Hatimaye Waraka umemtoa pangoni “mwenyewe”!

Hatimaye Waraka umemtoa pangoni “mwenyewe”!

Mnufaika namba moja kama sio namba mbili kashindwa kujizuia katoka pangoni kubweka.
Chezea waraka wa Modekai na Ester dhidi ya njama za Hamani.
 
TEC ni Baraza langu naliheshimu sana lakini naona limejaa unafiki mkubwa na uzandiki.


Sasa Tusubirie waraka wa BAKWATA na Kisha taasisi zingine za kidini!!!!

TEC acheni unafiki, acheni kuivuruga nchi, acheni kujiingiza kwenye siasa mnailigawa taifa letu.
Kumbukeni nchi ikichafuka hakuna atakaye pona.
Kujichanganya huwepo kutokana na hoja inasemaje. kuna hoja za kidini na kisiasa. Ukizichanganya hizi ndio tatizo.
 
Naona mods wanajitahidi kufuta threads zinazohusu maoni ya udini na siasa. But mwisho wa siku ukweli ni kwamba dini na siasa HAVITENGANI!
Wanasiasa ndio hao hao wanadini ama sivyo wakati wa uchaguzi wanasiasa wachaguliwe na wanasiasa wenzao na wanadini wabaki na imani zao!
Nchi ni yetu sote!
Kweli uwezi tenganisha dini na siasa,kuna watu kama bishop Desmond Tutu nI nfano mzuri alijijengea heshima ndani na nje ya Afrika kusini.
 
It is very simple! Issue ni mkataba mbovu sasa udini unatoka wapi. natamani Public figures wangelijitokeza wakamjibu. Ukiona hata Zito amenyamaza as if hakuna kinachoendele, ujue hawa dini inawafanya wajinga!
Hapo ulipomtaja Zitto nimekuelewa kabisa! Hawa jamaa sio wa kuwaamini kabisa! Hata wasome kivipi upumbavu hautoki kichwani mwao! Huyo mwarabu muislamu mwenzio kwanza yeye hataki kujiita mweusi! Ni racist! Anawaona waafrika kama manyani! Akina Zitto na Kikwete wanashangilia kumpa bandari muarabu ili hali muarabu anawanyanyapaa! Wanadhani kwa kumpa mwarabu bandari ndo wanaenda peponi! Hawa jamaa wapumbavu kabisa! Ni shida
 
Naam!

Sinema bado inaendelea kwa kasi huku vioja vikiendelea kujitokeza. Leo kuna matukio mawili makubwa yaliyotokea.

Waraka wa Baraza la Maaskofu (Roman Catholic) kupinga mkataba wa ubinafsishaji wa bandari za Tanganyika, ambao umesomwa nchi nzima katika kila kanisa na vigango vyake kote nchini. Jambo hili limewachanganya sana!

Na hivyo kupelekea kuibuka kwa tukio la pili...

Tukio la pili ni lile la kuibuka Rais Mstaafu Awamu ya Nne kutokea huko Rorya-Mara. Yeye anaujibu waraka huo kwa kuigeuza hoja na kuwa "Udini," akiamini yeye kwamba hatuelewi kinachoendelea.

Kiujumla, hawa wakuu wanazidi kujiumbua wao wenyewe, wameona wajaribu kutumia majukwaa ya kidini ili ku-push DP-WORLD.

Kesho tunasubiri tumsikie huyo Kinara wa nchi kwenye Jubilei nyingine ya kanisa lingine kutimiza miaka 60 huko Arusha. Hii ni kwa sababu Mkuu wa Sterling anajua kabisa nguvu ya TEC.

TEC inao uwezo wa kuongea na dunia na ikaeleweka.
View attachment 2723168View attachment 2723169
Hakikaa!!!Haukuna siri chin ya jua... 🤣
 
Kwenye Waraka vimetajwa Bunge, Mahakama na serikali. Bunge linaongozwa na Mkatoliki Baraza TEC imelishukia Bunge kwamba limewatelekeza Wananchi, huo udini unaozungumzwa ni upi?
 
Mnakosea jamani mbona mnakuwa na akili ndogo kiasi hicho. Alichomaanisha Dkt Kikwete ni kuwa madhabahuni siyo sehemu ya kuhubiria siasa na hili limejitokeza madhehebu yote siyo wakristo tu bali hata waislamu. Dkt Kikwete ni baba yetu tuwe na staha na heshima jamani. Atakeyebisha nitamlamba dislike [emoji107]

Kwanza jiulize JK aliyoongea alipaswa aongee Rais wa Tanzania kwa sasa,ukichunguza kwa umakini aliyoongea JK utagundua yeye ndo anaongoza nchi kwa sasa
 
Tarehe 25 December 2017, Askofu Zakaria Kakobe akiwa kanisani kwenye ibada ya Christmas, katika kanisa la FGBF Mwenge jijini Dar es Salaam, alinukuliwa akituma salamu kwa Rais wa JMT, Dkt. John P. Magufuli.

"Rais John Pombe Magufuli, nawe unatakiwa kutubu leo. Unaposherekea sikukuu ya Christmas, ili uridhiwe na Mungu unatakiwa nawe utubu".

"Leo ni siku ya watawala wa Tanzania kutubu. Leo tumeanza kuona misingi ya amani ya nchi yetu ikitikiswa. Amani iliyojengwa kwa gharama kubwa na waasisi wetu. Tumeanza kuona nchi hii ni ya chama kimoja na huu ni uovu. Mungu mwenyewe anaheshimu sheria basi kama na sisi tumeweka sheria tunapaswa kuheshimu sheria tulizojiwekea wenyewe. Hii si nchi ya chama kimoja. Kama mnataka kubadilisha si mbadilishe tu mara moja kupitia wabunge wenu wa CCM, si mko wengi?".

"Sheria ni lazima zizingatiwe! Na kwa hili nitapiga kelele mpaka Mlima Kilimanjaro. Huwezi kusema wewe huwezi kusemwa, wewe ni nani? Mungu anasemwa vibaya sembuse wewe?".

"Mungu mwenye nguvu kuliko Magufuli, ana nguvu kuliko majeshi yote ya nchi, lakini anatukanwa na bado hatumii majeshi yake. Hata wewe unaweza ukawa mvumilivu"

Baada ya kauli hii, Askofu Kakobe alipokonywa passport yake, alihojiwa uraia wake na aliandamwa na TRA kwa madai ya kodi.

Huyu alikuwa ni kiongozi wa dini ya Kikistro na alimkosoa Mkristo Magufuri

Huu ulikuwa udini? Wa dini gani?

Askofu wa Catholic Jimbo la Rulenge (Severine Niwemugizi) alimkosoa mkatoliki mwenzake Magufuri juu ya haki ya vyama vya siasa kufanya mikutano.

Aliishia kupokonywa passport na kuhojiwa uraia wake.

Alikuwa mdini? Akishabikia dini gani?

Nachukizwa sana na yeyote ambaye atataka kutugawa kwa misingi ya kidini.

Kukosoa haiwezi hata mara moja kuwa udini.

Kuwa kiongozi wa dini hakumnyimi haki kiongozi huyo kupata haki zake za kikatiba kutoa maoni juu ya mambo ya nchi yake kama anavyoweza kufanya Mwalimu, daktari, mkulima au mfugaji.

Tukemee wale wote wanaotaka kujificha kwenye udini pale tu wanapokosolewa kwa makosa waliyoyafanya wenyewe.

Mungu Ibariki Tanzania na watu wote.

Uhuru, Umoja na Amani
 
Naam!

Sinema bado inaendelea kwa kasi huku vioja vikiendelea kujitokeza. Leo kuna matukio mawili makubwa yaliyotokea.

Waraka wa Baraza la Maaskofu (Roman Catholic) kupinga mkataba wa ubinafsishaji wa bandari za Tanganyika, ambao umesomwa nchi nzima katika kila kanisa na vigango vyake kote nchini. Jambo hili limewachanganya sana!

Na hivyo kupelekea kuibuka kwa tukio la pili...

Tukio la pili ni lile la kuibuka Rais Mstaafu Awamu ya Nne kutokea huko Rorya-Mara. Yeye anaujibu waraka huo kwa kuigeuza hoja na kuwa "Udini," akiamini yeye kwamba hatuelewi kinachoendelea.

Kiujumla, hawa wakuu wanazidi kujiumbua wao wenyewe, wameona wajaribu kutumia majukwaa ya kidini ili ku-push DP-WORLD.

Kesho tunasubiri tumsikie huyo Kinara wa nchi kwenye Jubilei nyingine ya kanisa lingine kutimiza miaka 60 huko Arusha. Hii ni kwa sababu Mkuu wa Sterling anajua kabisa nguvu ya TEC.

TEC inao uwezo wa kuongea na dunia na ikaeleweka.
View attachment 2723168View attachment 2723169
Muasisi mkuu wa ufisadi na udini tanzania. Kila akiguswa anakimbiliaga kwa wenzake na kubwata oh Udini. Tunakumbuka wewe Jakaya ulihudhuria conference ya kusilimisha Africa Abuja. Ulivyo ndumilakuwili ukamshawishi komando wa zenj akajiunge OIC ukapigwa na kitu kizito kichwani. Tunakufahamu sana.
Watanzania wote tunaelewa kuwa kazi ya dini zote ni kuhubiri haki na usawa na kupambana na dhulma zote. Kazi ya serikali ni kusimamia haki itendeke. Ukiona wanakinzana jua mmoja anatafuta kukandamiza jamii.
DIni zinazokinzana na dhana ya kupambana na dhulma ni Dini za mashetani tu!
 
Kwenye Waraka vimetajwa Bunge, Mahakama na serikali. Bunge linaongozwa na Mkatoliki Baraza TEC imelishukia Bunge kwamba limewatelekeza Wananchi, huo udini unaozungumzwa ni upi?
Tena na huyo kiongozi wa bunge naye amesomewa waraka kanisani na picha hiyo hapo!
20230820_230958.jpg
 
Naam!

Sinema bado inaendelea kwa kasi huku vioja vikiendelea kujitokeza. Leo kuna matukio mawili makubwa yaliyotokea.

Waraka wa Baraza la Maaskofu (Roman Catholic) kupinga mkataba wa ubinafsishaji wa bandari za Tanganyika, ambao umesomwa nchi nzima katika kila kanisa na vigango vyake kote nchini. Jambo hili limewachanganya sana!

Na hivyo kupelekea kuibuka kwa tukio la pili...

Tukio la pili ni lile la kuibuka Rais Mstaafu Awamu ya Nne kutokea huko Rorya-Mara. Yeye anaujibu waraka huo kwa kuigeuza hoja na kuwa "Udini," akiamini yeye kwamba hatuelewi kinachoendelea.

Kiujumla, hawa wakuu wanazidi kujiumbua wao wenyewe, wameona wajaribu kutumia majukwaa ya kidini ili ku-push DP-WORLD.

Kesho tunasubiri tumsikie huyo Kinara wa nchi kwenye Jubilei nyingine ya kanisa lingine kutimiza miaka 60 huko Arusha. Hii ni kwa sababu Mkuu wa Sterling anajua kabisa nguvu ya TEC.

TEC inao uwezo wa kuongea na dunia na ikaeleweka.
View attachment 2723168View attachment 2723169
Waraka gani unasomwa kwenye makanisa tu baada ya misa ? huu ni udini , wala hauna kupepesa macho
 
Back
Top Bottom