View attachment 61411
Tumewaambia kabisa mje Sasa tuone!
Hapo ndani pakiingizwa up...u watoka na kuhesabiwa mmoja mmoja!View attachment 61411
Tumewaambia kabisa mje Sasa tuone!
mie ni muislamu, lakini sijajua mantiki ya kugomea sensa.
kwa ninavyo fahamu mimi, madhumuni ya sensa ni kusaidia kupanga maendeleo. mathalani, waweza kusonga ugali bila kujua idadi ya walaji? mfano mwingine dhahiri wa sensa nipale janga la njaa linapo tokea utajua mahitaji halisi ya wahanga, idadi kuamua pahala pa kuweka huduma muhimu kama soko, ama zahanati, ama vituo vya pollisi ama idara za mahakama, ni kutokana na idadi ya watu katika eneo husiki. maa muzi kama kugawa wilaya kuwa mkoa, na kuunda tarafa nyinine, ili kuharakisha maendeleo. mambo haya si dhani kama UISILAMU UNAKATAA
uislamu hau katazi sensa kama itakuwa ni ya kuridhisha,lkn tuna kata kuhesabiwa kwendana na serikali kuto kukubali madai yetu,
kama bado hujuwi basi soma hapa chini
KWA NINI WAISLAMU TUNAKATAA KUSHIRIKI KATIKA SENSA 2012
Nchi yetu imefanya sensa sita hadi sasa, mbili wakati wa ukoloni (1948,
1957) na nne katika Tanzania huru (1967, 1978, 1988 na 2002). Mara
zote hizo, waislamu wameshiriki sensa wakiamini kwamba ni zoezi
muhimu kwa maendeleo ya Taifa na hawakuwa na sababu ya kususia
sensa kutokana na historia ya dini yetu kuhimiza sensa.
Tatizo lililojitokeza mwaka huu na kupelekea waislamu kuamua kuisusia
sensa ijayo mwaka huu lilianzia na taarifa ya TBC1 iliyotolewa tarehe 26
Aprili, 2012 kwamba idadi ya wakristo nchini ni 52% na waislamu ni 32%.
Takwimu hizi sasa zinatumika kuhalalisha mgawanyo mbovu wa nafasi
za madaraka nnchini kwamba wakristo ni wengi katika nafasi mbali mbali
kwa sababu wao ni wengi.
Pamoja na Mkurugenzi wa TBC1 kukanusha mara kadhaa kwamba
takwimu hizo si sahihi, tumeng'amua kwamba kuna udini katika zoezi
zima la sensa na tayari kuna takwimu za idadi ya watanzania kwa dini
zao ambazo zinaonesha kuwa wakristo ni wengi kuliko waislamu na pia
kuna matumizi mabaya ya takwimu za sensa dhidi ya waislamu.
Udini katika zoezi la Sensa.
Mosi, Tumekuwa tukifuatilia zoezi la majaribio la sensa lililofanyika
mwanzoni mwa mwaka huu na tulichogundua ni kwamba maafisa
walioenesha zoezi hilo wengi wao walikuwa wakristo hadi dereva wa gari
hata maeneo ambayo waislamu ni wengi.
Katika mazingira haya na huku tayari kukiwa na takwimu zinazoonesha
idadi ya watanzania kwa mujibu wa dini zao zinazotolewa kupitia vyombo
vya habari vya serikali, ofisi na idara za serikali, tovuti mbali mbali za
taasisi za Kikristo na za asasi nyingine zisizo za kiserikali za ndani na nje
ya nchi, tukishiriki katika zoezi la sensa lijalo tutayapa nguvu tu madai
yao kwamba wakristo nchini ni wengi kuliko waislamu.
Mifano ya takwimu hizo
Tovuti ya wakatoliki – Wakristo 44%, Waislamu 34%
Kalenda Ofisi ya Serikali – Wakristo ,Waislamu
Tovuti ya Mambo ya Nje Marekani – Wakristo 62%, Waislamu 32%
Pili, viongozi wa Kikristo wamekuwa msitari wa mbele kupinga kutiwa
kipengele cha dini katika dodoso la sensa. Katika mazingira ya takwimu
tata ambazo hata Mkurugenzi wa idara ya takwimu anakiri kwamba si
takwimu sahihi ombi letu la kuwekwa kipengele cha dini katika dodoso la
sensa lingepokelewa kama ufumbuzi wa utata huo ili tuwe na takwimu
sahihi za idadi ya watanzania kwa dini zao lakini serikali imekataa kata
kata na inaunga mkono msimamo wa wakristo kutokuwekwa kipengele
cha dini katika dodoso la sensa, wakristo ambao tayari wanadai wao
wako wengi kuliko waislamu.
Tatu, dodoso la sensa limeandaliwa kuja kunufaisha wakristo kwa sababu
linauliza kuhusu idadi ya makanisa na misikiti wakati serikali imekataa
kuhusisha sensa na dini. Tuna shaka kwamba huu ni mpango wa
kuwawezesha wakristo kuchakachua takwimu hizo za majumba ya ibada
kuthibitisha kwamba wao ni wengi kuliko waislamu kama ambavyo tayari
wanadai.
Izingatiwe kwamba idadi ya makanisa itakuwa kubwa kuliko misikiti
kutokana na tofauti za kimadhehebu za wakristo hata pale ambapo wao
si wengi kwani katika Ukristo waumini wa dhehebu moja hawawezi
kufanya ibada katika Kanisa lisilo la dhehebu lao. Katika kijiji utakuta
makanisa manne mpaka matano au zaidi lakini msikiti ni mmoja tu
kutokana na ukweli kwamba waislamu huswali msikiti wowote hivyo
hawawezi kuwa na misikiti mingi kama makanisa.
Nimewaelewa na ninakubaliana nanyi Bw.Achahasira na Mandown ila sidhani kama ni jambo jema kususia sensa tukumbuke hao wakristo ni makafiri ambao malipo yao ni hapa hapa duniani si vyema kubishana na makafiri kwa kuwa tunapoteza muda na nguvu ambazo tungezitumia kuimarisha uislamu.