Hapo ndo kwetu! Mje Sasa!

Pukudu

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
3,148
2,219
ImageUploadedByJamiiForums1344571831.583546.jpg
Tumewaambia kabisa mje Sasa tuone!
 
Hivi kweli waIslam mmedhamiria hili jambo? Kweli hili limepata 'kibali' mbele ya Allah? Tusubiri tuone...
 
duh kali kuliko . je mawakala nao wamekataa au kwa vile kuna posho??
 
Inamaanisha nini hii?
Isn't this Insinuation?....kama hujachonga mwenyewe maandishi hayo sema umeyapata wapi!
 
Mmmmmmmmmmhhhhh!!!!!!!!!!! hii umejitengenezea, big up 4 trying
 
mie ni muislamu, lakini sijajua mantiki ya kugomea sensa.

kwa ninavyo fahamu mimi, madhumuni ya sensa ni kusaidia kupanga maendeleo. mathalani, waweza kusonga ugali bila kujua idadi ya walaji? mfano mwingine dhahiri wa sensa nipale janga la njaa linapo tokea utajua mahitaji halisi ya wahanga, idadi kuamua pahala pa kuweka huduma muhimu kama soko, ama zahanati, ama vituo vya pollisi ama idara za mahakama, ni kutokana na idadi ya watu katika eneo husiki. maa muzi kama kugawa wilaya kuwa mkoa, na kuunda tarafa nyinine, ili kuharakisha maendeleo. mambo haya si dhani kama UISILAMU UNAKATAA
 
BRODA, hawa waislamu wenye ufinyu wa mawazo wanasikitisha sana.
Ni bahati nzuri kuwa mpo baadhi wenye uelewa mzuri ambao bila shaka mtasaidia kuerevusha jamii yenye kutu kichwani.
Nilitegemea Waislamu wagome kuwa hawahesabiwi hadi kesi zote za wezi wa mali ya umma zifanyiwe kazi, kumbe wao udini mbele.
 
mie ni muislamu, lakini sijajua mantiki ya kugomea sensa.

kwa ninavyo fahamu mimi, madhumuni ya sensa ni kusaidia kupanga maendeleo. mathalani, waweza kusonga ugali bila kujua idadi ya walaji? mfano mwingine dhahiri wa sensa nipale janga la njaa linapo tokea utajua mahitaji halisi ya wahanga, idadi kuamua pahala pa kuweka huduma muhimu kama soko, ama zahanati, ama vituo vya pollisi ama idara za mahakama, ni kutokana na idadi ya watu katika eneo husiki. maa muzi kama kugawa wilaya kuwa mkoa, na kuunda tarafa nyinine, ili kuharakisha maendeleo. mambo haya si dhani kama UISILAMU UNAKATAA

uislamu hau katazi sensa kama itakuwa ni ya kuridhisha,lkn tuna kata kuhesabiwa kwendana na serikali kuto kukubali madai yetu,



kama bado hujuwi basi soma hapa chini



KWA NINI WAISLAMU TUNAKATAA KUSHIRIKI KATIKA SENSA 2012
Nchi yetu imefanya sensa sita hadi sasa, mbili wakati wa ukoloni (1948,
1957) na nne katika Tanzania huru (1967, 1978, 1988 na 2002). Mara
zote hizo, waislamu wameshiriki sensa wakiamini kwamba ni zoezi
muhimu kwa maendeleo ya Taifa na hawakuwa na sababu ya kususia
sensa kutokana na historia ya dini yetu kuhimiza sensa.
Tatizo lililojitokeza mwaka huu na kupelekea waislamu kuamua kuisusia
sensa ijayo mwaka huu lilianzia na taarifa ya TBC1 iliyotolewa tarehe 26
Aprili, 2012 kwamba idadi ya wakristo nchini ni 52% na waislamu ni 32%.
Takwimu hizi sasa zinatumika kuhalalisha mgawanyo mbovu wa nafasi
za madaraka nnchini kwamba wakristo ni wengi katika nafasi mbali mbali
kwa sababu wao ni wengi.
Pamoja na Mkurugenzi wa TBC1 kukanusha mara kadhaa kwamba
takwimu hizo si sahihi, tumeng’amua kwamba kuna udini katika zoezi
zima la sensa na tayari kuna takwimu za idadi ya watanzania kwa dini
zao ambazo zinaonesha kuwa wakristo ni wengi kuliko waislamu na pia
kuna matumizi mabaya ya takwimu za sensa dhidi ya waislamu.
Udini katika zoezi la Sensa.
Mosi, Tumekuwa tukifuatilia zoezi la majaribio la sensa lililofanyika
mwanzoni mwa mwaka huu na tulichogundua ni kwamba maafisa
walioenesha zoezi hilo wengi wao walikuwa wakristo hadi dereva wa gari
hata maeneo ambayo waislamu ni wengi.
Katika mazingira haya na huku tayari kukiwa na takwimu zinazoonesha
idadi ya watanzania kwa mujibu wa dini zao zinazotolewa kupitia vyombo
vya habari vya serikali, ofisi na idara za serikali, tovuti mbali mbali za
taasisi za Kikristo na za asasi nyingine zisizo za kiserikali za ndani na nje
ya nchi, tukishiriki katika zoezi la sensa lijalo tutayapa nguvu tu madai
yao kwamba wakristo nchini ni wengi kuliko waislamu.
Mifano ya takwimu hizo
Tovuti ya wakatoliki – Wakristo 44%, Waislamu 34%
Kalenda Ofisi ya Serikali – Wakristo ,Waislamu
Tovuti ya Mambo ya Nje Marekani – Wakristo 62%, Waislamu 32%
Pili, viongozi wa Kikristo wamekuwa msitari wa mbele kupinga kutiwa
kipengele cha dini katika dodoso la sensa. Katika mazingira ya takwimu
tata ambazo hata Mkurugenzi wa idara ya takwimu anakiri kwamba si
takwimu sahihi ombi letu la kuwekwa kipengele cha dini katika dodoso la
sensa lingepokelewa kama ufumbuzi wa utata huo ili tuwe na takwimu
sahihi za idadi ya watanzania kwa dini zao lakini serikali imekataa kata
kata na inaunga mkono msimamo wa wakristo kutokuwekwa kipengele
cha dini katika dodoso la sensa, wakristo ambao tayari wanadai wao
wako wengi kuliko waislamu.
Tatu, dodoso la sensa limeandaliwa kuja kunufaisha wakristo kwa sababu
linauliza kuhusu idadi ya makanisa na misikiti wakati serikali imekataa
kuhusisha sensa na dini. Tuna shaka kwamba huu ni mpango wa
kuwawezesha wakristo kuchakachua takwimu hizo za majumba ya ibada
kuthibitisha kwamba wao ni wengi kuliko waislamu kama ambavyo tayari
wanadai.
Izingatiwe kwamba idadi ya makanisa itakuwa kubwa kuliko misikiti
kutokana na tofauti za kimadhehebu za wakristo hata pale ambapo wao
si wengi kwani katika Ukristo waumini wa dhehebu moja hawawezi
kufanya ibada katika Kanisa lisilo la dhehebu lao. Katika kijiji utakuta
makanisa manne mpaka matano au zaidi lakini msikiti ni mmoja tu
kutokana na ukweli kwamba waislamu huswali msikiti wowote hivyo
hawawezi kuwa na misikiti mingi kama makanisa.
 
uislamu hau katazi sensa kama itakuwa ni ya kuridhisha,lkn tuna kata kuhesabiwa kwendana na serikali kuto kukubali madai yetu,



kama bado hujuwi basi soma hapa chini



KWA NINI WAISLAMU TUNAKATAA KUSHIRIKI KATIKA SENSA 2012
Nchi yetu imefanya sensa sita hadi sasa, mbili wakati wa ukoloni (1948,
1957) na nne katika Tanzania huru (1967, 1978, 1988 na 2002). Mara
zote hizo, waislamu wameshiriki sensa wakiamini kwamba ni zoezi
muhimu kwa maendeleo ya Taifa na hawakuwa na sababu ya kususia
sensa kutokana na historia ya dini yetu kuhimiza sensa.
Tatizo lililojitokeza mwaka huu na kupelekea waislamu kuamua kuisusia
sensa ijayo mwaka huu lilianzia na taarifa ya TBC1 iliyotolewa tarehe 26
Aprili, 2012 kwamba idadi ya wakristo nchini ni 52% na waislamu ni 32%.
Takwimu hizi sasa zinatumika kuhalalisha mgawanyo mbovu wa nafasi
za madaraka nnchini kwamba wakristo ni wengi katika nafasi mbali mbali
kwa sababu wao ni wengi.
Pamoja na Mkurugenzi wa TBC1 kukanusha mara kadhaa kwamba
takwimu hizo si sahihi, tumeng'amua kwamba kuna udini katika zoezi
zima la sensa na tayari kuna takwimu za idadi ya watanzania kwa dini
zao ambazo zinaonesha kuwa wakristo ni wengi kuliko waislamu na pia
kuna matumizi mabaya ya takwimu za sensa dhidi ya waislamu.
Udini katika zoezi la Sensa.
Mosi, Tumekuwa tukifuatilia zoezi la majaribio la sensa lililofanyika
mwanzoni mwa mwaka huu na tulichogundua ni kwamba maafisa
walioenesha zoezi hilo wengi wao walikuwa wakristo hadi dereva wa gari
hata maeneo ambayo waislamu ni wengi.
Katika mazingira haya na huku tayari kukiwa na takwimu zinazoonesha
idadi ya watanzania kwa mujibu wa dini zao zinazotolewa kupitia vyombo
vya habari vya serikali, ofisi na idara za serikali, tovuti mbali mbali za
taasisi za Kikristo na za asasi nyingine zisizo za kiserikali za ndani na nje
ya nchi, tukishiriki katika zoezi la sensa lijalo tutayapa nguvu tu madai
yao kwamba wakristo nchini ni wengi kuliko waislamu.
Mifano ya takwimu hizo
Tovuti ya wakatoliki – Wakristo 44%, Waislamu 34%
Kalenda Ofisi ya Serikali – Wakristo ,Waislamu
Tovuti ya Mambo ya Nje Marekani – Wakristo 62%, Waislamu 32%
Pili, viongozi wa Kikristo wamekuwa msitari wa mbele kupinga kutiwa
kipengele cha dini katika dodoso la sensa. Katika mazingira ya takwimu
tata ambazo hata Mkurugenzi wa idara ya takwimu anakiri kwamba si
takwimu sahihi ombi letu la kuwekwa kipengele cha dini katika dodoso la
sensa lingepokelewa kama ufumbuzi wa utata huo ili tuwe na takwimu
sahihi za idadi ya watanzania kwa dini zao lakini serikali imekataa kata
kata na inaunga mkono msimamo wa wakristo kutokuwekwa kipengele
cha dini katika dodoso la sensa, wakristo ambao tayari wanadai wao
wako wengi kuliko waislamu.
Tatu, dodoso la sensa limeandaliwa kuja kunufaisha wakristo kwa sababu
linauliza kuhusu idadi ya makanisa na misikiti wakati serikali imekataa
kuhusisha sensa na dini. Tuna shaka kwamba huu ni mpango wa
kuwawezesha wakristo kuchakachua takwimu hizo za majumba ya ibada
kuthibitisha kwamba wao ni wengi kuliko waislamu kama ambavyo tayari
wanadai.
Izingatiwe kwamba idadi ya makanisa itakuwa kubwa kuliko misikiti
kutokana na tofauti za kimadhehebu za wakristo hata pale ambapo wao
si wengi kwani katika Ukristo waumini wa dhehebu moja hawawezi
kufanya ibada katika Kanisa lisilo la dhehebu lao. Katika kijiji utakuta
makanisa manne mpaka matano au zaidi lakini msikiti ni mmoja tu
kutokana na ukweli kwamba waislamu huswali msikiti wowote hivyo
hawawezi kuwa na misikiti mingi kama makanisa.

nime kuelewa,

lakini nadhani hizo takwimu ni sampuli tu ambazo zinaweza kuwa sahihi ama sio sahihi, ndio maana zina tofautiana kutaka taasisi moja na nyingine. mathalani, wakati wa uchaguzi mkuu taasisi ya REDET na SYNOVET walitoa takwimu za ushindi wa raisi KIKWETE , makadirio ya kitafiti ambayo hayakuwa ya sahihi ( accuracy) kwa asilimia mia kwa mia lakini yalikuwa yanakaribiana na kutupa picha ya mwelekeo wa matoke wa uchaguzi mkuu mwaka 2010. makanisa na balozi walichukua sampuli na kutoa makario ya idadi ya waisilamu na wakristo, lakini hakuna sensa iliyo fanyika ndio maana takwimu zao zina tofautiana , kama ilifanyika basi walisahau kunihesabu.

kwanini makanisa yana hitaji takwimu za idadi ya waisilamu na wakristo

  • tuwaachie wenyewe wanajua ndio maana wanazo

kwanini Bakwata itahitaji takwimu za idadi ya wakristo na waisilamu:
  • kwasababu uisalamu ni dini ya kweli lazima dunia ikombolewe, dhima hii kwa tanzania wanayo BAKWATA na nilazima wajue wana watu wangapi na ipo kazi kiasi gani kuongeza ushawishi kwa makafiri (au walio kufuru) ili KUSILIMU
  • kwasababu bakwata inahitaji kupanga maendeleo ya waisilamu, ikiwa ni misikiti, madrasa, shule, vyuo vikuu . hivi ukienda bakwata ukiuliza Tanzania ina waisilimu wangapi, kati yao wanawake ni wangapi, na wanaume ni wangapi, na kati ya hao wana elimu kiasi gani (elimu dunia na akhera). takwimu hizi ni za msingi bakwata kuwa nazo ili kupanga maendeleo ya muisilamu mmoja mmoja na kwa makundi

hili la TBC kuwa na Takwimu hizo , labda watakuwa wamechukulia huko huko kwa makanisa na sioni tatizo la matumizi ya takwimu hizo kwa shirika hilo la utangazaji

hitimisho

 
Nimewaelewa na ninakubaliana nanyi Bw.Achahasira na Mandown ila sidhani kama ni jambo jema kususia sensa tukumbuke hao wakristo ni makafiri ambao malipo yao ni hapa hapa duniani si vyema kubishana na makafiri kwa kuwa tunapoteza muda na nguvu ambazo tungezitumia kuimarisha uislamu.
 
Nimewaelewa na ninakubaliana nanyi Bw.Achahasira na Mandown ila sidhani kama ni jambo jema kususia sensa tukumbuke hao wakristo ni makafiri ambao malipo yao ni hapa hapa duniani si vyema kubishana na makafiri kwa kuwa tunapoteza muda na nguvu ambazo tungezitumia kuimarisha uislamu.



kamwendo,


kwa uchunguzi nilioufanya kwa majamaa na marafiki wote wanao susia sensa ni kuwa hawapendezwi na njia hiyo lkn hawana njia nyingine ya kuonesha msimamo wao juu ya serikali.

serikali mara nyingi imekuwa ikiwachukulia waislamu ni bakwata hata kama wakijuwa bakwata HAIPENDWI NA HAIKUBALIKI na waislamu wengi.hii ndio moja ya sababu kuu ya kususia sensa inaweza kuonekana ni ndogo lkn hii tatizo ndio linalo zaa matatizo mengine yoooote ya leo na ya kesho.

uislam sio dini ya kuingia msikitini na kutoka tu,uislam ni mfumo kamili wa maisha ya mwanadamu.

mtume muhamad salalahu aleyhi wasalam alijenga taifa la kiislamu madina,ikumbukwe taifa lake lilikuwa na mayahudi na wapagani wengi tu.hakufundisha waislamu kusali msikitini na kuto kuleta mabadiliko katika yale wanayo yaona si sawa.

uislamu upo kwaajili ya kupigania haki kwa wote,hii inaweza kuwa ni kitu kigeni kwenye macho ya baadhi ya waislamu na wakristu.kama nchi inakandamiza sehemu mmoja basi tuna WAJIBU wakukemea kwa vitendo au hata kuonesha kuwa tumechukizwa.

serikali imekuwa ikiwapa nafasi kubwa makanisa kuliko waislamu kwa madai ya makanisa kuwa wao wapo wengi,na wakirusha takwimu za makanisa kwenye vyombo vya habari na wakijua kuwa takwimu hizo sio za ukweli kabisa.

ni kitu cha wazi kabisa kuwa nchi hii imegawanywa na makundi mawili ya kidini,na serikali kunyamazia haisaidi chochote bali huleta maafa tu mbeleni,serikali ina wajibu wakusikiliza madai ya waislamu na kuyafanyia kazi,hii itasaidia katika maendeleo ya nchi kwa badae,


ndugu kamwendo na imani kuwa umesoma hata kidogo siraa ya dini yako basi ningekuomba upitie.
 
Achahasira Ulichoandika ni hatari. Ukumbuke Kuwa huwezi kulazimisha mawazo Yako yakubaliwe na Watu wote. Mtoa takwimu katika nchi yeyote ni mtakwimu mkuu wa Serikali. Achana na takwimu za tovuti hata vyombo vya habari. Umeambiwa Kuwa tangu uhuru Serikali iliamua kuachana na maswali mawili yaani dini na kabila ili kujenga mshikamano. Nadhani ulijionea matatizo ya ukabila yalivyotaka kuisambaratisha Kenya wakati wa uchaguzi. Huko Nigeria unaona udini unavyowatafuna. Kwa maoni yangu Huku ni kuondoa umaskini kwa kutumia mgongo wa dini hasa pale unaposema .........Tumekuwa tukifuatilia zoezi la majaribio la sensa lililofanyika
mwanzoni mwa mwaka huu na tulichogundua ni kwamba maafisa
walioenesha zoezi hilo wengi wao walikuwa wakristo hadi dereva wa gari
hata maeneo ambayo waislamu ni wengi........
naomba nikujuze Kuwa ingawa Mimi ni binti wa kiisilamu siliungi mkono maana nisingependa nipate kazi kwa vile ati pengine kwa sababu ya ujinsi au imani yangu.

Pia umenena........

dodoso la sensa limeandaliwa kuja kunufaisha wakristo kwa sababu
linauliza kuhusu idadi ya makanisa na misikiti wakati serikali imekataa
kuhusisha sensa na dini. Tuna shaka kwamba huu ni mpango wa
kuwawezesha wakristo kuchakachua takwimu hizo za majumba ya ibada
kuthibitisha kwamba wao ni wengi kuliko waislamu kama ambavyo tayari
wanadai........

Hapa pia Nadhani hujafanya utafiti wa kutosha. Ni Kweli Kuwa wakati wa sensa ya majaribio kulikuwa na section iliyohusu huduma za jamii ikijumuisha Shule, hospitali, upatikanaji wa maji, matukio yaliyotokea katika Jumuia, matundu ya vyoo katika Shule, idadi ya waalimu n.k. Kama ujuavyo ile ilikuwa ni pilot na baada ya kufanya uchambuzi ikaonekana section Hii haikuwa na tija ikaondolewa. Naomba nikuthibitishie mwislamu mwenzangu Kuwa swali linalohusu idadi ya makanisa au misikiti halipo katika dodoso la sensa.
 
Back
Top Bottom