Sijui wengine wanaona kile kile ninachokiona mimi. Kama ni hivyo basi inatisha kwa kuwa sijawahi kuona hali hii ikijiri katika nchi yetu pendwa tangu ninakuwa mtu mzima miaka ile ya 1960s'. Katika historia ya taifa letu siku zote watanzania tumekuwa tunaunganika katika masuala yenye maslahi ya taifa. Lakini katika miaka ya hivi karibuni tunaanza kuona baadhi ya watu wakifurahia pale nchi yetu inapokuwa imeshikwa pabaya. Kwa mfano hivi sasa kuna hili suala la ndege yetu kuzuiliwa huko Afrika Kusini. Kuna watu wanashangilia. Kuna watu walishangilia pale IMF ilipotoa takwimu zake kuhusu kukua kwa uchumi kwa kuonyesha ukuaji wa 5% tofauti na takwimu za serikali zilizoonyesha ukuaji wa 7.1%. Hata kwenye mashindano ya Afcon yaliyoisha hivi karibuni huo Cairo kuna watu walioshangilia pale tulivyofungwa na Kenya! Kwa ufupi chochote kile kinachoonyesha Tanzania inafanya vibaya kinafanya baadhi ya watu wafanye sherehe. Kwa hakika hali hii haipendezi. Nini kimetokea hadi tukafika mahali watu wanafurahi nchi yao ikishikwa pabaya? Tutafakari na tufanye kile Waingereza wanasema "soul searching". Haipendezi tukiendelea hivi kama taifa.
Katika Fizikia, moja ya sheria za msingi kabisa ya ulimwengu ni "The Second Law of Thermodynamics".
Mwanasayansi maarufu wa Uingereza, Sir Arthur Eddington, ananukuliwa akisema, cheza na sheria zote za Fizikia, lakini ukiona majaribio yako yanapingana na The Second Law of Thermodynamics, fanyia kazi upya majaribio yako.
Hii sheria inasemaje?
Kifupi, kwa lugha isiyo ya kitaalamu sana, sheria hii inasema kwamba, kadiri muda unavyozidi kwenda mbele, katika closed systems zozote, mambo kwa kawaida huwa yanatoka kuwa simple kwenda complicated, entropy inaongezeka. Yani hata ukisema ufunge mlango wa chumba ukiache kiwe kisafi, ukakaa miaka miwili, utakuta chumba kina vumbi, kinahitaji kufagiliwa ili kiwe kisafi. Unaweza kukuta utando wa buibui.
Kwa hivyo, ili kukifanya chumba kiwe kisafi, inabidi kazi ifanyike kila mara kukisafisha. Ukisema tu "nilifagia wiki iliyopita, chumba changu safi" wakati watu wanaingia na kutoka, utajikuta una chumba kichafu.
Kwa nini naongelea "The Second Law of Thermodynamics" na habari za entropy na usafi wa chumba hapa?
Tuna tatizo la kufikiri kwamba kazi ya kujenga umoja wa kitaifa ilishamalizwa enzi za Nyerere. Sisi ni wamoja.
Nyerere mwenyewe katika uhai wake mwishoni alilalamikia kuchipuka kwa ukabila, akielewa kwamba kazi aliyoanza haikuisha. Na kwa kweli kazi hii haiishi. Ni sawa na kazi ya kufagia chumba niliyosema awali hapo. Ni kazi endelevu kizazi hata kizazi. Ukifikiri umemaliza hapo hapo ulichojenga kinaanza kuanguka.
Sasa basi, katika muktadha huu, watu wanapoona viongozi hawaishi kama wananchi wengine, wanapoona upendeleo, wanapoona hakuna ushirikishwaji umma katika maamuzi, wanaona hizi habari za umoja wa kitaifa ni ujinga. Wanaona sisi ni watumwa katika nchi yetu wenyewe, tunawatumikia mabwana wachache wanaofaidi matunda ya nchi hii kivulini, wakati sisi tunapigwa na jua.
Wengine wakiumwa wanapelekwa Ulaya, India na South Africa. Wengine hata hospitali za Wilaya hawamudu matibabu.
Sasa katika mfumo huu, utategemea vipi umoja wa kitaifa na uzalendo?