Haya ndiyo maridhiano tuyatakayo wananchi dhidi ya Serikali

Rabbon

JF-Expert Member
Apr 16, 2022
15,162
22,677
Napoongelea maridhiano kati ya Wananchi na Serikali naomba nieleweke kuwa, simaanishi aina Ile ya maridhiano kati ya CCM na ACT kule visiwani,

Maridhiano nayoongelea Si yake ya Mh Mbowe na kinana na team yake ambayo yaliendelea zaidi ya mwaka huku tukiendelea kukandamizwa na TOZO na Mfumuko wa bidhaa tukipewa sababu hafifu,

Maridhiano nibayoongelea yalenge yafuatayo;

1. RUSHWA iwe historia

Hatufurahishwi kusikia Majina ya viongozi wastaafu yakionekana kujirudia kijirithisha madaraka.

Hatutaki kusikia madawa hospitalini yakigawiwa Kwa upendeleo.

Mbolea Kwa wakulima ya ruzuku itufikie Kwa wakati bila Kutoa RUSHWA. Nk nk nk

2. Tunataka Sanduku la kura lirudi mahala pake

Tumechoka kusikia idadi ya wapiga kura kituoni ni 200 Kwa mfano, lakini katika matokeo zikihesabiwa tunapata idadi jumla ikiongezea na kufikia 250.

Wananchi tunajiuliza, hizo kura 50 Huwa zinaingizwa na maruhani ndani ya ballot box?

Wananchi pia tunataka wagombea tunaowataka ndio Majina Yao yarudishwe, hatutaki kuletewa wagombea wa mfukoni.

3. Umeme, maji na huduma za JAMII za uhakika

Hatutaki blaa blaa, pesa za kulipa bill ya umeme tunazo lakini umeme hamna,

Pesa ya kulipa bill ya maji IPO lakini maji hayatoki bombani!!

Tukilipia vifurushi vya data mitandaoni hatutaki kusikia hamna mtandao, hayatuhusu.

3. Huduma za AFYA

Maridhiano tuyatakayo ni dawa ziwepo za kutosha mahispitalini, Kumwambia mgonjwa kuwa hakuna madawa Hilo halimuhusu.

4. Miundombinu ya barabara

Maridhiano tuyatakayo ni barabara zijengwe za kutosha zitakazohimili msimu mzima.

Hatutaki kusikia mawasiliano ya barabara yakikatika na kutuzuia kufika tupatakapo.

5. Bima za AFYA

Maridhiano kati ya mama Serikali na mama mjamzito yafanyike Ili ijulikane mtoto atakayezaliwa anastahili matibabu ya bima Bure au la!!

Si sawa watoto wa maskini wazuiwe kupata bima wakati viongozi wakitibiwa Bure nje ya nchi Kwa Kodi za sirikali.

6. KILIMO

Maridhiano yafanyike, Kila Kijiji kikopeshwe tractors za KILIMO kupitia Benki ya KILIMO Ili kuepuka KILIMO Cha jembe la mkono.

7. ELIMU

Maridhiano yafanyike kuhakikisha chakula Bure mashuleni kinarudishwa kama enzi za Mwl Nyerere.

Walimu wapewe overtime wanaposahihisha mitihani au kutunga mitihani nje ya muda wa KAZI.

8. Madini

Maridhiano yafanyike wananchi tupate 50/50 katika mgao wa madini yetu.

Wazawa wakopeshwe na wasaidiwe zana za kisasa za kuchimba madini bila kuharibu mazingira.


9. UTUMISHI wa Umma

Maadili ya viongozi yarudi mahala pake, watumishi wa umma waache kufanya biashara ndani ya Serikali. Hili linahitaji maridhiano.

Ndugu Mwananchi unakaribishwa kuongeza eneo ambalo ungependa maridhiano yafanyike kati yetu na sirikali Ili Nchi ipumue.

Angalizo: Wananchi hatufurahishwi na TABIA ya viongozi Wachache wa Vyama vya siasa kujifungia sirini kujadili issues tusozijua Wala kushirikishwa, maridhiano yanatakiwa yawe ya WAZI peupe, sababu hii ni Nchi yetu sote, Nchi hii si ya CCM, CHADEMA na ACT pekee.

ASALI ni tamu, hivyo ni muhimu wote turambe Kwa haki, Si Wachache Kwa RUSHWA.

Karibu🙏. Amen

Itaendelea......!!
 
10. Maridhiano yanayohitajika ni kuhusu aina Gani ya Uchumi tuiendee,

Tujadiliane ikiwa tufuate sera za Ujamaa, Ubepari au mixture ya Ubepari na Ujamaa.
 
11. Mkataba wetu wananchi na Serikali yaani Katiba:

A: Asiwepo kiongozi wa Sirikali, Wabunge au Taasisi itakayochezea Katiba yetu Kwa kuongeza au kupunguza chochote bila ridhaa au kura ya maoni kwa wananchi wote.

Maridhiano ni muhimu kuondoa sintofahamu.

KATIBA ya nchi Si kijitabu tu,

B: Ndani ya kitabu kiitwacho KATIBA, Kuna wananchi zaidi ya mil 60.

Ndani ya KATIBA Kuna Pande kubwa la ardhi ya Watanzania , Rais wa Nchi amepewa kuilinda ardhi na kuisimamia,

Ni MARUFUKU kuuza ardhi Kwa wageni, KATIBA imekataza.

C: Pia ndani ya Katiba Kuna majeshi yote ya ulinzi na USALAMA, hivyo kitabu hiki Si Cha kawaida.

Ndani ya Katiba zimo fursa zote za kiuchumi,kijamii na kisiasa ambazo wananchi wanatakiwa wapewe Kwa usawa na HAKI.
 
12. Maridhiano juu ya pension ya wastaafu.

Maridhiano yanahitajika kupatikana maana Kuna unyanyasaji inaendelea Kwa wazee wetu,

Haiwezekani pension zitolewe Kwa watumishi wa umma pekee,

Nchi yetu ni ya wakulima na wafanyakazi, hivyo wakulima pia wana HAKI kupata pension maana alishiriki kuilisha Nchi Hadi mgongo ukapinda uzeeni.
 
Ikiwa HOJA hizi za wananchi zitapuuzwa, thead hii itunzwe Hadi pale chama kipya kitapoongoza Serikali kishike hatamu.
Ninavyoelewa maridhiano ni kuhusiana na:
1. wananchi wanahitaji Katiba ya namna gani ili waweze kujitawala Kwa denikrasia sahihi.....inayoweza kusema Mbunge asiwe Waziri, Mbunge angalau awe na kisomo say kuanzia diploma etc
2. Utaratibu wa uchaguzi ukoje.....tume huru ya uchaguzi, MaDED ambao mara nyingi ni makada na chama tawala wasiwe sehemu ya tume huru.
3. Mahakama huru
4. Uchaguzi Mkuu uhojiwe mahakamani incase kama mgombea wa kitu cha urais akicheza rafu za kisiasa
5. Katiba inayosema hakutakuwa na nafasi ya naDC na Makatibu Tarafa badala yake kunakuwa na RC ambaye chini yake kuna DEDs, Watendaji Kata, Watendaji na Mtaa/kijiji
5. Wananchi wawe na uwezo wa kumwajibisha Mbunge na diwani kama hawatekelezi wajibu wao kwa sababu ya uzembe badala ya utaratibu wa sasa ambapo chama ndo chenye madaraka hayo.
5. Katiba iruhusu mgombea huru kuanzia ngazi Rai's, Mbunge na Diwani. Isiwe lazima kupitia chama cha siasa.
Mengine yote; mambo ya umeme, maji, rushwa iwe ni sera ya chama husika. Chama kitakachoshindwa kutekeleza hayo wananchi wawe na nguvu ya kukipiga chini.
 
11. Mkataba wetu wananchi na Serikali yaani Katiba:

A: Asiwepo kiongozi wa Sirikali, Wabunge au Taasisi itakayochezea Katiba yetu Kwa kuongeza au kupunguza chochote bila ridhaa au kura ya maoni kwa wananchi wote.

Maridhiano ni muhimu kuondoa sintofahamu.

KATIBA ya nchi Si kijitabu tu,

B: Ndani ya kitabu kiitwacho KATIBA, Kuna wananchi zaidi ya mil 60.

Ndani ya KATIBA Kuna Pande kubwa la ardhi ya Watanzania , Rais wa Nchi amepewa kuilinda ardhi na kuisimamia,

Ni MARUFUKU kuuza ardhi Kwa wageni, KATIBA imekataza.

C: Pia ndani ya Katiba Kuna majeshi yote ya ulinzi na USALAMA, hivyo kitabu hiki Si Cha kawaida.

Ndani ya Katiba zimo fursa zote za kiuchumi,kijamii na kisiasa ambazo wananchi wanatakiwa wapewe Kwa usawa na HAKI.
Uuuuwiii! Wewe noma kwelikweli. Maridhiano na tunu mnazokubaliana mathalani kusalimia shikamoo, kuacha matusi, kuacha uongo, kuheshimu Muungano, na kedhalika. Kujenga lami Lindi au airport Chato hizo ni sera, ili wasiotaka lami wakunyime kura zao (CHADEMA) na wanaotaka airport (CCM) wakupe zao. Manake ndo CHADEMA wakaambulia 87%/13% kama 2020.
 
Uuuuwiii! Wewe noma kwelikweli. Maridhiano na tunu mnazokubaliana mathalani kusalimia shikamoo, kuacha matusi, kuacha uongo, kuheshimu Muungano, na kedhalika. Kujenga lami Lindi au airport Chato hizo ni sera, ili wasiotaka lami wakunyime kura zao (CHADEMA) na wanaotaka airport (CCM) wakupe zao. Manake ndo CHADEMA wakaambulia 87%/13% kama 2020.
Najaribu kukuelewa,

Wananchi tunachopinga ni wanasiasa kujifungia vyumba vya Siri kujadiliana jinsi ya kugawana madaraka ilhali Nchi Iko GIZANI.

Ndomana nasemaje, maridhiano ni Umeme wa uhakika uwepo.

Sera zipi zitatumika haituhusu!!
 
Ninavyoelewa maridhiano ni kuhusiana na:
1. wananchi wanahitaji Katiba ya namna gani ili waweze kujitawala Kwa denikrasia sahihi.....inayoweza kusema Mbunge asiwe Waziri, Mbunge angalau awe na kisomo say kuanzia diploma etc
2. Utaratibu wa uchaguzi ukoje.....tume huru ya uchaguzi, MaDED ambao mara nyingi ni makada na chama tawala wasiwe sehemu ya tume huru.
3. Mahakama huru
4. Uchaguzi Mkuu uhojiwe mahakamani incase kama mgombea wa kitu cha urais akicheza rafu za kisiasa
5. Katiba inayosema hakutakuwa na nafasi ya naDC na Makatibu Tarafa badala yake kunakuwa na RC ambaye chini yake kuna DEDs, Watendaji Kata, Watendaji na Mtaa/kijiji
5. Wananchi wawe na uwezo wa kumwajibisha Mbunge na diwani kama hawatekelezi wajibu wao kwa sababu ya uzembe badala ya utaratibu wa sasa ambapo chama ndo chenye madaraka hayo.
5. Katiba iruhusu mgombea huru kuanzia ngazi Rai's, Mbunge na Diwani. Isiwe lazima kupitia chama cha siasa.
Mengine yote; mambo ya umeme, maji, rushwa iwe ni sera ya chama husika. Chama kitakachoshindwa kutekeleza hayo wananchi wawe na nguvu ya kukipiga chini.
Nimejaribu kuongea lugha ya wananchi vijijini,

Sera hatuhusu, wanasiasa wakijifungia kujadili vyeo, wajue wananchi tunataka umeme wa HAKIKA, maji nk nk.

Maridhiano ni kuhakikisha Umaskini wa watz unaondoka, na huduma muhimu zinapatikana.
 
13: Tukae chini tukubaliane kuwa ni MWIKO watumishi wa Serikali wa Umma Hasa viongozi wa level ya juu kufanya biashara.

Jambo hili linasababisha watumishi hao kuinflate Bei za bidhaa au huduma kuliko kawaida sababu ya connection na kulindana.

Mzigo wanaomsababishia MKULIMA na mfanyakazi ni mkubwa.
 
Ninavyoelewa maridhiano ni kuhusiana na:
1. wananchi wanahitaji Katiba ya namna gani ili waweze kujitawala Kwa denikrasia sahihi.....inayoweza kusema Mbunge asiwe Waziri, Mbunge angalau awe na kisomo say kuanzia diploma etc
2. Utaratibu wa uchaguzi ukoje.....tume huru ya uchaguzi, MaDED ambao mara nyingi ni makada na chama tawala wasiwe sehemu ya tume huru.
3. Mahakama huru
4. Uchaguzi Mkuu uhojiwe mahakamani incase kama mgombea wa kitu cha urais akicheza rafu za kisiasa
5. Katiba inayosema hakutakuwa na nafasi ya naDC na Makatibu Tarafa badala yake kunakuwa na RC ambaye chini yake kuna DEDs, Watendaji Kata, Watendaji na Mtaa/kijiji
5. Wananchi wawe na uwezo wa kumwajibisha Mbunge na diwani kama hawatekelezi wajibu wao kwa sababu ya uzembe badala ya utaratibu wa sasa ambapo chama ndo chenye madaraka hayo.
5. Katiba iruhusu mgombea huru kuanzia ngazi Rai's, Mbunge na Diwani. Isiwe lazima kupitia chama cha siasa.
Mengine yote; mambo ya umeme, maji, rushwa iwe ni sera ya chama husika. Chama kitakachoshindwa kutekeleza hayo wananchi wawe na nguvu ya kukipiga chini.
Kwa UFUPI ni kwamba tunahitaji KATIBA MPYA ILIYO BORA kwa maaana;
1.Shirikishi
2.Itakayotoa mgawanyo ulio sawa wa MHIMILI ya DOLA
3.Itakayoheshimu na kulinda UTAWALA wa SHERIA
4.Itakayopunguza madaraka ya Mfalme/Malkia, Rais wetu
5.Itakayorudisha madaraka makubwa kwa wananchi
6.Yenye TUNU za TAIFA
7.Itakayo LINDA kwa NGUVU zote MALI ASILI za Taifa
 
Kwa UFUPI ni kwamba tunahitaji KATIBA MPYA ILIYO BORA kwa maaana;
1.Shirikishi
2.Itakayotoa mgawanyo ulio sawa wa MHIMILI ya DOLA
3.Itakayoheshimu na kulinda UTAWALA wa SHERIA
4.Itakayopunguza madaraka ya Mfalme/Malkia, Rais wetu
5.Itakayorudisha madaraka makubwa kwa wananchi
6.Yenye TUNU za TAIFA
7.Itakayo LINDA kwa NGUVU zote MALI ASILI za Taifa
Thanks, Ubarikiwe.
 
1. RUSHWA iwe historia

Hatufurahishwi kusikia Majina ya viongozi wastaafu yakionekana kujirudia kijirithisha madaraka.

Hatutaki kusikia madawa hospitalini yakigawiwa Kwa upendeleo.

Mbolea Kwa wakulima ya ruzuku itufikie Kwa wakati bila Kutoa RUSHWA. Nk nk nk

2. Tunataka Sanduku la kura lirudi mahala pake

Tumechoka kusikia idadi ya wapiga kura kituoni ni 200 Kwa mfano, lakini katika matokeo zikihesabiwa tunapata idadi jumla ikiongezea na kufikia 250.

Wananchi tunajiuliza, hizo kura 50 Huwa zinaingizwa na maruhani ndani ya ballot box?

Wananchi pia tunataka wagombea tunaowataka ndio Majina Yao yarudishwe, hatutaki kuletewa wagombea wa mfukoni.

3. Umeme, maji na huduma za JAMII za uhakika

Hatutaki blaa blaa, pesa za kulipa bill ya umeme tunazo lakini umeme hamna,

Pesa ya kulipa bill ya maji IPO lakini maji hayatoki bombani!!

Tukilipia vifurushi vya data mitandaoni hatutaki kusikia hamna mtandao, hayatuhusu.

3. Huduma za AFYA

Maridhiano tuyatakayo ni dawa ziwepo za kutosha mahispitalini, Kumwambia mgonjwa kuwa hakuna madawa Hilo halimuhusu.

4. Miundombinu ya barabara

Maridhiano tuyatakayo ni barabara zijengwe za kutosha zitakazohimili msimu mzima.

Hatutaki kusikia mawasiliano ya barabara yakikatika na kutuzuia kufika tupatakapo.

5. Bima za AFYA

Maridhiano kati ya mama Serikali na mama mjamzito yafanyike Ili ijulikane mtoto atakayezaliwa anastahili matibabu ya bima Bure au la!!

Si sawa watoto wa maskini wazuiwe kupata bima wakati viongozi wakitibiwa Bure nje ya nchi Kwa Kodi za sirikali.

6. KILIMO

Maridhiano yafanyike, Kila Kijiji kikopeshwe tractors za KILIMO kupitia Benki ya KILIMO Ili kuepuka KILIMO Cha jembe la mkono.

7. ELIMU

Maridhiano yafanyike kuhakikisha chakula Bure mashuleni kinarudishwa kama enzi za Mwl Nyerere.

Walimu wapewe overtime wanaposahihisha mitihani au kutunga mitihani nje ya muda wa KAZI.

8. Madini

Maridhiano yafanyike wananchi tupate 50/50 katika mgao wa madini yetu.

Wazawa wakopeshwe na wasaidiwe zana za kisasa za kuchimba madini bila kuharibu mazingira.


9. UTUMISHI wa Umma

Maadili ya viongozi yarudi mahala pake, watumishi wa umma waache kufanya biashara ndani ya Serikali. Hili linahitaji maridhiano.

Ndugu Mwananchi unakaribishwa kuongeza eneo ambalo ungependa maridhiano yafanyike kati yetu na sirikali Ili Nchi ipumue.

Angalizo: Wananchi hatufurahishwi na TABIA ya viongozi Wachache wa Vyama vya siasa kujifungia sirini kujadili issues tusozijua Wala kushirikishwa, maridhiano yanatakiwa yawe ya WAZI peupe, sababu hii ni Nchi yetu sote, Nchi hii si ya CCM, CHADEMA na ACT pekee.

ASALI ni tamu, hivyo ni muhimu wote turambe Kwa haki, Si Wachache Kwa RUSHWA.

Karibu🙏. Amen

Itaendelea......!!
Haya yote ni magumu san kiutekelezaji kwa CCM!! Na hapa ndipo unajifunza tu hawa watu wana nia gan juu ya Tanzania, majibu nadhan kila mmoja anaelewa when anapogundua hayo hapo juu hawataki na hawawez tekeleza!! Na mamb ya msingi kama haya huez ona machawa akina Lucas mwashamba, choiceVariable, Faizafoxy, covax, CM hawa wote hawez changia positive kweny mamb kama haya wala kutoa solutions!! Wao ni praise and worship!
 
Haya yote ni magumu san kiutekelezaji kwa CCM!! Na hapa ndipo unajifunza tu hawa watu wana nia gan juu ya Tanzania, majibu nadhan kila mmoja anaelewa when anapogundua hayo hapo juu hawataki na hawawez tekeleza!! Na mamb ya msingi kama haya huez ona machawa akina Lucas mwashamba, choiceVariable, Faizafoxy, covax, CM hawa wote hawez changia positive kweny mamb kama haya wala kutoa solutions!! Wao ni praise and worship!
Ndugu Pac the Don, ni usiku saana, Giza ni Totoro na wingu zito limeifunika Nchi.

Kinachotupa waonaji matumaini ni Nuru njema sana itakayon'gaa patakapokucha, maana tangu kuumbwa Kwa Dunia, jua halijawahi goma chomoza na kuliachia Giza kutawala milele.

Ni Kweli ujumbe unaweza onekana hautekelezeki Kwa waliopo,

Lakini amini nakwambia, Nyuzi za aina hii zitafukuliwa Ili zifanyiwe KAZI atakapoinuka Mtawala sahihi.

Amen
 
14. Maridhiano kuhusu VYOMBO vya habari, ujulikanao kama mhimili wa nne.

Kumekuwepo na jitihada za chini Kwa chini kuzima sauti ya wananchi kumulika UOVU na mapungufu ya viongozi na uongozi wetu,

Wananchi tunataka mihimili iheahimiane na ifanye KAZI na majukumu yake Kwa uhuru.

TBC na vyombo vingine viruhusiwe Kutoa habari Kwa HAKI bila kupangiwa Wala kutishwa.

Sakata la Bandari na mkataba wa kimangungo utufunze kutorudia makosa hayo.

Si sawa, Mtu aliyevaa BOOT kubwa kusimama juu ya mguu wa Mwananchi aliye peku halafu akitoa sauti ya ukelele kuonyesha anavyoumia, anaambiwa anyamaze, wakati huo huo akiendelea kuumizwa.

Nchi ni yetu sote, pasiwepo na First , middle au lower class citizens,

Nchi ni yetu sote.

Amen
 
Ndugu Pac the Don, ni usiku saana, Giza ni Totoro na wingu zito limeifunika Nchi.

Kinachotupa waonaji matumaini ni Nuru njema sana itakayon'gaa patakapokucha, maana tangu kuumbwa Kwa Dunia, jua halijawahi goma chomoza na kuliachia Giza kutawala milele.

Ni Kweli ujumbe unaweza onekana hautekelezeki Kwa waliopo,

Lakini amini nakwambia, Nyuzi za aina hii zitafukuliwa Ili zifanyiwe KAZI atakapoinuka Mtawala sahihi.

Amen
Nakubaliana naww, but siamin mtawala au Rais ndie ataweza fumua mfumo uliopo!! But hii inahitaji full revolution toka ndan ya CCM.
 
Napoongelea maridhiano kati ya Wananchi na Serikali naomba nieleweke kuwa, simaanishi aina Ile ya maridhiano kati ya CCM na ACT kule visiwani,

Maridhiano nayoongelea Si yake ya Mh Mbowe na kinana na team yake ambayo yaliendelea zaidi ya mwaka huku tukiendelea kukandamizwa na TOZO na Mfumuko wa bidhaa tukipewa sababu hafifu,

Maridhiano nibayoongelea yalenge yafuatayo;

1. RUSHWA iwe historia

Hatufurahishwi kusikia Majina ya viongozi wastaafu yakionekana kujirudia kijirithisha madaraka.

Hatutaki kusikia madawa hospitalini yakigawiwa Kwa upendeleo.

Mbolea Kwa wakulima ya ruzuku itufikie Kwa wakati bila Kutoa RUSHWA. Nk nk nk

2. Tunataka Sanduku la kura lirudi mahala pake

Tumechoka kusikia idadi ya wapiga kura kituoni ni 200 Kwa mfano, lakini katika matokeo zikihesabiwa tunapata idadi jumla ikiongezea na kufikia 250.

Wananchi tunajiuliza, hizo kura 50 Huwa zinaingizwa na maruhani ndani ya ballot box?

Wananchi pia tunataka wagombea tunaowataka ndio Majina Yao yarudishwe, hatutaki kuletewa wagombea wa mfukoni.

3. Umeme, maji na huduma za JAMII za uhakika

Hatutaki blaa blaa, pesa za kulipa bill ya umeme tunazo lakini umeme hamna,

Pesa ya kulipa bill ya maji IPO lakini maji hayatoki bombani!!

Tukilipia vifurushi vya data mitandaoni hatutaki kusikia hamna mtandao, hayatuhusu.

3. Huduma za AFYA

Maridhiano tuyatakayo ni dawa ziwepo za kutosha mahispitalini, Kumwambia mgonjwa kuwa hakuna madawa Hilo halimuhusu.

4. Miundombinu ya barabara

Maridhiano tuyatakayo ni barabara zijengwe za kutosha zitakazohimili msimu mzima.

Hatutaki kusikia mawasiliano ya barabara yakikatika na kutuzuia kufika tupatakapo.

5. Bima za AFYA

Maridhiano kati ya mama Serikali na mama mjamzito yafanyike Ili ijulikane mtoto atakayezaliwa anastahili matibabu ya bima Bure au la!!

Si sawa watoto wa maskini wazuiwe kupata bima wakati viongozi wakitibiwa Bure nje ya nchi Kwa Kodi za sirikali.

6. KILIMO

Maridhiano yafanyike, Kila Kijiji kikopeshwe tractors za KILIMO kupitia Benki ya KILIMO Ili kuepuka KILIMO Cha jembe la mkono.

7. ELIMU

Maridhiano yafanyike kuhakikisha chakula Bure mashuleni kinarudishwa kama enzi za Mwl Nyerere.

Walimu wapewe overtime wanaposahihisha mitihani au kutunga mitihani nje ya muda wa KAZI.

8. Madini

Maridhiano yafanyike wananchi tupate 50/50 katika mgao wa madini yetu.

Wazawa wakopeshwe na wasaidiwe zana za kisasa za kuchimba madini bila kuharibu mazingira.


9. UTUMISHI wa Umma

Maadili ya viongozi yarudi mahala pake, watumishi wa umma waache kufanya biashara ndani ya Serikali. Hili linahitaji maridhiano.

Ndugu Mwananchi unakaribishwa kuongeza eneo ambalo ungependa maridhiano yafanyike kati yetu na sirikali Ili Nchi ipumue.

Angalizo: Wananchi hatufurahishwi na TABIA ya viongozi Wachache wa Vyama vya siasa kujifungia sirini kujadili issues tusozijua Wala kushirikishwa, maridhiano yanatakiwa yawe ya WAZI peupe, sababu hii ni Nchi yetu sote, Nchi hii si ya CCM, CHADEMA na ACT pekee.

ASALI ni tamu, hivyo ni muhimu wote turambe Kwa haki, Si Wachache Kwa RUSHWA.

Karibu. Amen

Itaendelea......!!
Maridhainao ni chaka la wanasiasa kukaa mezani na wanasiasa hakujawahi kuwa na shida hiyo hata kidogo si unaona mbowe siku hizi abweki tena kama zaman licha ya kuwekwa ndani na saa100 mwenyewe
 
Maridhainao ni chaka la wanasiasa kukaa mezani na wanasiasa hakujawahi kuwa na shida hiyo hata kidogo si unaona mbowe siku hizi abweki tena kama zaman licha ya kuwekwa ndani na saa100 mwenyewe
Wanasiasa wanapigania maslah Yao wenyewe.

Wakulima na makundi mengine tuinuke kupambania maslah yetu kama wafabiashara wa kariakoo walivofanya.
 
Back
Top Bottom