Acha tu wawaponde lakini wanakosea sana. Nimeona kila mtu anawalalamikia..ni kweli inawezekana wana problem, tena kubwa tu..PHSYCOLOGICALLY. Na cha kusikitisha ni kwamba wanaume ndio wamesababisha hii hali. Kuzalishwa na kutelekezwa si jambo rahisi hata kidogo, wengine walikuwa masomoni wameshindwa kuendelea wanaona kabisa dunia imewageuka, uwezo wa kumlea mtoto peke yake hawezi.
Mtasema kuwa kayataka mwenyewe angebana migui yake. Hilo ni suala la kipuuzi, kwanini wewe mwanaume usijitulize ukafunga zipu yako usimuingilie dada wa watu kama unajua majukumu huyawezi au huna mpango na binti wa watu.
wanaume mnatumia uanaume wenu vibaya kukandamiza mabinti ili mpate mtakacho hlf baadae unasepa. Wapo wanaume wachache wanaojitambua wanawajibika kutokana na makosa yao. Hata kama hatamuoa binti basi atahakikisha mtoto wake anapata matunzo ipasavyo.
Uzuri ni kwamba hawa single mothers baada ya kusononeka sana wananyanyuka na kupata nguvu ya kulea watoto wao wenyewe na kuendelea maisha. Big up to them na mungu anawasimamia!
Mwisho wa siku mwanaume akiona dada wa watu amemove on maisha yanasonga, katoto kazuri kana afya...eti ndio lijanaume linakuja. Hovyo kabisa!
Nyie wanaume mmepewa jukumu la kuwa kichwa cha familia lakini hamtumii vyema ukichwa mliopewa. Mwanaume yupo kwenye position sahihi ya kupunguza hawa single mothers waliojaa kila mahali, watoto wa mitaani, na hata hii biashara ya uchangudoa inashamiri kwaajili yenu.
NIMEKUBALI KUWA SINGLE MOTHERS NI SHIDA. WANAHITAJI MSAADA WA KISAIKOLOJIA ZAIDI. Kuwaponda haisaidii na badala yake mnaongeza tatizo liwe kubwa zaidi.