PostGE2025 Heche: CHADEMA imetoa mawakili nchi nzima kwa watu wote wenye kesi za uhaini, hakuna kurudi nyuma hadi ukombozi upatikane

PostGE2025 Heche: CHADEMA imetoa mawakili nchi nzima kwa watu wote wenye kesi za uhaini, hakuna kurudi nyuma hadi ukombozi upatikane

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bara John Wegesa Heche amesema chama hicho kwa kitatoa mawakili kwa wote walioshtakiwa kesi za uhaini nchi nzima

Akizungumza nje ya viunga vya Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Dar es Salaam leo Novemba 12, 2025 baada ya kusikilzwa kwa kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu, Heche amebainisha kuwa chama hicho hakitarudi nyuma kitaendelea kusonga mbele

"hakuna kurudi nyuma mpaka nchi hii itakapopata ukombozi", amesema Heche

Heche amerejelea kauli ya Umoja wa Mataifa kutaka uchunguzi kufanyika kwa mauaji yaliyotokea na madai ya miili kuchukuliwa na vyombo vya usalama kupelekwa kusiko julikana ili kupoteza ushahidi, akisema vyombo vya kitaifa ndivyo vifanye uchunguzi huo 'na siyo vyombo vya dola vya Tanzania
,
Pamoja na hayo amebainisha kuwa vikao vya Sektretarieti pamoja na Kamati Kuu ya chama hicho vitaanza muda wowote vikilenga kutoa msimamo wa juu ya matukio yaliyotokea Oktoba 29, 20205 nchini


 
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bara John Wegesa Heche amesema chama hicho kwa kitatoa mawakili kwa wote walioshtakiwa kesi za uhaini nchi nzima.

Akizungumza nje ya viunga vya Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Dar es Salaam leo Novemba 12, 2025 Heche amebainisha kuwa chama hicho hakitarudi nyuma kitaendelea kusonga mbele.

"hakuna kurudi nyuma mpaka nchi hii itakapopata ukombozi", amesema Heche.

Pamoja na hayo amebainisha kuwa vikao vya Sektretarieti pamoja na Kamati Kuu ya chama hicho vitaanza muda wowote vikilenga kutoa msimamo wa juu ya matukio yaliyotokea Oktoba 29, 20205 nchini.

 
Back
Top Bottom