HATARI HII: UDOM Walitaka kulipua Chuo- Prof. Kikula

HATARI HII: UDOM Walitaka kulipua Chuo- Prof. Kikula

Edson Zephania

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2011
Posts
517
Reaction score
112
Jana ktk taarifa ya habari ya radio mwangaza ya saa 1 usiku nilimsikia Prof. Kikula akiwaambia wakuu wa wilaya waliokuwa wametembelea chuo hicho kuwa wanasiasa wasimshinikize kuwarudisha wanafunzi hao kwani anazo taarifa kuwa walitengeneza mabomu ya petroli ili kupambana na Polisi endapo wangekwenda kuwatawanya kwa nguvu hivyo kungepelekea chuo kulipuliwa na kuwaka moto.
 
mh! Ana uhakika au ndo yale ya intelijensia hivi hawa wasomi wetu vipi? Hawajui kuwa ''no research no right to speak''?
 
kashalewa maji ya bendera ya kijani huyo anadhalilisha hata usomi wake jamani mh hiiinji si mcheso
 
Kwa kweli waache siasa wawerejeshe watoto shule. Maana baada yy kushughulikia taaluma anaanza kujiingiza kwenye mambo ya siasa

kuwa strong kikula usilete propaganda za kijinga
 
Dah!!kama ni kweli,hyo ingekua hatar sana...
 
Nakubaliana na Prof Kikula, hizo habari ata mimi nimezisikia kutoka kwa mwanafunzi mmoja ambae kasimamishwa chuo! Inasemekana ni maagizo kutoka kwa Lema
 
Siku zote alikua wapi kusema haya!huu ni uongo kutoka kwa mtu mwenye heshima kwa jamii.acha siasa tekeleza majukumu yako.warudishe masela chuo wakamue kitabu kwani kitaa ni noma.
 
Kuna waliofukuzwa nikiwa mwaka wa kwanza UDSM na taifa likatangaziwa kwamba tuligoma kwenda kufanya kazi vijijini. Hakuna hata mmoja wetu alikuwa amepangiwa kazi vijijini. Hawa CCM wana kawaida ya kutangaza uongo.

Zaidi ya hayo, lengo la kumtupia polisi chupa ya petroli ili asikuumize au kukua (mana hawa polisi wa Tanzania hawakawii kuua) sio LENGO la KULIPUA chuo. Sensationalism will not do!
 
jee? wamekamatwa na hayo mabom au ndousani wakutakakutuaminisha kujipatia kibali chakuwafukuza shure wanafunzi wa sio wataka nakubaki na bendera fata upepo
 
Nakubaliana na Prof Kikula, hizo habari ata mimi nimezisikia kutoka kwa mwanafunzi mmoja ambae kasimamishwa chuo! Inasemekana ni maagizo kutoka kwa Lema
Sio ya Riz1 maana na yeye anatuma vijana watake kumtoa m/kiti wtu wa uvccm mkoa wa Arusha
 
Nakubaliana na Prof Kikula, hizo habari ata mimi nimezisikia kutoka kwa mwanafunzi mmoja ambae kasimamishwa chuo! Inasemekana ni maagizo kutoka kwa Lema
ndugu acha unafiki hakukuwa na mabomu hacheni kutuchafua wanaUDOM. Kikula anatafuta namna ya kujisafisha na kujitetea kwa uma siku zote ukweli utabaki ukweli
 
Nakubaliana na Prof Kikula, hizo habari ata mimi nimezisikia kutoka kwa mwanafunzi mmoja ambae kasimamishwa chuo! Inasemekana ni maagizo kutoka kwa Lema
acha utoto,kama walitaka kufanya hivyo kwa nn wasikamatwe?kila mtawala tz anafanya kazi kwa hisia pasipo elimu zao hilo ndo tatizo kubwa sana,pia kwa kupenda umbeya wanaongoza.wajue nchi itawashinda kwa undumilakuwil wao.
 
acha utoto,kama walitaka kufanya hivyo kwa nn wasikamatwe?kila mtawala tz anafanya kazi kwa hisia pasipo elimu zao hilo ndo tatizo kubwa sana,pia kwa kupenda umbeya wanaongoza.wajue nchi itawashinda kwa undumilakuwil wao.
Wewe na Prof. Kikula nani mtoto? Yaani mtu kupata taarifa kuwa wanafunzi walitaka kulipua chuo ni utoto? Acha upofu wa ufahamu
 
Tanzania ni nchi ya ajabu kweli; mtu akiteuliwa na CCM kushika wadhifa wowote ule ni lazima tuwe makini naye sana kwa sababu hata kama ana digrii ngapi za uzamili, atazifungia uvunguni ili amtumikie bwana mkubwa wa CCM.
 
Wewe na Prof. Kikula nani mtoto? Yaani mtu kupata taarifa kuwa wanafunzi walitaka kulipua chuo ni utoto? Acha upofu wa ufahamu
rudi shule kasome maana ya utoto na upofu mbweha we,kaul bila hatua ya vyombo vya usalama n unafik.achen ushoga fanyen kaz
 
Itatakiwa RPC atoe maelezo kwa hili. Hapa kuna mtu kashindwa kazi. itabidi adhibitishe.
 
Nakubaliana na Prof Kikula, hizo habari ata mimi nimezisikia kutoka kwa mwanafunzi mmoja ambae kasimamishwa chuo! Inasemekana ni maagizo kutoka kwa Lema

Mtoto wa nyoka ni nyoka. Nini kingine umesikia?
 
Jana ktk taarifa ya habari ya radio mwangaza ya saa 1 usiku nilimsikia Prof. Kikula akiwaambia wakuu wa wilaya waliokuwa wametembelea chuo hicho kuwa wanasiasa wasimshinikize kuwarudisha wanafunzi hao kwani anazo taarifa kuwa walitengeneza mabomu ya petroli ili kupambana na Polisi endapo wangekwenda kuwatawanya kwa nguvu hivyo kungepelekea chuo kulipuliwa na kuwaka moto.

Kwenye red
Nashauri pindi wanafunzi wakirudishwa nyumbani kwa maana ya kufunga chuo, walimu na viongozi wa chuo nao wapelekwe likizo isiyo na malipo hadi chuo kitakapofunguliwa. Kama wapo kufundisha na wanafunzi hawapo kwa nini waendelee kulipwa?
 
Back
Top Bottom