wamarekani weusi kwanini chozi lisimtoke?
 
Hakika wametoka mbali Lizarazu.
Sana...

Vipi lakin mkuu we wako hamjatoka nae mbali?

mimi wangu nilikutana nae la nne baada ya mimi kurudia darasa na ndio alinisaidia sana kuvuka kwenda la tano, huwezi amini hadi leo hii niko nae.
 
Sana...

Vipi lakin mkuu we wako hamjatoka nae mbali?

mimi wangu nilikutana nae la nne baada ya mimi kurudia darasa na ndio alinisaidia sana kuvuka kwenda la tano, huwezi amini hadi leo hii niko nae.
Una bahati sana mkuu. Hapana ni hukuhuku juu.
 
Ni kweli. Kuna shida mahali. Wanaume wengi wanatembea peke yao kwenye ndoto zao.
Shida inaanzia kwa wazazi, ukimwambia ndoto anakusimanga na kukukatisha tamaa wengi wao wanasema dhahiri, wewe fulani huwezi labda uwe mwalimu,n.k huwezi kuwa raisi,n.k. Itakuaje kwa mwanamke uliyekutana nae atakuelewa vipi?

Personally ninaushuhuda wa rafiki yangu, alimuuza mchumba wake kama yeye akiwa mtu mwenye nyadhifa au umaarufu mjini ataweza stress za magezetini na vyombo vya habari? Dada kafunguka, yeye hawezi kabisa...atapendelea kama wataishi maisha ya chini, watoto wasome shule nzuri, chakula kiwepo nyumbani, aweze kuvaa vizuri basi.

Shida ipo kwenye jamii. Wahindi an ideal husband ni yule mwenye mabavu na uwezo wa kupambana na "social evils" ambazo huwakumba wanawake wa India kwa sehemu kubwa. Ila hapa kwetu wanawake wanapenda wanaume wenye pesa maana jamii yetu janga kubwa ni umasikini. Tunaamini ukiwa na pesa kila kitu kitakua sawa, kiasi kwamba wengi huamini ugomvi wa wazazi waliokuwa wakiuona walipokua wadogo chanzo ni pesa. Hivyo mume akiwa na pesa hakuna shida tena.
 
Dahhh very true. Kuna mtu niliachana kwa kumwambia "tunaachana kwasababu nakupenda sana, siku moja naweza kufa kama nitaendelea kuishi na wewe"

Mapenzi ya siku hizi, everyone either he or she is on guards every time. Unakua ka vile upo kwenye mahusiano na some sort of nemesis. Kila siku mashindano, who talk more smarter,more responsible, more everything.....

All in all deep down within us, ipo roho yenye upendo ila tunaogopa kupenda. Love has become a vice not a virtue
Katika kupenda naamini ni vema kuanza kumpenda mtu kwa asilimia 100 halafu zitabaki au kupungua kutokana na mtu atakapolipokea na kulienzi pendo lako kwake.

Kuliko kuanza na asilimia 0 ukitegemea penzi liongezeke kadri mtu atakavyokuwa anakujali na kukuenzi. Hili ni pendo la kinafiki na bahati mbaya wengi wapo kwenye aina hii ya kupenda.
 
.................................. Ila hapa kwetu wanawake wanapenda wanaume wenye pesa maana jamii yetu janga kubwa ni umasikini. Tunaamini ukiwa na pesa kila kitu kitakua sawa, kiasi kwamba wengi huamini ugomvi wa wazazi waliokuwa wakiuona walipokua wadogo chanzo ni pesa. Hivyo mume akiwa na pesa hakuna shida tena.
Sawa mkuu. Acha tutafute pesa kwa bidii tutimize ndoto zao.
 
Inaizidi hata couple ya jay z na beyonce ?
Hao nao wana historia nayo,kwa kumbu kumbu nilizo nazo jigga & be wanaishi kwa utii fulan,coz ata ukiangalia age zao jigga mkubw kwa 12 ivi ...bt michele & obama only 3 yrs ivi ndo mana kuna greit respect 1 anothr,ata scandal zao sio kama za kina jay & beyonc ni zile za muda,readily undercorrection....still hawafiki obama & michelle....kinda lyk dem nd ar ril greit
 
Obama aongea haya kwa hisia mpaka chozi likamdondoka.

“For the past 25 years you have not only been my wife and mother of my children, you have been my best friend. You took on a role you didn’t ask for. And you made it your own with grace and with grit and with style, and good humor.”

"Kwa miaka zaidi ya 25 iliyopita, umekuwa sio tu mke wangu na mama wa watoto wangu lakini rafiki yangu mkubwa.Ulichukua jukumu ambalo hukuuliza na ukalifanya kuwa lako kwa neema , ujasiri, mipango na ucheshi mzuri. Uliifanya Ikulu kuwa sehemu ya kila mtu."

Nasi si vibaya tukiwa marafiki wakubwa wa wapenzi wetu (Ambao sio) . Tuchukue majukumu ya wenza wetu na kuyafanya ya kwetu na maisha yatakuwa raha mustarehe kwa miaka mingi. Utakumbukwa na mwenzako baada ya miaka mingi mpaka atamwaga chozi kama ilivyotokea kwa mkuu Obama.

View attachment 459965
Unajua ni kwa nini alilia? Analia sababu anajua mwisho wa ndoa yake umefikia. Inasemekana, "eti", Michelle alikuwa anataka kumwaga Obama siku nyingi tu lakini kwa sababu ya Urais akaona atachafua hali ya hewa, hivyo akaamua kusubiria jamaa amalize muda wake ndio amteme. Kama hizi tetesi zinaukweli basi itajulikana muda sio mrefu.
 
Katika kupenda naamini ni vema kuanza kumpenda mtu kwa asilimia 100 halafu zitabaki au kupungua kutokana na mtu atakapolipokea na kulienzi pendo lako kwake.

Kuliko kuanza na asilimia 0 ukitegemea penzi liongezeke kadri mtu atakavyokuwa anakujali na kukuenzi. Hili ni pendo la kinafiki na bahati mbaya wengi wapo kwenye aina hii ya kupenda.
Hujawai kutana na matapeli wa mapenzi, jamii inabadilika kutokana na makosa ya jana. Mtu anakwambia anakupenda na wewe unampa hizo 100% baada ya 2 months ikatokea una mimba anakukana, na hamjafahamiana kiasi hicho kwamba inamjua kaka, dada au kwao. Wewe utafanya nini?
 
Unajua ni kwa nini alilia? Analia sababu anajua mwisho wa ndoa yake umefikia. Inasemekana, "eti", Michelle alikuwa anataka kumwaga Obama siku nyingi tu lakini kwa sababu ya Urais akaona atachafua hali ya hewa, hivyo akaamua kusubiria jamaa amalize muda wake ndio amteme. Kama hizi tetesi zinaukweli basi itajulikana muda sio mrefu.
Du! Hii bado sijaipata.
 
Hujawai kutana na matapeli wa mapenzi, jamii inabadilika kutokana na makosa ya jana. Mtu anakwambia anakupenda na wewe unampa hizo 100% baada ya 2 months ikatokea una mimba anakukana, na hamjafahamiana kiasi hicho kwamba inamjua kaka, dada au kwao. Wewe utafanya nini?
Navyosema kumpenda mtu kwa asilimia 100 haina maana niwe mjinga. Mtu kuniambia ananipenda haimaanishi ananipenda kweli, inawezekana amenitamani tu.
Na hakuna upendo wa maneno, upendo ni matendo...nukta

Na kwa hiyo scenario yako hivi mtu hata simjui vizuri na wala hatujakubaliana tuzae, naanzaje kubeba mimba???? Siwezi
 
Nilipomuongelea mama magufuli nilimuweka kwenye kundi la wanawake walioanzia chini na waume zao,unaweza usiuone mchango wake kwa muono wako kwasababu unataka kumlinganisha na mwingine lkn mchango wake anaujua mumewe. Kumbuka mke ni image ya mumewe kwahiyo michelle alikuwa image ya Obama, unapomsifia Michelle hauwezi ukaacha kumsifia Obama maana asingekuwa na Obama maybe asingekuwa Michelle tunaemfahamu.

Kuhusu wanawake wenye kipato kikubwa kuliko waume zao mie nawashuhudia wengi tu huku mitaani na maisha yanasonga vizuri tu.

Hao wanaotafuta waume kwa vigezo vya rangi hata wanaume wanachagua hivyo nashangaa kwanini umeegemea upande wa wanawake tu,maybe wanawake hawapaswi kuwa na choices bali anayekuja ye ajibebee tu, mtu anakuwa na yule aliyemridhia kama ambavyo michelle alimridhia obama maana alikidhi vigezo vyake.

Hii ya wanawake wa sasa kuangalia mwanaume ambae ana unafuu wa maisha ni kwakuwa maisha yamebadilika mpendwa,sio kama zamani mkikosa mboga utakwenda kuchuma hata kwenye shamba la jirani. hakuna anaependa shida ndio maana angalia hata thread za wanaume wanaotafuta wachumba utaona anahitaji alojiajiri au aloajiriwa,wengine mwenye elimu fulani,kwakuwa birds of the same feadhers flies together.

Vigezo vyako vinaweza visiwe vya yule, kwahiyo heshimu tu vigezo vya mwenzio. Hata wanaume wa sasa walio wengi hauwezi kuwalingalisha na baba/babu zetu kuna vingi wanakosa.

Itoshe kusema nyakati zimebadilika and alot hv changed, usitegemee meanamke awe wa 50s wakati we ni wa 80s. Ila wanawake wema na wanaume wema still wapo wengi tu ni vile wewe unavyochanga karata zako kuwapata.

Naheshimu sana mawazo mpendwa na bila shaka tunaelewana vizuri. Nakubali kuwa mke ni image ya mumewe na ndio maana hata pengine mkanganyiko uliomo kwenye familia ya mkuluu yaani yeye na mke wake umechangia aonekane mtu wa ajabu ajabu tu kila leo amekosa mpaka huruma kwa familia nyingi za kitanzania hadi kufikia hatua kutuambia tufe na njaa.

Hiyo ya wanawake wenye nguvu kiuchumi na elimu kubwa kuolewa na wanaume wenye nguvu ndogo kiuchumi na elimu ndogo asee labda utakuwa unaziona huko mtaani unakoishi ila kwa ndoa nyingi nnazoziona mimi it is absolutely opposite na huko mtaani kwako.

Alafu nimelezea zaidi kwa kuegemea wanawake kulingana na topic yenyewe nilivyoikuta lakini pamoja na hivyo kuna mahali nime admit kuwa hata sisi wanaume tunatakiwa kuwa responsible coz we all have fair share in current situations, kuhusu kuwa na machaguo sikatai ila kuwa na vigezo vilivyopitiliza bila hata kufikiria kwa kina kuhusu vigezo hivyo huo ni upuuzi mkubwa. Bila shaka wewe mwenyewe unajua ni jinsia gani hasa inayokujaga na vigezo vingi.

Point kubwa hapo labda ni nyakati kubadilika kiuchumi na hii ndio imefanya huu uharibifu wote uwepo kiasi cha mapenzi kugeuka biashara na geniune love imekuwa replaced na vitu vingi ndio ile mtu anakupenda baada ya kuona una huakika wa kumlisha. Hivyo hatuna budi kucopy uhalisia uliopo.
 
Unajua ni kwa nini alilia? Analia sababu anajua mwisho wa ndoa yake umefikia. Inasemekana, "eti", Michelle alikuwa anataka kumwaga Obama siku nyingi tu lakini kwa sababu ya Urais akaona atachafua hali ya hewa, hivyo akaamua kusubiria jamaa amalize muda wake ndio amteme. Kama hizi tetesi zinaukweli basi itajulikana muda sio mrefu.
Hahaha
Hii nayo habari mpya sijawahi skia
Landa ntafuatilia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom