Mtondoli
Member
- Nov 9, 2021
- 70
- 174
Ndugu zangu habarini, kuna kitu kinanisononesha Sana katika vipaumbele vya serikali ili kumletea mwananchi maendeleo, naona vipaumbele vikuu ni miundombinu ambayo mwisho wa siku huwezi kuigeuza kuwa chakula, hatuwezi kula daraja la Salenda, wala hatuwezi kula ndege zilizoagizwa na zilizonunuliwa, wananchi hawawezi kuzigeuza kuwa ugali au kitoweo nafikiri ni anasa tu.
Inanisikitisha Kama tuna pesa ya kununua ndege cash lakini hatuna pesa ya kuagiza mbolea ili kusaidia kilimo Cha nchi hii, waziri mkuu anasema wananchi wanaoingiza mbolea kutoka nchi jirani wasizuiwe swali ni je hizo nchi jirani zinatoa wapi hiyo mbolea,,tuacheni utani huu ni msimu wa kilimo unaoweza kuwa mbaya zaidi kuwahi kutokea Jana nilikuwa rukwa wilaya ya kwela mbolea ni 140,000 tafakari
Inanisikitisha Kama tuna pesa ya kununua ndege cash lakini hatuna pesa ya kuagiza mbolea ili kusaidia kilimo Cha nchi hii, waziri mkuu anasema wananchi wanaoingiza mbolea kutoka nchi jirani wasizuiwe swali ni je hizo nchi jirani zinatoa wapi hiyo mbolea,,tuacheni utani huu ni msimu wa kilimo unaoweza kuwa mbaya zaidi kuwahi kutokea Jana nilikuwa rukwa wilaya ya kwela mbolea ni 140,000 tafakari