Hatimae Pedeshee Ndama akiri kutakatisha fedha

Hatimae Pedeshee Ndama akiri kutakatisha fedha

Mfanyabiashara, Ndama Shabani Hussein (Pichani katikati) maarufu kama Ndama mtoto ya Ng'ombe amekiri mahakamani kosa la kutakatisha zaidi ya billioni 1.2.

Ndama anadaiwa kuwa Februari 20, 2014 jijini Dar es Salaam, alighushi nyaraka ya kibali cha kusafirisha madini na sampuli za madini kwa kusudi la kuonesha kuwa kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Company Limited iliruhusiwa kusafirisha maboxi manne ya dhahabu yenye kilogramu 207 yenye thamani ya Dola za Marekani 8,280,000.00 kwenda Australia kwa kampuni ya Trade TJL DTYL Limited wakati akijua si kweli.

Chanzo: Nipashe


Dah namuona mwananguu mbetwa robert pembeni hapo... daaah jamaaa kapakaza sana gundi mademu zetu pale IFM kwa hizi hela walizopiga TTCL
 
Naombeni mnisaidie maana ya hili neno "kutakatisha fedha"
Kutakatisha fedha ni tafsiri ya kienyeji toka katika msemo wa kiingereza "Money laundering". Nitakupa mfano ili kukupa maana yake.
Mfano: John anauza madawa ya kulevya kisha anachukua zile pesa ananunua kahawa kisha akiiuza anachukua pesa anapeleka bank hapo anaonekana kama kafanya biashara halali, ile fedha inaoneka chanzo chake ni halali kumbe chanzo ni haramu. Mfano mwingine unachukua pesa labda ya serikali unaenda kuweka bank ktk fixed account kwa muda wa miezi 6 kisha unaichukua riba iliyopatikana wewe binafsi, ile pesa ya serikali unapeleke ktk matumizi yaliyokusudiwa. Kwa kifupi ni kitendo cha kufanya biashara haramu na kuingiza ile pesa ktk mzunguko halali kwa lengo la kujipatia pesa halali.
 
  • Thanks
Reactions: SDG
No wonder kuna binti mmoja hakimu alikuwa hana akili alipokiwa primary mpaka secondary lakini alipokija kiwa hakimu alipata utajiri mpaka akaenda kuoa sharo moja hivi akalitafitia na kazi kwenye mifuko ya pensheni ana ukwasi wa hatari.

Vijana someeni uhakimi unalipa sana bongo
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Mfanyabiashara, Ndama Shabani Hussein (Pichani katikati) maarufu kama Ndama mtoto ya Ng'ombe amekiri mahakamani kosa la kutakatisha zaidi ya billioni 1.2.

Ndama anadaiwa kuwa Februari 20, 2014 jijini Dar es Salaam, alighushi nyaraka ya kibali cha kusafirisha madini na sampuli za madini kwa kusudi la kuonesha kuwa kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Company Limited iliruhusiwa kusafirisha maboxi manne ya dhahabu yenye kilogramu 207 yenye thamani ya Dola za Marekani 8,280,000.00 kwenda Australia kwa kampuni ya Trade TJL DTYL Limited wakati akijua si kweli.

Chanzo: Nipashe


Shikamoo Mtakatif* Pessa !!
Eleri Waru'ka paa !!
 
Mi naona hii case ni ya kugushi vibali,
labda kama dhahabu aliiba au aliipata kwa utapeli ama kainunua kwa pesa za madawa ya kulevya.

Lakini kama dhahabu kainunua kwa pesa halali akataka kuisafirisha akagushi vibali labda ili kuepuka kodi,
sijana laundry hapa au labda money laundry ina maana pana kuliko nayoijua
 
Ndamaaa muda ndio huo tena umekutupa hakusoma majira mapema nenda jela kwenye historia ya maalwatan nawe umo
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Mi naona hii case ni ya kugushi vibali,
labda kama dhahabu aliiba au aliipata kwa utapeli ama kainunua kwa pesa za madawa ya kulevya.

Lakini kama dhahabu kainunua kwa pesa halali akataka kuisafirisha akagushi vibali labda ili kuepuka kodi,
sijana laundry hapa au labda money laundry ina maana pana kuliko nayoijua
Sidhani kama aliuza hiyo dhahabu....alifoji documents tu
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Kuna kipindi hii industry ya upigaji ilikuwa na watu wa kila aina huko.....yaani hii industry...balaa lake sio dogo....
 
Back
Top Bottom