Nampendamilele
JF-Expert Member
- Jun 12, 2024
- 427
- 653
Za siku nyingi humu ndani.. hope mko poa
Najua humu kuna wakongwe wa mahusiano naweza kupata kujua mawili matatu juu ya haya mahusiano
Nipo na mwanaume sasa ni miezi 6 ya mahusiano… nampenda kwa upande wangu na yeye anaonesha kunipenda japo yeye anajua moyoni mwake..
Ni mwanaume mzuri ananijali na tunaishi vizuri kwakweli nisiwe muongo… mimi nina kazi na yeye ana kazi yake, amenizidi miaka 7
Ila kama unavojua kuna muda unafika unahitaji kupata mtu wa kutulia nae na kufanya maisha.. nafikiri wengi mnafahamu wanawake wengi ndoto yao kubwa ni kuwa na familia yaani ndoa( japo wengi watajifanya hawaitaji ndoa kwamba sio kitu cha lazima UONGA) kila mtu anahitaji familia ni vile tu unakuta mdada anakosa mtu anaemtaka wa kumuoa ndio anabaki kupondea ndoa
Sasa ni hivi mimi huyu kijana sifahamu mahali anapoishi na nimejaribu kumwambia hata akanioneshe wapi anaishi amekuwa akinipiga kalenda.. hili sio shida sana labda kwasababu mahusiano bado machanga
Kitu kilichofanya niadike huu uzi ni namna tunavyoendesha haya mahusiano.. ni mtu ambae hataki kuniaminisha chochote yaani hata ile kuonesha kwamba tuna future hapana yupo kimya
Nimewahi kumuuliza hatima ya mahusiano yetu ni nini?? Ananijibu kuwa ni swali gumu ila yeye kwa sasa bado hajawa tayari kuwa serious labda siku za mbeleni
Anasema tu kuwa tuendelee kuwa na mahusiano tutaona mbeleni kama Mungu amepanga sisi tuwe pamoja tutaoana
Wakuu hiyo hali inaniwazisha sana nashindwa nini cha kuamua.. nashindwa kumuweka upande gani.. mtu umeamua kumpenda halafu yeye kumbe hayuko serious
Ambacho nina kiwaza kichwani wangu nimtoe kwenye ile nafasi ambayo nimemuweka nimrudishe chini kabisa nijiandae kwa lolote
Naomba mwenye kuelewa haya mambo anipe ushauri
Najua humu kuna wakongwe wa mahusiano naweza kupata kujua mawili matatu juu ya haya mahusiano
Nipo na mwanaume sasa ni miezi 6 ya mahusiano… nampenda kwa upande wangu na yeye anaonesha kunipenda japo yeye anajua moyoni mwake..
Ni mwanaume mzuri ananijali na tunaishi vizuri kwakweli nisiwe muongo… mimi nina kazi na yeye ana kazi yake, amenizidi miaka 7
Ila kama unavojua kuna muda unafika unahitaji kupata mtu wa kutulia nae na kufanya maisha.. nafikiri wengi mnafahamu wanawake wengi ndoto yao kubwa ni kuwa na familia yaani ndoa( japo wengi watajifanya hawaitaji ndoa kwamba sio kitu cha lazima UONGA) kila mtu anahitaji familia ni vile tu unakuta mdada anakosa mtu anaemtaka wa kumuoa ndio anabaki kupondea ndoa
Sasa ni hivi mimi huyu kijana sifahamu mahali anapoishi na nimejaribu kumwambia hata akanioneshe wapi anaishi amekuwa akinipiga kalenda.. hili sio shida sana labda kwasababu mahusiano bado machanga
Kitu kilichofanya niadike huu uzi ni namna tunavyoendesha haya mahusiano.. ni mtu ambae hataki kuniaminisha chochote yaani hata ile kuonesha kwamba tuna future hapana yupo kimya
Nimewahi kumuuliza hatima ya mahusiano yetu ni nini?? Ananijibu kuwa ni swali gumu ila yeye kwa sasa bado hajawa tayari kuwa serious labda siku za mbeleni
Anasema tu kuwa tuendelee kuwa na mahusiano tutaona mbeleni kama Mungu amepanga sisi tuwe pamoja tutaoana
Wakuu hiyo hali inaniwazisha sana nashindwa nini cha kuamua.. nashindwa kumuweka upande gani.. mtu umeamua kumpenda halafu yeye kumbe hayuko serious
Ambacho nina kiwaza kichwani wangu nimtoe kwenye ile nafasi ambayo nimemuweka nimrudishe chini kabisa nijiandae kwa lolote
Naomba mwenye kuelewa haya mambo anipe ushauri