Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,267
- 9,715
Ndugu zangu Watanzania,
Aliyekuwa katibu wa Rais mstaafu ndugu Dkt Abdallal makame amesema ya kuwa mzee Alli Hassan Mwinyi Rais mstaafu wa awamu ya pili ,Anaendelea kupatiwa matibabu ya kifua chini ya uangalizi wa madaktari bingwa.
Amesema kuwa hakuna mipango ya kumsafirisha na kumpeleka nje ya nchi kwa sasa labda kama madaktari wataona kuna haja ya kumsafirisha na kufanya hivyo hapo baadaye kwenda nje ya nchi ,lakini kwa sasa ataendelea kupatiwa matibabu na madaktari wetu bingwa hapa hapa nchini.
Rai yangu Watanzania tuendelee kumuombea mzee wetu huyu apone na kurejea katika hali yake ya kawaida.Mungu amponye haraka na aendelee kumjalia na kumuongezea siku za kuishi hapa Duniani.ili hatimaye hapo mwakani aweze kutimiza miaka mia moja yaani karne moja tangia kuzaliwa kwake Tarehe 8-5-1925.
Itakumbukwa ya kuwa ni wakati wa awamu yake ambapo ndipo mfumo wa vyama vingi hapa nchini ulipoanzishwa ,licha ya kwamba wengi wa watanzania walikuwa hawaafiki na hawautaki mfumo wa vyama vingi ambapo 80% ya watanzania walisema wangependa tuendelee na mfumo wa chama kimoja.
Ni wakati wa utawala na uongozi wake ndipo kulipofanyika mageuzi makubwa ya kiuchumi,ambapo Secta Binafsi zikaanza kukua na kustawi,maisha ya watanzania yakaanza kuimarika, Watanzania wakaanza kumiliki mali nyingi tu binafsi na kuwa na haki ya kugombea nafasi za uongozi tofauti na hapo awali ambapo kuwa tajiri au kuwa na mali nyingi ilikuwa kitu au jambo ambalo lingekunyima nafasi ya kupewa uongozi au kuulizwa maswali ya umepata wapi mali zote hizo.
Uongozi wa mzee wetu Mwinyi ulileta uhuru wa kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja na kila mwenye juhudi binafsi aliinuka kiuchumi na kumiliki mali na utajiri mkubwa bila hofu yoyote ile. Ni wakati wake hata mambo ya uwekezaji yaliongezeka sana hapa nchini,lakini pia serikali ilianza kujiondoa taratibu katika kufanya biashara na badala yake kubakia msimamizi ili kubaki na jukumu la kukusanya kodi tu.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
Aliyekuwa katibu wa Rais mstaafu ndugu Dkt Abdallal makame amesema ya kuwa mzee Alli Hassan Mwinyi Rais mstaafu wa awamu ya pili ,Anaendelea kupatiwa matibabu ya kifua chini ya uangalizi wa madaktari bingwa.
Amesema kuwa hakuna mipango ya kumsafirisha na kumpeleka nje ya nchi kwa sasa labda kama madaktari wataona kuna haja ya kumsafirisha na kufanya hivyo hapo baadaye kwenda nje ya nchi ,lakini kwa sasa ataendelea kupatiwa matibabu na madaktari wetu bingwa hapa hapa nchini.
Rai yangu Watanzania tuendelee kumuombea mzee wetu huyu apone na kurejea katika hali yake ya kawaida.Mungu amponye haraka na aendelee kumjalia na kumuongezea siku za kuishi hapa Duniani.ili hatimaye hapo mwakani aweze kutimiza miaka mia moja yaani karne moja tangia kuzaliwa kwake Tarehe 8-5-1925.
Itakumbukwa ya kuwa ni wakati wa awamu yake ambapo ndipo mfumo wa vyama vingi hapa nchini ulipoanzishwa ,licha ya kwamba wengi wa watanzania walikuwa hawaafiki na hawautaki mfumo wa vyama vingi ambapo 80% ya watanzania walisema wangependa tuendelee na mfumo wa chama kimoja.
Ni wakati wa utawala na uongozi wake ndipo kulipofanyika mageuzi makubwa ya kiuchumi,ambapo Secta Binafsi zikaanza kukua na kustawi,maisha ya watanzania yakaanza kuimarika, Watanzania wakaanza kumiliki mali nyingi tu binafsi na kuwa na haki ya kugombea nafasi za uongozi tofauti na hapo awali ambapo kuwa tajiri au kuwa na mali nyingi ilikuwa kitu au jambo ambalo lingekunyima nafasi ya kupewa uongozi au kuulizwa maswali ya umepata wapi mali zote hizo.
Uongozi wa mzee wetu Mwinyi ulileta uhuru wa kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja na kila mwenye juhudi binafsi aliinuka kiuchumi na kumiliki mali na utajiri mkubwa bila hofu yoyote ile. Ni wakati wake hata mambo ya uwekezaji yaliongezeka sana hapa nchini,lakini pia serikali ilianza kujiondoa taratibu katika kufanya biashara na badala yake kubakia msimamizi ili kubaki na jukumu la kukusanya kodi tu.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.