Hapa kuna upendo au natumika nifungueni macho

Hapa kuna upendo au natumika nifungueni macho

Nampendamilele

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2024
Posts
427
Reaction score
653
Za siku nyingi humu ndani.. hope mko poa

Najua humu kuna wakongwe wa mahusiano naweza kupata kujua mawili matatu juu ya haya mahusiano

Nipo na mwanaume sasa ni miezi 6 ya mahusiano… nampenda kwa upande wangu na yeye anaonesha kunipenda japo yeye anajua moyoni mwake..

Ni mwanaume mzuri ananijali na tunaishi vizuri kwakweli nisiwe muongo… mimi nina kazi na yeye ana kazi yake, amenizidi miaka 7

Ila kama unavojua kuna muda unafika unahitaji kupata mtu wa kutulia nae na kufanya maisha.. nafikiri wengi mnafahamu wanawake wengi ndoto yao kubwa ni kuwa na familia yaani ndoa( japo wengi watajifanya hawaitaji ndoa kwamba sio kitu cha lazima UONGA) kila mtu anahitaji familia ni vile tu unakuta mdada anakosa mtu anaemtaka wa kumuoa ndio anabaki kupondea ndoa

Sasa ni hivi mimi huyu kijana sifahamu mahali anapoishi na nimejaribu kumwambia hata akanioneshe wapi anaishi amekuwa akinipiga kalenda.. hili sio shida sana labda kwasababu mahusiano bado machanga

Kitu kilichofanya niadike huu uzi ni namna tunavyoendesha haya mahusiano.. ni mtu ambae hataki kuniaminisha chochote yaani hata ile kuonesha kwamba tuna future hapana yupo kimya

Nimewahi kumuuliza hatima ya mahusiano yetu ni nini?? Ananijibu kuwa ni swali gumu ila yeye kwa sasa bado hajawa tayari kuwa serious labda siku za mbeleni
Anasema tu kuwa tuendelee kuwa na mahusiano tutaona mbeleni kama Mungu amepanga sisi tuwe pamoja tutaoana

Wakuu hiyo hali inaniwazisha sana nashindwa nini cha kuamua.. nashindwa kumuweka upande gani.. mtu umeamua kumpenda halafu yeye kumbe hayuko serious

Ambacho nina kiwaza kichwani wangu nimtoe kwenye ile nafasi ambayo nimemuweka nimrudishe chini kabisa nijiandae kwa lolote

Naomba mwenye kuelewa haya mambo anipe ushauri
 
Kwa maelezo ulio yatoa uzoefu wangu unaonyesha kwamba...

Wewe unampenda sana huyo mwanaume, na unatumia moyo badala ya kutumia akili kufanya maamuzi.
Mwisho niseme tu kwamba...

Huyo mwanaume hana upendo wa dhati kwako, na hana mpango wa kukuoa wala hatokuja kufanya maisha na wewe.

Itoshe kusema kwamba.... wewe sio mwanamke wa ndoto yake.
 
Za siku nyingi humu ndani.. hope mko poa

Najua humu kuna wakongwe wa mahusiano naweza kupata kujua mawili matatu juu ya haya mahusiano

Nipo na mwanaume sasa ni miezi 6 ya mahusiano… nampenda kwa upande wangu na yeye anaonesha kunipenda japo yeye anajua moyoni mwake..

Ni mwanaume mzuri ananijali na tunaishi vizuri kwakweli nisiwe muongo… mimi nina kazi na yeye ana kazi yake, amenizidi miaka 7

Ila kama unavojua kuna muda unafika unahitaji kupata mtu wa kutulia nae na kufanya maisha.. nafikiri wengi mnafahamu wanawake wengi ndoto yao kubwa ni kuwa na familia yaani ndoa( japo wengi watajifanya hawaitaji ndoa kwamba sio kitu cha lazima UONGA) kila mtu anahitaji familia ni vile tu unakuta mdada anakosa mtu anaemtaka wa kumuoa ndio anabaki kupondea ndoa

Sasa ni hivi mimi huyu kijana sifahamu mahali anapoishi na nimejaribu kumwambia hata akanioneshe wapi anaishi amekuwa akinipiga kalenda.. hili sio shida sana labda kwasababu mahusiano bado machanga

Kitu kilichofanya niadike huu uzi ni namna tunavyoendesha haya mahusiano.. ni mtu ambae hataki kuniaminisha chochote yaani hata ile kuonesha kwamba tuna future hapana yupo kimya

Nimewahi kumuuliza hatima ya mahusiano yetu ni nini?? Ananijibu kuwa ni swali gumu ila yeye kwa sasa bado hajawa tayari kuwa serious labda siku za mbeleni
Anasema tu kuwa tuendelee kuwa na mahusiano tutaona mbeleni kama Mungu amepanga sisi tuwe pamoja tutaoana

Wakuu hiyo hali inaniwazisha sana nashindwa nini cha kuamua.. nashindwa kumuweka upande gani.. mtu umeamua kumpenda halafu yeye kumbe hayuko serious

Ambacho nina kiwaza kichwani wangu nimtoe kwenye ile nafasi ambayo nimemuweka nimrudishe chini kabisa nijiandae kwa lolote

Naomba mwenye kuelewa haya mambo anipe ushauri
KWANI AMESHAPIGA?
 
Miezi sita hujui kwake hii ni taa nyekundu tayari kwako anaweza akawa mme wa mtu au anakutumia tu anza kuchukua hatua ikiwemo kutaka kujua kwake na angalau ata ndugu yake mmoja umjue
inanipa mawazo hiyo japo ananipa airtime sana ila nyie wanaume wajanja sana ukute anaongeleaga chooni
 
Njoo kwangu tufanye malengo ya maishaa maana huyo ameshakuonyesha rangi nyekundu Bado sijapata mwanamke mwenye malengo ya maisha
 
Back
Top Bottom