G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 12,428
- 39,616
Sasa ni dhahiri wenye CCM wanajulikana na ule msemo wa "CCM ina wenyewe" sasa tunauelewa kiufasaha.
CCM iliwahi kufanya uchaguzi Arumeru mashariki na kumsimamsha mtoto wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo marehemu Jeremiah Sumari bwana Sioi Sumari. Vivyo hivyo imefanya katika jimbo la Kalenga kwa kumsimamisha mtoto wa aliyekuwa mbunge.
Pale Chalinze tayari Ridhiwani Jakaya Mrisho Kikwete ameshashinda kura za maoni hivyo hatutarajii miujiza kubadili matokeo hayo kutokana na sababu lukuki!
Ninachohoji hapa ni kitendo cha wanaCCM 'wakubwa' kuwaweka katika ulingo mmoja hawa watoto wa vigogo na wagombea wengine wasio na 'chakuwabeba'.Mbaya zaidi ni pale ambapo watoto hawa wa 'vigogo' wanapoonekana dhahiri kukosa vipaji vya utumishi kwa walala hoi na hata uongozi hivyo kuonekana dhahiri kubebwa na watangulizi!
Ni ukweli usiopingika kwamba ukimchukua mtoto wa kigogo ukamuweka katika ulingo mmoja na asiye wa kigogo usitarajie maajabu kutoka kwa wajumbe wa CCM walala hoi ambao ndiyo wapiga kura! Piga mayowe onyesha kila aina ya kipaji cha utumishi ulichonacho lakini hutafua dafu kwa mtoto wa 'kigogo' ambaye hasemi na hana kipaji chochote cha utumishi!
Wapo watakaosema kuwa ni wananchi wameamua. Siyo kweli hata kidogo! Changanueni mtaifahamu nguvu iliyoamua!
Ni wajibu wenu wana Kalenga wana Chalinze na wengine kujifunza kutoka kwa wana Arumeru mashariki chagueni mtu mtakayeweza kupigania naye maisha yenu bega kwa bega! Mkimuita ataitika na kuja mbio kuwasikiliza na kutoa usaidizi kutoka moyoni!
Pumzika kwa amani baba wa taifa la Tanzania!
CCM iliwahi kufanya uchaguzi Arumeru mashariki na kumsimamsha mtoto wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo marehemu Jeremiah Sumari bwana Sioi Sumari. Vivyo hivyo imefanya katika jimbo la Kalenga kwa kumsimamisha mtoto wa aliyekuwa mbunge.
Pale Chalinze tayari Ridhiwani Jakaya Mrisho Kikwete ameshashinda kura za maoni hivyo hatutarajii miujiza kubadili matokeo hayo kutokana na sababu lukuki!
Ninachohoji hapa ni kitendo cha wanaCCM 'wakubwa' kuwaweka katika ulingo mmoja hawa watoto wa vigogo na wagombea wengine wasio na 'chakuwabeba'.Mbaya zaidi ni pale ambapo watoto hawa wa 'vigogo' wanapoonekana dhahiri kukosa vipaji vya utumishi kwa walala hoi na hata uongozi hivyo kuonekana dhahiri kubebwa na watangulizi!
Ni ukweli usiopingika kwamba ukimchukua mtoto wa kigogo ukamuweka katika ulingo mmoja na asiye wa kigogo usitarajie maajabu kutoka kwa wajumbe wa CCM walala hoi ambao ndiyo wapiga kura! Piga mayowe onyesha kila aina ya kipaji cha utumishi ulichonacho lakini hutafua dafu kwa mtoto wa 'kigogo' ambaye hasemi na hana kipaji chochote cha utumishi!
Wapo watakaosema kuwa ni wananchi wameamua. Siyo kweli hata kidogo! Changanueni mtaifahamu nguvu iliyoamua!
Ni wajibu wenu wana Kalenga wana Chalinze na wengine kujifunza kutoka kwa wana Arumeru mashariki chagueni mtu mtakayeweza kupigania naye maisha yenu bega kwa bega! Mkimuita ataitika na kuja mbio kuwasikiliza na kutoa usaidizi kutoka moyoni!
Pumzika kwa amani baba wa taifa la Tanzania!