The Garang
JF-Expert Member
- Jan 16, 2018
- 2,333
- 4,153
vipi swala la luku mkuu haiishi au yanajiwekea
vipi swala la luku mkuu haiishi au yanajiwekea
Sio kwa kina BIG kweli? 😂Mpwa....
Niliwahi kupanga Chumba maeneo fulani ya magomeni....ile nyumba ilikuwa na vyumba saba lakini wapangaji tuliokuwa tunajuana ni mimi na jamaa mmoja.....nilikaa pale miezi miwili pasi nakuonana na wapangaji wengine zaidi ya jamaa ninayekutana naye akiwa anatoka na kurudi kazini.....lakini kipindi chote shughuli zote za kuashiria kuwa vile vyumba wanaishi watu zilikuwa zinaendelea kama vile kupika na mazungumzo yaliyojaa vicheko vya hapa na pale.......lakini ukikaa koridoni huoni mtu......kilichonifanya nikimbie ile nyumba ilikuwa siku ya jumapili...nilichelewa kuamka....muda nilio amka nikachukua ndoo yangu kwenda bafuni kujimwagia....nikakuta bafuni kuna mtu anaoga kutokana na viashiria vya kumwagika kwa maji humo bafuni.....nikasema ngoja nisubirie tu hapa hapa kuliko kujisumbua kurudi chumbani kwangu......nilikaa karibu na mlango kabisa.....baada ya muda kadhaa kimya kikatawala mule bafuni kuashiria kwamba mtu ameshatoka sasa lakini atakuwa amepitia wapi......wakati naangaza macho kwenye korido nikaona kuna kandambili zimeloa kwenye moja ya ile milango ambayo sijawahi kuwaona watu wakiingia humo.....akili yangu ikaniambiaa kuwa kuna kitu hakipo sawa.....nikaingia bafuni nikaoga.....nikarudi chumbani kwangu nikavaa nikatoka......nilipokuwa mitaani nikamtafuta mtu mzima kidogo ambaye ni mwenyeji na kumdadisi kuhusu nyumba ile.....akaniambia ile nyumba ni nzito.....na inakaliwa na watu wazito......huo ndio ukawa mwisho wa mimi kukaa mule ndani na hata vyombo niliagiza watu wanileteee......
Maili mbili hasa kwa mudi ndo mambo yao hayoHayo mambo yaskie tu,
Niliishi nyumba moja maeneo ya airport dodoma,sitosahau tuliyokua tunashuhudia,
Kubwa zaid tukahamia nyumba iliyokua haiishi mtu kwa kitambo kirefu maili mbili ikawa changamoto mno, mauza uza kila kukicha
yule jran wa gobaSio kwa kina BIG kweli?
Tena huwa yanakodi bodaboda kumkimbiza yanaetaka kumdhuru...Kumbe majin ya bongo kwenye giza hayaoni
Hivi bado ana mabasi?sasa hiyo imeshashindikana, maana kuna wazungu walipanga humo, japo waliambiwa wao wakawa wabishi,
Unaambiwa walicharazwa bakora, na kulazimishwa waongee kiswahili
Siku ya pili mbna walihama wenyewe, chezea ndondocha weyeeeh.
Yaan hapa mbavu sina wallah, huyo OTTAWA kakimbila makambako sahivi ndo anakofanya shughuri zake, mweeeeh
Nani anaweka luku
Na Mimi nahitaji pia namba ya huyo mtumishi Kwa ajili ya maombeziNaomba mawasiliano ya huyo mtumishi wa Mungu nahitaji maombi mkuu
Hii ishawahi nitokea nilipanga nyumba buguruni kumbe mwenye nyumba na dalali ndo michezo yao ikifika usiku full kuwashwa mara panya walie hovyo,mara umwagiwe maji.Sijui why leo nipo kwenye mood ya kuongelea hii Topic , I hope itagusa watu na kuwasaidia kuchukua hatua. Mara nyingi tumekua tukiangalia Film’s za kutisha huko Hollywood kuhusu hizi haunted houses na mikasa ya kutisha kuhusu hizo nyumba zilizotawaliwa na ma roho /majini/ mapepo machafu. Na wengi wetu tumekua tukifikiria tu kuwa hizo ni hadithi na kamwe matukio kama hayo hayapo kwenye ulimwengu wetu.
Watu wengi wamejikuta wakipata mikosi kwenye maisha yao, nuksi kwa kuhamia , kupanga or kununua nyumba zilizofanyiwa mazindiko ya kishetani pasipo wao wenyewe kujua.
Unakuta mtu unapanga nyumba, ghafla mambo yako yanaanza kwenda hovyo, matatizo kazini, ndoa hakuna mawasiliano mazuri, mara ukiamka asubuhi unakuta umenyolewa nywele, mara unakua mvivu mvivu tu , biashara haiendi Sawa yani kila kitu kwako kinakua hovyo mwanzo mwisho , pesa zinakukimbia, marafiki hamna
Tuwe Makini sana na nyumba tunazohamia, Ni vizuri mtu kufanya spiritual cleansing before kuhamia kwenye nyumba za kupanga kila mtu kulingana na imani yake kama muislam, mkristo au mshirikina, kwa sababu hatujui hizo nyumba zimefanyiwa manuizi au matambiko na sisi bila kujua tunahamia tu , kwa vile nyumba iko masaki , mbezi beach tunaamini huko hakuna mambo ya kishirikina wakati wamiliki wengi wa hayo maeneo wanafuga majini kwa ajili ya kulinda mali zao , unajikuta mtu huna hili wala lile unahamia kwenye apartments hapo ndo unakua mwanzo wa mabalaa na nuksi katika maisha yako .
Hao watu wazito ni wachawi mfano wake hakuna usijidanganyeTafuta pesa sheikh hakuna Cha mchawi Wala nini?hv umeishawahi kujiuliza kwanini mauza uza na zile Swaga za Yule mzee manyau huwa hazitokei Wala haIfanywi mikocheni,masaki,oyster bay,upanga?
Swaga na story za kichawi utazisikia Kawe,manzese,Tandale,buguruni,
Ni muda kama uko tayari nitafuteAcha tu ndugu yangu. Yamenikuta. Sijui kama ni stage tu ya maisha nakumbana nayo au kuna mtu anajaribu kunikwamisha. Ila kama ni mtu ananikwamisha siku nitakuja kumgundua ataisoma namba!! Na naomba kama kuna mtaalamu yeyote anaeweza kunisaidia nipo tayari kutoa ushirikiano ila asiwe tapeli
Miaka kama mitatu hivi nilibahatika kupata kazi sehemu flani, kazi ilikuwa na maslahi kweli kweli na ukizingatia mimi nilikuwa bahili kweli kweli. Hela yangu ilikuwa hailiwi kizembe.
Nikawa pia nafanya kilimo, kilimo nacho kikawa kinanilipa kweli kweli. Hela ikanitembelea kweli kweli. Kila nikichungulia kwenye akaunti ikawa inanona vilivyo. Kabla nikiwa naenda likizo akaunti yangu ilikuwa inasoma 57M.
Kufika home kijiji cha kwanza nikamwambia mzee anionyeshe sehemu ya kujenga. Nikaanza chapu maana nilikuwa na likizo ya mwezi m1 tu.
Of course mimi napenda vitu quality. Nikaanza ujenzi wa nyumba ya ndoto zangu ambayo itakuwa ni ya familia yangu pia. Ni nyumba kubwa tu.
Likizo ilivyoisha tu nikarudi zangu mzigoni nyuma nikaacha ujenzi ukiendelea. Nikapaua, nikaweka dirisha na milango ya chuma, nikapiga plasta, wiring na plumbing. Ikawa gumzo pale kijiji. Bwana bwana bwana weee, ghafla mambo yakawa yamebadilika kwa speed ya 5G
Mara vuuup, nikafukuzwa kazi. Lakini akaunti yangu ikawa iko vizuri tu. Nikasema isiwe tabu. Nikasema suburi nifanye biashara pamoja na kuendelea na kilimo kama kawa. Cha kushangaza kila nikitia hela huko inafia huko hairudishi hata mtaji. Nikatia mzigo kwa mara nyingine safari hii nilipigwa hasara mpaka nikikumbuka natetemeka.
Ikawa najikingoja tu hivyo hivyo. Miezi 7 haikuisha 22M sijui zikivyokauka kauka na sasa nipo sina hata mia.
Bado sijakata tamaa, nipo napambana kutafuta chaka lingine maana kama elimu na mavyeti ninayo ya kutosha ila hili nuksi lililonijia sitakaa nilisahau kamwe.
Kimsingi roho hata hainiumi kwa vile kila nikiangalia mjengo wangu natabasamu najisemea kimoyomoyo "Asante Mungu" japokuwa haijaisha ila kwa umri wangu wa 30's nina imani nitapambana nikamilishe nyumba ya ndoto zangu kijijini kwanza ila sijui ni kwa namna gani maana kila nachofanya hakiendi.
Napitia wakati mgumu sana ndugu zangu. Niombeeni. Au nasema uongo ndugu zangu???
KAMA KUNA MTU YUKO NYUMA YA HILI NASEMA AJIANDAE, TENA NASEMA AJIANDAE KWELI KWELI. ONCE NITAKAPOMJUA, hiiiiiiiiiiiiiiii!!!!!!
Mtaani hapa kuna nyumba ilishashindikana kukalika, sasahivi naona majini ndio yanajitawala maana ikifika jioni yanawasha taa asubuhi yanazima.
Chuma cha chumaKuna jamaa alinunua nyumba kule kwa wagosi Tanga ,lakini nyumba ile iliuzwa na bank baada ya mgosi kushindwa kulipa bank .
Bwana bwana yule mgosi kumbe aliacha jini mle ndani acha bwana mnunuzi apigwe MBUPU kila siku machine machine anawekwa style kama za Giggy money akaona aaaaaaaah bhaghosha ntapoteza ubingwa kabisa akatimua .