Haya maisha bhana!!

Haya maisha bhana!!

Umekariri sana dogo wa veta mwalimu wako veta alikuwa NTA level gani au Na yeye aliishia VETA ? Veta ni kwa watu waliofeli na wenye uwezo mdogo
Hiyo nimeona baada ya kusafiri nchi zilizoendelea ,trade skills jobs zinalipa sana.
Vipi unaweza kuandika proposal Kwa ajili ya NGO yangu
 
Mkuu labda lugha imekuwa ya direct sana ila huo ni ukweli.
Mtu mwenye GPA ya Nne kwa accounting and finance ni mtu ambaye kama hakuwa anakariri darasani sio mtu wa kukosa ajira na ikiwa anaitwa interview kabisa.
Shida ni kama haitwi interview ila kama anaitwa interview tena zenyewe hizo za UTUMISHI inabidi afaulu.

Interview za huko hata wenye GPA za Pass huwa wanapita vizuri tu na wala hawana connection. Sasa GpA ya 4 anafeli wapi.
Sawa mkuu hapo itakuwa nimekuelewa sana afu Mimi labda nilichukulia personal
 
Sio nimeenda shule tu, ninayo hadi Shahada ya Uzamili. Wewe unadhani kwanini waajiri wengi sasa hivi wameacha kuajiri kwa kigezo cha ukubwa wa GPA? Kwa sababu wengi wana GPA kubwa ila kichwani chenga tu.
Mkuu basi we kiboko nipe connection mkuu
 
Ungeniuliza miaka 3 nyuma / ningesoma bandiko lako hili miaka 3 nyuma, lazima ningekubaliana na wewe na hakuna mtu angenibadili msimamo wangu.

Ila nikwambie kitu mkuu, God works in mysterious ways. Usikate tamaa, vitu vinawezekana. Amini katika jitihada, muda na Mungu. Siku yako itafika tu, keep your head up soldier.
 
Jipe moyo as long as una afya njema bado una kila sababu ya kusonga mbele nakuamini ipo siku neema itashuka
Juzi nilienda muhimbili nikakuta kuna dada ziwa lake moja linatoa usaa ana maumivu makali amegundulika ana kansa anatakiwa afanyiwe operesheni lakini hana hiyo pesa ambayo ni kama laki 6!
Hapo alipo anasema anasubiri tu kufa,ana maumivu binafsi sijawahi kuona ndo niliona hapo!
Mshukuru Mungu ndugu yangu hata thread unaweza kuandika na bando unalo!
 
Kazi inakufuata kazini haijarishi ni kazi gani unafanya

Mchongo unakuja mchongoni haijarishi ni mchongo gani unaufanya

Bahati haikufuati nyumbani/kitandani bahati hutokea ukiwa kazini

Mkuu weka vyeti pembeni vaa nguo za kazi sio tai na michomeko

ingia kitaani fyatua tofari,piga undaka,piga mishe za mikokoteni,beba gunia pakia au kushusha box

huko ndiko utakutana na njia ya kutokea kimaisha

kwani huko kunawatu watavutiwa na upeo wa hakiri yako mkuu

NIAMINI

KUNA WATU WANA PESA LAKINI HAWANA HAKIRI YA KUZITUMIA KWANI HAWANA ELIMU

NA HAWAJA PATA WA KUWASHAURI HAO WOOTE UTAWAKUTA karia Koo,mabibo,manzese,mpaka bandarini SIO NYUMBANI

NA UKIWA HUKO USIRUHUSU WAJUE ELIMU YAKO BARI WASHANGAZWE NA UTENDAJI WA UBONGO WAKO
 
Wahenga walisema kua uyaone na kweli nimeyaona natamani hata nisingekuwepo duniani. Nimepiga kitabu kwa bidii diploma G.P.A ya 4 degree 4.0 na sioni muelekeo wowote.

Wakuu kitaa ni kugumu natamani hata niyeyuke nilisoma accounting and finance na sioni ikininufaisha kwa chochote, nawaza kwanini nilizaliwa
Usichague kazi.....wenzio mpaka zege tulibeba.....vibarua mixer.....na vibiashara ambavyo wengine huvidharau....wanzuki..
Fegi....
 
Wahenga walisema kua uyaone na kweli nimeyaona natamani hata nisingekuwepo duniani. Nimepiga kitabu kwa bidii diploma G.P.A ya 4 degree 4.0 na sioni muelekeo wowote.

Wakuu kitaa ni kugumu natamani hata niyeyuke nilisoma accounting and finance na sioni ikininufaisha kwa chochote, nawaza kwanini nilizaliwa
Sasa hivi bila kutoa chochote ajira utasikia kwa wakubwa tu
 
Jipe moyo as long as una afya njema bado una kila sababu ya kusonga mbele nakuamini ipo siku neema itashuka
Juzi nilienda muhimbili nikakuta kuna dada ziwa lake moja linatoa usaa ana maumivu makali amegundulika ana kansa anatakiwa afanyiwe operesheni lakini hana hiyo pesa ambayo ni kama laki 6!
Hapo alipo anasema anasubiri tu kufa,ana maumivu binafsi sijawahi kuona ndo niliona hapo!
Mshukuru Mungu ndugu yangu hata thread unaweza kuandika na bando unalo!
pamoja mkuu
 
Back
Top Bottom