Hatuna umeme siku tano

Hatuna umeme siku tano

Kisendi

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2009
Posts
699
Reaction score
180
Huku Majohe, Ukonga, Kipunguni, Chanika, Gongo la mboto, Pugu, Kisarawe na maeneo yote ya Gongo la Mboto hatuna umeme leo siku ya tano. Hatukumbuki kabisa, imebidi nihame kwa muda maana kazi zangu zinategemea umeme. Swali la kujiuliza huku hatuna maji ya dawasco tunavuta chini kutumia mashine.

Wanadai transforma imeungua sasa swali la kujiuliza wanashindwa hata kutugawia kwa line nyingine tukagawana na wengine ili tusukume maji. Hili taifa letu tusipobadilika sisi wenyewe umasikini utaendelea kututafuna haiwezekani siku tano bila umeme. Waziri Simbachawene waamshe hao tanesco. Tumechoka...
 
Ni kweli kabisa, tumechoka kukaa bila umee. Kila kitu kina umuhimu kwa maisha ya binadamu. Me pia nimehama na hivi nipo likizo imenipelekea nibadili mazingira
 
Ungepitia pitia habari muhimu za wiki iliyopita ungeelewa kuwa mitambo mipya kabisa ya kufua umeme kwa kutumia gas iliyopo Kinyerezi imekwisha simikwa na sasa inafanyiwa majaribio.

Na mitambo ya zamani inayotumia mafuta mazito nayo inabadilishwa ili itumie gas yetu, kwa hiyo tutegemee umeme kukatika hapa na pale kwa takriban miezi miwili.

Kikwete anatuwachia umeme wa miaka 20 ijayo.
 
Kuweni wavumilivu umeme mtapata tena wa kumwaga.

Kule kwetu hatujawahi kuupata tangu kabla ya ukoloni lkn tuna subira kwani serikali yetu imeliona hilo na juhudi zinafanyika kutupatia umeme
 
Vumilieni
Hata kama wanabadilisha mitambo nyinyi kama wateja hilo haliwahusu.....walitakiwa kuwa na mbadala nyie msiathirike wakati zoezi linaendelea....

Ila kwa kuwa tunaenda kwa matukio na hakuna anayejali watakata tu
 
Ungepitia pitia habari muhimu za wiki iliyopita ungeelewa kuwa mitambo mipya kabisa ya kufua umeme kwa kutumia gas iliyopo Kinyerezi imekwisha simikwa na sasa inafanyiwa majaribio.

Na mitambo ya zamani inayotumia mafuta mazito nayo inabadilishwa ili itumie gas yetu, kwa hiyo tutegemee umeme kukatika hapa na pale kwa takriban miezi miwili.

Kikwete anatuwachia umeme wa miaka 20 ijayo.

Wewe unaongea kama nani?ww ni msemaji wa serikali,Tanesco au?
 
Ungepitia pitia habari muhimu za wiki iliyopita ungeelewa kuwa mitambo mipya kabisa ya kufua umeme kwa kutumia gas iliyopo Kinyerezi imekwisha simikwa na sasa inafanyiwa majaribio.

Na mitambo ya zamani inayotumia mafuta mazito nayo inabadilishwa ili itumie gas yetu, kwa hiyo tutegemee umeme kukatika hapa na pale kwa takriban miezi miwili.

Kikwete anatuwachia umeme wa miaka 20 ijayo.

Kweli Ww Ni Zaid Ya BabaRIZ, DUH!
 
Ungepitia pitia habari muhimu za wiki iliyopita ungeelewa kuwa mitambo mipya kabisa ya kufua umeme kwa kutumia gas iliyopo Kinyerezi imekwisha simikwa na sasa inafanyiwa majaribio.

Na mitambo ya zamani inayotumia mafuta mazito nayo inabadilishwa ili itumie gas yetu, kwa hiyo tutegemee umeme kukatika hapa na pale kwa takriban miezi miwili.

Kikwete anatuwachia umeme wa miaka 20 ijayo.

Webibi kweli hamnazo kabisaaa.......
Yaani mleta uzi analeta habari nyingine, alafu wewe unachangia kwa kuleta maudhui tofauti kabisa na kile kilicho kusudiwa.
Agghhhh.... yaani huyo baba riz1 una mahaba nae ya hatari hata haupati usingizi kwaajili yake aiseee.....
 
Ungepitia pitia habari muhimu za wiki iliyopita ungeelewa kuwa mitambo mipya kabisa ya kufua umeme kwa kutumia gas iliyopo Kinyerezi imekwisha simikwa na sasa inafanyiwa majaribio.

Na mitambo ya zamani inayotumia mafuta mazito nayo inabadilishwa ili itumie gas yetu, kwa hiyo tutegemee umeme kukatika hapa na pale kwa takriban miezi miwili.

Kikwete anatuwachia umeme wa miaka 20 ijayo.

Hizi hadithi niliwahikusimuliwa miaka miwili nyuma kwamba mgao waumeme Tanzania utakua historia
 
Huku Majohe, Ukonga, Kipunguni, Chanika, Gongo la mboto, Pugu, Kisarawe na maeneo yote ya Gongo la Mboto hatuna umeme leo siku ya tano. Hatukumbuki kabisa, imebidi nihame kwa muda maana kazi zangu zinategemea umeme. Swali la kujiuliza huku hatuna maji ya dawasco tunavuta chini kutumia mashine.

Wanadai transforma imeungua sasa swali la kujiuliza wanashindwa hata kutugawia kwa line nyingine tukagawana na wengine ili tusukume maji. Hili taifa letu tusipobadilika sisi wenyewe umasikini utaendelea kututafuna haiwezekani siku tano bila umeme. Waziri Simbachawene waamshe hao tanesco. Tumechoka...

Mkuuu poleni sana nasikia kipande hicho UKAWA ni wengi mno,Ni mpango Wa azabu ili muichague CCM
 
As well kuna Amani na Utulivu mnatakiwa kuchagua Ccm, Mkome kupenda Chama kisichowapenda. Jana Pia si mlijazana kwny Kura za Maoni mkamchagua Mteule wa Mamlaka ya Juu
 
Back
Top Bottom