Hii sio kweli, kama ni kweli basi jokery ..kituko cha mwaka 2016.. Wamekosa ubunifu na hawaoni mbali ...mimi sitaki kuamini bado kama serikali ina mpango huo.
Kwa nini hili ni kituko cha mwaka?
Mosi Harusi zinalipa kodi labda mahari ndio hailipiwi. Arusi zinafanyika kwenye ma Hall ambayo yanalipa kodi.
Harusi wafanya mapambo kwa makampuni yalosajiliwa
Arusi wananunua vinywaji vinavolipia ushuru
Arusi wana chapisha kadi xinazolipiwa kodi
Arusi wana kodi magari yanayolipiwa ushuru
Karibu kila jambo la Arusi linalipiwa kodi , sasa wazo hili sijui linataka kukata kodi kwenye sehemu gani
Kwa ukweli Taifa lolote imara lenye maadili mema linapatikana kutokana na ndoa zinazo tambuliwa ambapo familia hules watoto ambao baadae huwa ndio viongozi wa Taifa. Ndoa ndio msingi wa kukuwa kwa watu . Bila wayu hakuna Taifa. Hivyo Ndoa sio jambo la anasa ni la lazima la kufa na kupona. Wenzetu nchi nyengine ili kulinda maadili mema serikali zao hutoa funds kwa vijana wanao taka kuoa...wengine husaidiwa hata nyumba za kuanza maisha na wengine hupewa bure gharama zote za Arusi. Yote haya ni kwa nia ya kujenga taifa lenye maadili na kuepusha watoto wa mitaani.
Unapo anza kuweka gharama katika ndoa kwa njia ya kodi ina athari sana kwa vijana kukaa bila ya ndoa , na wengine kuamua kukaa ma baro baro bila kuoa.
Kama ni ukweli basi ni upotevu . Viongozi wa dini walikemee serikali inapaswa kuhimiza ndoa ..kuondoa uchafu katika jamii na kupunguza ukimwi. Ikiwezekana ichangie gharama za arusi hata kwa mikopo..
Hivi serikali zetu zina ogopa nini kuangalia upya sera za madini na kuweka mipango madhubuti ya kupata faida zaidi huko ? Kila kiongoxi akija anakuja na sera za kukamua raia ...huku kwenye madini gas wapo kimya kabisa na hakuna mwenye uchungu kabisa..mna faidikia huko .
Kama kweli hilo la kodi ya arusi ni upotovu mkubwa kabisa ambao haujawahi kufanywa