Tunadhibiti ubora wa vyeti UDOM-Prof Kikula

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Tunadhibiti ubora wa vyeti UDOM-Prof Kikula


Na Mwandishi Wetu

UONGOZI wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), umetupili mbali madai ya wahitimu wa kozi mbalimbali kuwa vyeti vyao vimecheleweshwa tangu walipohitimu
Novemba mwaka jana, ukidai kuwa hatua hiyo ni muhimu kudhibiti wa ubora wa nyaraka hizo.

Akizungumza na Majira kwa njia ya simu jana, Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Idris Kikula alisema chuo hicho kimeweka utaratibu kuhakikisha vyeti vyake vinakuwa bora zaidi kiasi cha kushindwa kugushiwa na wajanja.

Prof. Kikula alikuwa akijibu swali la gazeti hili kuhusu malalamiko ya baadhi ya wahitimu wa shahada za awali na zile za uzamili kucheleweshewa vyeti hadi sasa.

"Jamani UDOM ni moja kati ya vyuo vikuu vinavyotoa vyeti kwa wakati, kinachofanyika ni kusimamia ubora wake, vyeti vyetu si rahisi kugushi ndio maana tunachapa nje ya nchi na hatuwezi kusema ni wapi maana ni siri yetu," alisema Profesa Kikula.

Hata hivyo Prof. Kikula aliwataka Watanzania hususan wasomi kujenga tabia ya kujiamini na kuwa wadadisi kutafuta taarifa sahihi maeneo husika na kuacha tabia ya kulalamika.

"Jamani tunataka tujenge taifa ya aina gani! Tusiwe walalamikaji tu kwa kila kitu, ni aibu kwa mwanachuo kuhitimu bila kujua taratibu za vyuo vikuu," alisema Prof. Kikula.

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo hicho Utafiti na Taaluma Profesa Ludovick Kinabo, alisema vyeti vya wahitimu wa Chuo hicho vililetwa hata kabla ya mahafali ya kwanza mwaka jana.

"Vyeti vya wahitimu vililetwa mapema, wapo wachache ambao kulikuwa na dosari ndogondogo tulishavipokea jana (juzi Machi 2) kwa DHL," alisema Profesa Kinabo.

Alisema kwa kawaida vyeti vya taaluma vinavyoonesha alama na maendeleo ya taaluma kwa kila mwanafunzi huchelewa kidogo kutokana na uhakiki ili kuepuka makosa yasiyo ya lazima.

Hata hivyo alisema vyeti hivyo pia vitawasili nchini ndani ya wiki mbili kuanzia sasa.
 
PHP:
"Jamani UDOM ni moja kati ya vyuo vikuu vinavyotoa vyeti kwa wakati, kinachofanyika ni kusimamia ubora wake, vyeti vyetu si rahisi kugushi ndio maana tunachapa nje ya nchi na hatuwezi kusema ni wapi maana ni siri yetu," alisema Profesa Kikula.
 
Hata hivyo Prof. Kikula aliwataka Watanzania hususan wasomi kujenga tabia ya kujiamini na kuwa wadadisi kutafuta taarifa sahihi maeneo husika na kuacha tabia ya kulalamika.
 
"Jamani tunataka tujenge taifa ya aina gani! Tusiwe walalamikaji tu kwa kila kitu, ni aibu kwa mwanachuo kuhitimu bila kujua taratibu za vyuo vikuu," alisema Prof. Kikula.
Kuna uhaja wavyuo vyote kuweka kwenye mtandao wahitimu wao na picha zao kuondokana na ukihiyo.........
 
Back
Top Bottom