Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 3,621
- 6,511
Ukiangalia ramani ya uwanja mpya unaojengwa wa Arusha utaona viboksi boksi vingi vinavyoashiria majengo ya aina fulani.
Tukumbuke eneo lililochaguliwa kujenga uwanja huu ni nje kabisa ya mji na hakuna makazi yoyote yaliyo karibu na uwanja huo kwa sasa.
Wenzetu wakiamua kupeleka viwanja nje ya mji (angalia viwanja vilivyotumika katika AFCON kule Morocco) wanahakikisha wanamaitain uwazi katika mandhari ya eneo linalozunguka uwanja kwa kutokuwa na ujenzi wowote holela au wa hata majengo marefu.
Ukiangalia mandhari ya nje ya uwanja wa Mkapa haivutii na yanatia aibu kwa sababu kuna vibanda vingi vilivyojengwa holela.
Nawaza, waliotengeneza ramani hii wanataka kutuambia kuwa vibanda vitakavyokuja kuchipuka baadae kuzunguka eneo zima la uwanja ni sehemu ya mandhari wanayokusudia iwepo kuzunguka uwanja ili "kupendezesha" au wameamua kuwa wakweli kwamba watanzania ndiyo asili yetu hiyo na hilo halitaweza kuzuilika? Inafikirisha sana.
Tukumbuke eneo lililochaguliwa kujenga uwanja huu ni nje kabisa ya mji na hakuna makazi yoyote yaliyo karibu na uwanja huo kwa sasa.
Wenzetu wakiamua kupeleka viwanja nje ya mji (angalia viwanja vilivyotumika katika AFCON kule Morocco) wanahakikisha wanamaitain uwazi katika mandhari ya eneo linalozunguka uwanja kwa kutokuwa na ujenzi wowote holela au wa hata majengo marefu.
Ukiangalia mandhari ya nje ya uwanja wa Mkapa haivutii na yanatia aibu kwa sababu kuna vibanda vingi vilivyojengwa holela.
Nawaza, waliotengeneza ramani hii wanataka kutuambia kuwa vibanda vitakavyokuja kuchipuka baadae kuzunguka eneo zima la uwanja ni sehemu ya mandhari wanayokusudia iwepo kuzunguka uwanja ili "kupendezesha" au wameamua kuwa wakweli kwamba watanzania ndiyo asili yetu hiyo na hilo halitaweza kuzuilika? Inafikirisha sana.