Halima Bulembo: Bunge si lazima kuonekana live

Halima Bulembo: Bunge si lazima kuonekana live

Huyu binti naye uwezo wake wa kufikiri ndio umefikia hapo.
 
Je wananchi watapimaje kwamba mbuge wao hakuwasemea kero zao wakati wamenyimwa haki ya kumwangalia anavyoyasema? uoni itakua ngumu kwa mwananchi kumwajibisha mbunge kwenye sanduku la kura iwapo atajitetea kua amefanya kazi yake lakini serikali ndo hawakuwajibika?
Kwani wabunge wameanza kuchaguliwa mwaka huu? Kuanzia Uhuru tulikuwa na Bunge na wabunge walikuwa wanaibana serikali bila hata ya wananchi kujua kinachoendelea huko bungeni!
 
Je wananchi watapimaje kwamba mbuge wao hakuwasemea kero zao wakati wamenyimwa haki ya kumwangalia anavyoyasema? uoni itakua ngumu kwa mwananchi kumwajibisha mbunge kwenye sanduku la kura iwapo atajitetea kua amefanya kazi yake lakini serikali ndo hawakuwajibika?
Kwani wabunge wameanza kuchaguliwa mwaka huu? Kuanzia Uhuru tulikuwa na Bunge na wabunge walikuwa wanaibana serikali bila hata ya wananchi kujua kinachoendelea huko bungeni!
Ndio nyie lumumba mnajulikana kwa kupindisha na kulisha watu maneno
Mimi siyo Lumumba! Ni Mtanzania huru ambaye sifuati mkumbo kama nyumbu na kuzungusha mikono kujitoa akili!
 
Siyo yeye tu wabunge wengi humu bungeni ni mizigo hasa hawa wa kuteuliwa, wanakwenda kulinda maslahi yao peke yao na ya waliowachagua. Hii si kwa CCM tu hata upinzani ndiyo maana kwa hili nampenda Zitto kabwe maana yeye hajali kuitwa msaliti pale anapoona kuna ukweli lakini watu walioelimika kama kina Tundu Lisu nao wananaswa katika mtego kama huu hata wale wa CCM walioelimika wanakisemea chama chao CCM bila kujali kama ni kwa manufaa ya umma ama manufaa ya CCM na kundi la majambazi. Demokrasia tanzani ni ya ujanja ujanja tu. Taabu sana ndiyo maana wakati mwingine nashangaa hata sisi wananchi tunaingia katika mkenge wa vyama vyetu ku support kila ujinga ili mradi unatoka katika midomo ya watu wenye itikadi moja na sisi utadhani ni lazima kuunga kila neno analosema Magufuli ama Mbowe tunajisahau kuwa sisi ndiyo mabosi wao hao wanasiasa.
mkuu, ulichoandika hapo ndio siasa zilizovyo. ili kuwa mwanasiasa mzuri ni lazima uwe mnafiki ama ndumi la kuwili. sisi kazi zetu hizi hazinaga siasa that's i love this job of mine.
 
kasome civics utajua kazi za mbunge, kazi ya mbunge ni kuongea kuishauri serikali na kutunga sheria hayo mengine ziada!

inaonyesha kama uko serious au unatania kuwa hujui kazi za wqbunge ni nini, kama kazi zao ni kuongea basi TV ndio inawahusu zaidi, kasome tena civics kama hikuelewa!
Kwani wabunge waliochaguliwa kuanzia uhuru kabla ya Bunge kurushwa "live" walikuwa hawaongei humo bungeni na wananchi walikuwa hawaridhiki kwa vile hawaonekani?
 
Mimi nina shida sana na wabunge wa aina hii, wabunge wasiofahamu taratibu wala sheria. Wabunge wasiokuwa na hoja za nguvu badala yake wanaishia kujadili watu. Hakuna sehemu serikali inaposema Bunge lisirushwe live.Serikali imesema uwezo wa kituo cha TBC kurusha Bunge live muda wote haupo, hivyo litarusha mambo kadhaa live na mengine yatarushwa jioni/usiku yakiwa yamerekodiwa. Kitengo cha Mawasiliano katika Ofisi ya Bunge itakuwa iko live muda wote kupitia feed yake maalum ambapo kituo chochote chenye kutaka kurusha matangazo live kitarusha na tayari wameshatoa hizo frequency zao. Wabunge wa namna hii bila kujali wanatoka chama gani waelimishwe na waambiwe jambogani wanalotakiwa kulifanya bungeni. Kama walipewa ubunge kwa hisani basi waliowatunuku angalau wawape darasa wajue kule sio sehemu ya kutafutia wachumba
 
Huyu naye ni jipu! Tunaomba JPM uangalie pia haya majipu mbuzi...!
 
Kwani wabunge wameanza kuchaguliwa mwaka huu? Kuanzia Uhuru tulikuwa na Bunge na wabunge walikuwa wanaibana serikali bila hata ya wananchi kujua kinachoendelea huko bungeni!
Tanganyika na baadae Tz bara hapakuwa na tv. Ndio unapenda turudi huko, ili muendelee kuwapumbaza wa Tz. Hao Waheshimiwa mabinti wanaoletwa na Baba au washikaji tutauonea wapi uwezo wao?
 
Elimu na uelewa wa kupambanua mambo ni tofauti kabisa. Anaelimu lakini pengine hawezi au ndio mtizamo wake
sijui kama anaelewa mantiki ya bunge laivu. anaona upande wa wabunge badala kufikiria haki ya wananchi kupata habari!
 
sijui kama anaelewa mantiki ya bunge laivu. anaona upande wa wabunge badala kufikiria haki ya wananchi kupata habari!
Ndio kundi la hata sehemu kubwa ya wabunge wa lumumba wanavyolichukulia swala hili.
 
Yule binti wa miaka 16 aliyehutubia UN ni bora kuliko huyu.
 
Kwani wabunge waliochaguliwa kuanzia uhuru kabla ya Bunge kurushwa "live" walikuwa hawaongei humo bungeni na wananchi walikuwa hawaridhiki kwa vile hawaonekani?
una umli gani wewe? naona kioja si hoja hapa!

miaka ya zamani wanafunzi tuu walikuwa wanaenda shule bila viatu! simu za kuloroga, barua za SLP nk unaelewa umeandika nini hapo?

Enzi hizoo unatamani na wewe? hiyo TV alikuwa nayo Juliasi pekeyake! chama kilikuwa kimoja, ubishi ulikuwa hauruhusiwi hivi unaelewa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom