Naam!
Sinema bado inaendelea kwa kasi huku vioja vikiendelea kujitokeza.leo kuna matukio mawili makubwa yaliyotokea.
Waraka wa baraza la maaskofu(Roman catholic)kupinga mkataba wa ubinafsishaji wa bandari za Tanganyika.
Ambao umesomwa nchi nzima katika kila kanisa na vigango vyake kote nchini.
Jambo hili limewachanganya sana!
Na hivyo kupelekea kuibuka kwa tukio la pili....
.....Tukio la pili ni lile la kuibuka Rais mstaafu awamu awamu ya nne kutokea huko Rorya-Mara.
Yeye anaujibu waraka huo kwa kuigeuza hoja na kuwa "Udini" akiamini yeye kwamba hatuelewi kinachoendelea.
Kiujumla hawa wakuu wanazidi kujiumbua wao wenyewe,wameona wajaribu kutumia platforms za kidini ili ku-push DP-WORLD.
Kesho tunasubiri tumsikie huyo Kinara wa nchi kwenye Jubilei nyingine ya kanisa lingine kutimiza miaka 60 huko Arusha.
Hii ni kwa sababu mkuu wa sterling anajua kabisa nguvu ya TEC.
TEC inao uwezo wa kuongea na Dunia na ikaeleweka.
View attachment 2723168View attachment 2723169