mafutamingi
JF-Expert Member
- Feb 14, 2011
- 2,772
- 2,171
Sijui wengine wanaona kile kile ninachokiona mimi. Kama ni hivyo basi inatisha kwa kuwa sijawahi kuona hali hii ikijiri katika nchi yetu pendwa tangu ninakuwa mtu mzima miaka ile ya 1960s'.
Katika historia ya taifa letu siku zote watanzania tumekuwa tunaunganika katika masuala yenye maslahi ya taifa. Lakini katika miaka ya hivi karibuni tunaanza kuona baadhi ya watu wakifurahia pale nchi yetu inapokuwa imeshikwa pabaya.
Kwa mfano hivi sasa kuna hili suala la ndege yetu kuzuiliwa huko Afrika Kusini. Kuna watu wanashangilia. Kuna watu walishangilia pale IMF ilipotoa takwimu zake kuhusu kukua kwa uchumi kwa kuonyesha ukuaji wa 5% tofauti na takwimu za serikali zilizoonyesha ukuaji wa 7.1%.
Hata kwenye mashindano ya Afcon yaliyoisha hivi karibuni huo Cairo kuna watu walioshangilia pale tulivyofungwa na Kenya!
Kwa ufupi chochote kile kinachoonyesha Tanzania inafanya vibaya kinafanya baadhi ya watu wafanye sherehe. Kwa hakika hali hii haipendezi.
Nini kimetokea hadi tukafika mahali watu wanafurahi nchi yao ikishikwa pabaya? Tutafakari na tufanye kile Waingereza wanasema "soul searching". Haipendezi tukiendelea hivi kama taifa.
Katika historia ya taifa letu siku zote watanzania tumekuwa tunaunganika katika masuala yenye maslahi ya taifa. Lakini katika miaka ya hivi karibuni tunaanza kuona baadhi ya watu wakifurahia pale nchi yetu inapokuwa imeshikwa pabaya.
Kwa mfano hivi sasa kuna hili suala la ndege yetu kuzuiliwa huko Afrika Kusini. Kuna watu wanashangilia. Kuna watu walishangilia pale IMF ilipotoa takwimu zake kuhusu kukua kwa uchumi kwa kuonyesha ukuaji wa 5% tofauti na takwimu za serikali zilizoonyesha ukuaji wa 7.1%.
Hata kwenye mashindano ya Afcon yaliyoisha hivi karibuni huo Cairo kuna watu walioshangilia pale tulivyofungwa na Kenya!
Kwa ufupi chochote kile kinachoonyesha Tanzania inafanya vibaya kinafanya baadhi ya watu wafanye sherehe. Kwa hakika hali hii haipendezi.
Nini kimetokea hadi tukafika mahali watu wanafurahi nchi yao ikishikwa pabaya? Tutafakari na tufanye kile Waingereza wanasema "soul searching". Haipendezi tukiendelea hivi kama taifa.