Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
HALI ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari hapa nchini, Dk. Stephen Ulimboka, inazidi kuzorota na madaktari walio karibu naye wamelidokeza Tanzania Daima Jumapili, kuwa sasa wanasubiri Kudra za Mwenyezi Mungu
Kiongozi huyo ambaye alitekwa, kuteswa na kutupwa katika msitu wa Mabwepande jijini Dar es Salaam mwishoni mwa mwezi uliopita anatibiwa katika hospitali moja nchini Afrika Kusini ambayo hadi sasa haijawekwa wazi.
Mmoja wa madaktari ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini alisema kiongozi huyo aliyelazwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi yumo katika koma, ambayo ni hali ya nusu mfu - nusu hai, na anahitaji zaidi sala za Watanzania.
Huwezi kusema anaendelea vizuri, jambo muhimu hapa ni kumwomba Mungu awaongezee maarifa madaktari wale ili kupigania uhai wa mwenzetu.
Kwa hali aliyoondoka nayo hapa nchini na jinsi tunavyopokea taarifa kutoka huko, kwakweli hazileti matumaini, alisema Dk. huyo.
Dk. Ulimboka inadaiwa amepata madhara makubwa katika figo zake ambapo ilidaiwa moja ilipata ufa na nyingine iligoma kufanya kazi, baadhi ya mbavu zake zimepata majeraha.
Kichwa cha daktari huyo pia kilipata hitilafu kutokana na kipigo hicho kinachodaiwa kufanywa na maofisa Usalama wa Taifa ingawa serikali imekana kuhusika na kitendo hicho cha kinyama.
Baadhi ya madaktari waliozungumza na Tanzania Daima Jumapili jana jijini Dar es Salaam katika mkutano na viongozi wa dini wamesema ukweli wa kipigo cha kiongozi huyo hautawekwa wazi.
Walibainisha kuwa hawana imani na tume itakayoundwa au iliyoundwa kushughulikia jambo hilo kwa sababu tayari viongozi wa serikali wamesema serikali haihusiki.
Rais, waziri wamesema serikali haihusiki na tukio hili, sasa kama tume ikibaini kuna mkono wa serikali ukweli utawekwa wazi hapo? alihoji mmoja wa madaktari.
Tanzania Daima Jumapili liliwasiliana na Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania, Namala Mkopi, kuhusu afya ya Dk. Ulimboka ambapo aligoma kuzungumzia suala hilo.
Dk. Mkopi alisema jana walikuwa kwenye mazungumzo na viongozi wa dini kuhusu mgomo wa madaktari na si vinginevyo.
Viongozi wa dini waingilia
Wakati hali ya Dk. Ulimboka ikizidi kuwa tete, viongozi wa dini nchini wamemtaka Rais Jakaya Kikwete akutane nao pamoja na madaktari ili kuupatia ufumbuzi mgomo wa madaktari.
Viongozi hao walisema mgomo wa madaktari unaoendelea hivi sasa unawatesa wananchi wasio na hatia.
Kauli ya viongozi hao wa dini ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Sheikh Said Mwaipopo mara baada ya kikao chao na madaktari.
Sheikh Mwaipopo alisema wamechukua hatua hiyo baada ya kubaini kuwa serikali inasuasua kulizungumzia jambo hilo kwa makini na kulipatia ufumbuzi ili kuokoa maisha ya watu wa kipato cha chini wanaotegemea hospitali za serikali.
Kuna mambo mbalimbali yanaweza kutokea, inawezekana taarifa sahihi hazimfikii Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, hivyo tunaomba kukutana naye kwa mazungumzo ya amani ili kurudisha hali ya amani nchini, aliongeza Mwaipopo.
Sheikh Mwaipopo alifafanua kuwa tamko lao limejigawa katika sehemu kuu tano, ambapo wanaamini kukutana huko kunaweza kuwa ishara ya kumaliza mgogoro unaowakabili na kutafutiwa ufumbuzi wa haraka.
Alisema miongoni mwa mambo waliyoazimia ni kuitaka serikali ifute kesi iliyoifungua Mahakama Kuu Kitengo cha Kazi, ambayo ilitoa zuio la mgomo huo.
Aliongeza kuwa pia wameitaka iwarejeshe madaktari wote walioachishwa kazi pamoja na Rais Kikwete akubali kukutana na viongozi wa dini, wanaharakati wa haki za binadamu na madaktari.
Naye Mchungaji wa EAGT Mabibo, Lawrence Mnzavaz, alisema hawahusiki na tuhuma zinazovumishwa kuhusu tukio lililotokea la Dk. Ulimboka, kwa sababu hakuna aliyeshuhudia uovu huo unavyofanyika.
Alisema tamko lao halitakubaliana na kauli ya aina yoyote itakayowataka wananchi kuandamana, kwani wanaamini hiyo si njia sahihi ya kumaliza tatizo lililopo.
Kiongozi huyo alisema iwapo rais atashauriwa vibaya na kukataa kukutana na umoja wa viongozi hao, hawatakuwa na la kufanya kwa sababu maamuzi hayo yatakuwa yamefanywa na kiongozi wa nchi.
Kiongozi huyo ambaye alitekwa, kuteswa na kutupwa katika msitu wa Mabwepande jijini Dar es Salaam mwishoni mwa mwezi uliopita anatibiwa katika hospitali moja nchini Afrika Kusini ambayo hadi sasa haijawekwa wazi.
Mmoja wa madaktari ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini alisema kiongozi huyo aliyelazwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi yumo katika koma, ambayo ni hali ya nusu mfu - nusu hai, na anahitaji zaidi sala za Watanzania.
Huwezi kusema anaendelea vizuri, jambo muhimu hapa ni kumwomba Mungu awaongezee maarifa madaktari wale ili kupigania uhai wa mwenzetu.
Kwa hali aliyoondoka nayo hapa nchini na jinsi tunavyopokea taarifa kutoka huko, kwakweli hazileti matumaini, alisema Dk. huyo.
Dk. Ulimboka inadaiwa amepata madhara makubwa katika figo zake ambapo ilidaiwa moja ilipata ufa na nyingine iligoma kufanya kazi, baadhi ya mbavu zake zimepata majeraha.
Kichwa cha daktari huyo pia kilipata hitilafu kutokana na kipigo hicho kinachodaiwa kufanywa na maofisa Usalama wa Taifa ingawa serikali imekana kuhusika na kitendo hicho cha kinyama.
Baadhi ya madaktari waliozungumza na Tanzania Daima Jumapili jana jijini Dar es Salaam katika mkutano na viongozi wa dini wamesema ukweli wa kipigo cha kiongozi huyo hautawekwa wazi.
Walibainisha kuwa hawana imani na tume itakayoundwa au iliyoundwa kushughulikia jambo hilo kwa sababu tayari viongozi wa serikali wamesema serikali haihusiki.
Rais, waziri wamesema serikali haihusiki na tukio hili, sasa kama tume ikibaini kuna mkono wa serikali ukweli utawekwa wazi hapo? alihoji mmoja wa madaktari.
Tanzania Daima Jumapili liliwasiliana na Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania, Namala Mkopi, kuhusu afya ya Dk. Ulimboka ambapo aligoma kuzungumzia suala hilo.
Dk. Mkopi alisema jana walikuwa kwenye mazungumzo na viongozi wa dini kuhusu mgomo wa madaktari na si vinginevyo.
Viongozi wa dini waingilia
Wakati hali ya Dk. Ulimboka ikizidi kuwa tete, viongozi wa dini nchini wamemtaka Rais Jakaya Kikwete akutane nao pamoja na madaktari ili kuupatia ufumbuzi mgomo wa madaktari.
Viongozi hao walisema mgomo wa madaktari unaoendelea hivi sasa unawatesa wananchi wasio na hatia.
Kauli ya viongozi hao wa dini ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Sheikh Said Mwaipopo mara baada ya kikao chao na madaktari.
Sheikh Mwaipopo alisema wamechukua hatua hiyo baada ya kubaini kuwa serikali inasuasua kulizungumzia jambo hilo kwa makini na kulipatia ufumbuzi ili kuokoa maisha ya watu wa kipato cha chini wanaotegemea hospitali za serikali.
Kuna mambo mbalimbali yanaweza kutokea, inawezekana taarifa sahihi hazimfikii Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, hivyo tunaomba kukutana naye kwa mazungumzo ya amani ili kurudisha hali ya amani nchini, aliongeza Mwaipopo.
Sheikh Mwaipopo alifafanua kuwa tamko lao limejigawa katika sehemu kuu tano, ambapo wanaamini kukutana huko kunaweza kuwa ishara ya kumaliza mgogoro unaowakabili na kutafutiwa ufumbuzi wa haraka.
Alisema miongoni mwa mambo waliyoazimia ni kuitaka serikali ifute kesi iliyoifungua Mahakama Kuu Kitengo cha Kazi, ambayo ilitoa zuio la mgomo huo.
Aliongeza kuwa pia wameitaka iwarejeshe madaktari wote walioachishwa kazi pamoja na Rais Kikwete akubali kukutana na viongozi wa dini, wanaharakati wa haki za binadamu na madaktari.
Naye Mchungaji wa EAGT Mabibo, Lawrence Mnzavaz, alisema hawahusiki na tuhuma zinazovumishwa kuhusu tukio lililotokea la Dk. Ulimboka, kwa sababu hakuna aliyeshuhudia uovu huo unavyofanyika.
Alisema tamko lao halitakubaliana na kauli ya aina yoyote itakayowataka wananchi kuandamana, kwani wanaamini hiyo si njia sahihi ya kumaliza tatizo lililopo.
Kiongozi huyo alisema iwapo rais atashauriwa vibaya na kukataa kukutana na umoja wa viongozi hao, hawatakuwa na la kufanya kwa sababu maamuzi hayo yatakuwa yamefanywa na kiongozi wa nchi.