Hawa ndiyo wenye CCM, wengine endeleeni kupiga domo!

Hawa ndiyo wenye CCM, wengine endeleeni kupiga domo!

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
12,428
Reaction score
39,616
Sasa ni dhahiri wenye CCM wanajulikana na ule msemo wa "CCM ina wenyewe" sasa tunauelewa kiufasaha.

CCM iliwahi kufanya uchaguzi Arumeru mashariki na kumsimamsha mtoto wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo marehemu Jeremiah Sumari bwana Sioi Sumari. Vivyo hivyo imefanya katika jimbo la Kalenga kwa kumsimamisha mtoto wa aliyekuwa mbunge.

Pale Chalinze tayari Ridhiwani Jakaya Mrisho Kikwete ameshashinda kura za maoni hivyo hatutarajii miujiza kubadili matokeo hayo kutokana na sababu lukuki!

Ninachohoji hapa ni kitendo cha wanaCCM 'wakubwa' kuwaweka katika ulingo mmoja hawa watoto wa vigogo na wagombea wengine wasio na 'chakuwabeba'.Mbaya zaidi ni pale ambapo watoto hawa wa 'vigogo' wanapoonekana dhahiri kukosa vipaji vya utumishi kwa walala hoi na hata uongozi hivyo kuonekana dhahiri kubebwa na watangulizi!

Ni ukweli usiopingika kwamba ukimchukua mtoto wa kigogo ukamuweka katika ulingo mmoja na asiye wa kigogo usitarajie maajabu kutoka kwa wajumbe wa CCM walala hoi ambao ndiyo wapiga kura! Piga mayowe onyesha kila aina ya kipaji cha utumishi ulichonacho lakini hutafua dafu kwa mtoto wa 'kigogo' ambaye hasemi na hana kipaji chochote cha utumishi!

Wapo watakaosema kuwa ni wananchi wameamua. Siyo kweli hata kidogo! Changanueni mtaifahamu nguvu iliyoamua!
Ni wajibu wenu wana Kalenga wana Chalinze na wengine kujifunza kutoka kwa wana Arumeru mashariki chagueni mtu mtakayeweza kupigania naye maisha yenu bega kwa bega! Mkimuita ataitika na kuja mbio kuwasikiliza na kutoa usaidizi kutoka moyoni!


Pumzika kwa amani baba wa taifa la Tanzania!
 
We mburula unavyohangaika na hii post tangu jana kwenye matanuru ya fb mpaka huku nilikuambia kuwa wivu hautakusaidia dogo fanya maisha yako acha kudandia kwa watu.
 
Usisahu pia kuwaeleza watu kuwa chadema ni mtei,mbowe na slaa wengine wabeba mikoba tu.
 
Si bora hao ccm kuliko ile saccoss yenu.
 
C .c .yemu ni kichaka cha majitu yaliyo funga mikataba na shetani kwaajili ya kuwanyonya wa tanzania kama kupe!
 
Sioni mantiki ya post yako, kwanza elewa kuwa Ridhiwan naye ni raia wa tz na haki kama ulivyo na haki ww kuhusu nchi yako kwa mujibu wa katiba, pia tambua kuwa hajateuliwa ila kachaguliwa na wananchi na siyo kwamba alikuwa pekee bali walikuwa wagombea wengi na yeye ndyo kaibuka mshindi, so..! sioni haja ya kulaumu.
 
Sasa ni dhahiri wenye CCM wanajulikana na ule msemo wa "CCM ina wenyewe" sasa tunauelewa kiufasaha.

CCM iliwahi kufanya uchaguzi Arumeru mashariki na kumsimamsha mtoto wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo marehemu Jeremiah Sumari bwana Sioi Sumari. Vivyo hivyo imefanya katika jimbo la Kalenga kwa kumsimamisha mtoto wa aliyekuwa mbunge.

Pale Chalinze tayari Ridhiwani Jakaya Mrisho Kikwete ameshashinda kura za maoni hivyo hatutarajii miujiza kubadili matokeo hayo kutokana na sababu lukuki!

Ninachohoji hapa ni kitendo cha wanaCCM 'wakubwa' kuwaweka katika ulingo mmoja hawa watoto wa vigogo na wagombea wengine wasio na 'chakuwabeba'.Mbaya zaidi ni pale ambapo watoto hawa wa 'vigogo' wanapoonekana dhahiri kukosa vipaji vya utumishi kwa walala hoi na hata uongozi hivyo kuonekana dhahiri kubebwa na watangulizi!

Ni ukweli usiopingika kwamba ukimchukua mtoto wa kigogo ukamuweka katika ulingo mmoja na asiye wa kigogo usitarajie maajabu kutoka kwa wajumbe wa CCM walala hoi ambao ndiyo wapiga kura! Piga mayowe onyesha kila aina ya kipaji cha utumishi ulichonacho lakini hutafua dafu kwa mtoto wa 'kigogo' ambaye hasemi na hana kipaji chochote cha utumishi!

Wapo watakaosema kuwa ni wananchi wameamua. Siyo kweli hata kidogo! Changanueni mtaifahamu nguvu iliyoamua!
Ni wajibu wenu wana Kalenga wana Chalinze na wengine kujifunza kutoka kwa wana Arumeru mashariki chagueni mtu mtakayeweza kupigania naye maisha yenu bega kwa bega! Mkimuita ataitika na kuja mbio kuwasikiliza na kutoa usaidizi kutoka moyoni!


Pumzika kwa amani baba wa taifa la Tanzania!

Mkuu ulichosema sasa CCM hawana nguvu ya kuishambulia Chadema kwa kutunga . Viti maalum wa Chadema waliingia kwa merits za Chama lakini wakafanya kuwa personal . Now they are in for it hawana la kusema bali kukimbilia kusema Saccoss nk . Chadema will never be and is not saccoss maana inawanyima usingizi .Names calling ni ufinfu kama ni saccos mbona CCM wanatumia nguvu sana kukabiliana na Chadema ? Kujifariji kwingine bi upuuzi .
 
We mburula unavyohangaika na hii post tangu jana kwenye matanuru ya fb mpaka huku nilikuambia kuwa wivu hautakusaidia dogo fanya maisha yako acha kudandia kwa watu.

ungekua na akili ungekwenda kuwaelimisha ndugu zako kule dutwa, ngeme, itilima, ng'esha ngeme nk, waache kunya mtoni manake Wanachafua ule mto unafanana na ID yako
 
Ninavyojua mimi. Uongozi ni karama na haufundishwi... Sasa kama mtu ana karama hiyo kwann asitumie fursa kama ipo? Pia katiba yetu inaruhusu mtz yeyote kugombea. Haiangalii baba ake ashawah kuwa kiongozi au n kiongoz wa serkal hivyo watu hawa wanaruhusiwa na pia hawajajipitisha wao au baba zao hawajawapitisha. Wajumbe ndio waliowapitisha. Cdm kumbukeni hii singo haijauzika kabisa huku kalenga. Naona mnaipeleka chalinze wananchi wanasikiliza sera. Acheni kuwattack wagombea kama mnavyofanya kwa G Mgimwa mtaangukia pua. Washawishin watu wawape kura na sio kulalama et huyu baba ake n rais mara baba ake aliwah kuw mbunge..... Kila mtz ana haki ya kuchagua na kuchaguliwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom