Hali halisi ya umeme ilivyo Nigeria inatisha sana,by #shany!

Hali halisi ya umeme ilivyo Nigeria inatisha sana,by #shany!

Crocodiletooth

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2012
Posts
22,433
Reaction score
26,986
#Shany ni mtanzania anayeishi nigeria kwa miaka mingi kidogo,anatunyetisha hali ilivyo na uhalisia wake!,
#Wale wa upande wapi wajionee na wajiulize,jinsi serekali yetu tukufu inavyo wapenda watanzania kwa kila sekta,japo kwa umahamuma wao hupuuza na kujiona wao ndiyo wana akili nzuri na wapo sahihi zaidi kwa rasilimali tulizonazo,
Wenzetu wana mafuta kabisa!,na wameshafanya mapinduzi ya kiserekali mara kadhaa lakini hakuna lolote,let question our self are we right?,au ni uchu tu wa makenge maji,
Code:
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

NIGERIA HAKUNA UMEME, NAJIVUNIA TANZANIA 🇹🇿💃

Ngojeni niwape ka-umbea kidogo leo 😁 Kama hamkujua basi leo mjue… si mnanijua Mama Mally siwezi kukosa story za hawa viumbe 😂

Umeme huku Nigeria ni wa mgao, ila kwa ukweli kabisa unaweza kusema hakuna umeme. Imagine NEPA wakikata umeme leo, wanaweza kurudisha wiki ijayo, mwezi ujao au hata baada ya miezi kadhaa 😭 Kuna wakati nguzo ikiharibika mtaa mzima unakaa miezi sita gizani 😳 Everywhere kimya, ni sauti za majenereta tu zinanguruma mchana na usiku 😭🤣

Sasa kwangu mimi nyumba ipo karibu kabisa na barabara. Nje nina fremu 6 — tano zina wapangaji.
Mmoja kinyozi, mwingine msusi, mwingine fundi nguo, mwingine anauza vifaa vya P.O.P vya ujenzi. Huyu wa P.O.P yeye hata generator haihitaji sana 😁

Lakini kinyozi akipata mteja lazima awashe generator.
Msusi akitaka kuosha nywele, kukausha au kufanya weaving lazima awashe.
Fundi nguo akimaliza kushona naye awashe pasi 😭

Halafu bado mimi huku ndani nikitaka kupampu maji lazima niwashe generator pia 😭
Sasa magari yanapita nje nonstop, humo humo majenereta yanaunguruma… maskio yatabaki salama kweli? 😭🤣

Huku wananchi tumeshazoea maisha ya generator. Lazima ununue mafuta angalau lita mbili kila siku. Mimi nina majenereta mawili:

Moja kubwa — hili ukiwasha unaweza kutumia fridge, kupampu maji na vitu vizito. Nikimaliza kujaza maji nalizima.

Halafu nahamia hili dogo wanaliita “economic generator” 😭🤣
Hili ni la budget kabisa. Ukiwasha unatumia feni, kuchaji simu, taa na blender.

Sasa mafuta lita mbili ukianza kuwasha saa mbili usiku, kufika saa kumi alfajiri generator inazima yenyewe 😭 mafuta yameisha… enjoyment done finish 😂💔

Wanigeria wengi washazoea hali hii kiasi kwamba siku umeme ukiwa stable kila mtu anafurahi kama ameshinda bahati nasibu 😭 Utamsikia mtu anasema:
“And so e suppose be!”
(Yaani: “Hivi ndivyo inavyotakiwa kuwa.”) 😂

Mfano tu wiki iliyopita NEPA wamekuwa wanatupatia umeme kuanzia saa 12 jioni hadi saa 4 usiku, halafu wanakata. Unarudi tena saa 10 alfajiri hadi saa moja asubuhi, then basi tena 😭

Jana nilipopost video watu wengi waliniuliza kuhusu solar.
Wakuu, huku solar ndiyo mpango mzima sasa hivi 😭 Ukiweza ku-afford unafunga tu maisha yaendelee.

Mfumo mdogo wa biashara wenye fridge unaweza kufika mpaka milioni 1.5 za Kitanzania.

Lakini mimi jana nimefunga solar ya nyumba nzima 😭💃
Tukapitisha waya hadi kwenye fremu zote za nje.

Hii solar inapampu maji, tutawasha fridge za ndani, na hata wine shop yangu itatumia fridge bila stress 😭💃 Wapangaji wote wa fremu watatumia pia.

Kwa jumla tumetumia kama milioni 6.5 za Kitanzania 😭 lakini sasa:

✅ NEPA bye bye 👋
✅ Hakuna bili za umeme tena
✅ Hakuna mafuta ya generator tena
✅ Hakuna kelele za majenereta tena 😭💃

Tanzania nyumbani habari 👋🇹🇿

#shanystoryteller #truestory #viralpost
 
Ndiyo nchi inadaiwa kuwa na wasomi wengi kupindukia nadhani ni wasomi maneno mingi,aka jamii ya lissu 😃
 
Ndiyo nchi inadaiwa kuwa na wasomi wengi kupindukia nadhani ni wasomi maneno mingi,aka jamii ya lissu 😃
Wasomi wengi wasio na ajira,ushirika na NEPA wala serikali ndiyo unataka waizalishie Nigeria umeme?Ulinganisho wako ni batili na hauna mashiko.Lakini,kama unampenda sana Lissu unaruhusiwa kumuhusisha na kila kinachokukera.
 
Yaani mnakosa usingizi kukokotoa matatizo ya nchi za watu ili kuhalalisha wizi,utekaji na mauaji mnayoyafanya hapa! Mbona usiseme Norway haina rasilimali nyingi kama sisi ila ni tajiri na salama kuliko sisi? Yaani nyie mnatugeuzia nyuso zetu kwenye nchi za kijinga ili ku justify ujinga wenu? Hatutakubali
 
Nigeria 🇳🇬 hi au ilolo mbey
Nigeria yenye wasomi wengi jamii ya lissu,maneno mengi ya matumaini,wamwsha pindua taifa lao mara chungu mzima lakini hali iliyopo ndiyo hali gani sasa?
--kila anayepindua nigeria anajitajirisha and then anakaa pembeni kimyaaa 🤪🤪
 
Yaani mnakosa usingizi kukokotoa matatizo ya nchi za watu ili kuhalalisha wizi,utekaji na mauaji mnayoyafanya hapa! Mbona usiseme Norway haina rasilimali nyingi kama sisi ila ni tajiri na salama kuliko sisi? Yaani nyie mnatugeuzia nyuso zetu kwenye nchi za kijinga ili ku justify ujinga wenu? Hatutakubali
Ndiyo utajua mwisho wao kufikiria ni urefu wa pua zao.Kwamba Tanzania iridhike na shida zake kwa sababu Nigeria wanatumia umeme wa vijenereta!Mmmmmffff!
 
Nigeria yenye wasomi wengi jamii ya lissu,maneno mengi ya matumaini,wamwsha pindua taifa lao mara chungu mzima lakini hali iliyopo ndiyo hali gani sasa?
--kila anayepindua nigeria anajitajirisha and then anakaa pembeni kimyaaa 🤪🤪
Hata wewe ungewashauri Bashite na wabunge wenzake wapuuzi waachane na safari ya kwenda kuishangilia Serengeti boys na wabaki bungeni wajadili mambo ya maendeleo kwa nchi.
 
#Shany ni mtanzania anayeishi nigeria kwa miaka mingi kidogo,anatunyetisha hali ilivyo na uhalisia wake!,
#Wale wa upande wapi wajionee na wajiulize,jinsi serekali yetu tukufu inavyo wapenda watanzania kwa kila sekta,japo kwa umahamuma wao hupuuza na kujiona wao ndiyo wana akili nzuri na wapo sahihi zaidi kwa rasilimali tulizonazo,
Wenzetu wana mafuta kabisa!,na wameshafanya mapinduzi ya kiserekali mara kadhaa lakini hakuna lolote,let question our self are we right?,au ni uchu tu wa makenge maji,
Code:
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

NIGERIA HAKUNA UMEME, NAJIVUNIA TANZANIA 🇹🇿💃

Ngojeni niwape ka-umbea kidogo leo 😁 Kama hamkujua basi leo mjue… si mnanijua Mama Mally siwezi kukosa story za hawa viumbe 😂

Umeme huku Nigeria ni wa mgao, ila kwa ukweli kabisa unaweza kusema hakuna umeme. Imagine NEPA wakikata umeme leo, wanaweza kurudisha wiki ijayo, mwezi ujao au hata baada ya miezi kadhaa 😭 Kuna wakati nguzo ikiharibika mtaa mzima unakaa miezi sita gizani 😳 Everywhere kimya, ni sauti za majenereta tu zinanguruma mchana na usiku 😭🤣

Sasa kwangu mimi nyumba ipo karibu kabisa na barabara. Nje nina fremu 6 — tano zina wapangaji.
Mmoja kinyozi, mwingine msusi, mwingine fundi nguo, mwingine anauza vifaa vya P.O.P vya ujenzi. Huyu wa P.O.P yeye hata generator haihitaji sana 😁

Lakini kinyozi akipata mteja lazima awashe generator.
Msusi akitaka kuosha nywele, kukausha au kufanya weaving lazima awashe.
Fundi nguo akimaliza kushona naye awashe pasi 😭

Halafu bado mimi huku ndani nikitaka kupampu maji lazima niwashe generator pia 😭
Sasa magari yanapita nje nonstop, humo humo majenereta yanaunguruma… maskio yatabaki salama kweli? 😭🤣

Huku wananchi tumeshazoea maisha ya generator. Lazima ununue mafuta angalau lita mbili kila siku. Mimi nina majenereta mawili:

Moja kubwa — hili ukiwasha unaweza kutumia fridge, kupampu maji na vitu vizito. Nikimaliza kujaza maji nalizima.

Halafu nahamia hili dogo wanaliita “economic generator” 😭🤣
Hili ni la budget kabisa. Ukiwasha unatumia feni, kuchaji simu, taa na blender.

Sasa mafuta lita mbili ukianza kuwasha saa mbili usiku, kufika saa kumi alfajiri generator inazima yenyewe 😭 mafuta yameisha… enjoyment done finish 😂💔

Wanigeria wengi washazoea hali hii kiasi kwamba siku umeme ukiwa stable kila mtu anafurahi kama ameshinda bahati nasibu 😭 Utamsikia mtu anasema:
“And so e suppose be!”
(Yaani: “Hivi ndivyo inavyotakiwa kuwa.”) 😂

Mfano tu wiki iliyopita NEPA wamekuwa wanatupatia umeme kuanzia saa 12 jioni hadi saa 4 usiku, halafu wanakata. Unarudi tena saa 10 alfajiri hadi saa moja asubuhi, then basi tena 😭

Jana nilipopost video watu wengi waliniuliza kuhusu solar.
Wakuu, huku solar ndiyo mpango mzima sasa hivi 😭 Ukiweza ku-afford unafunga tu maisha yaendelee.

Mfumo mdogo wa biashara wenye fridge unaweza kufika mpaka milioni 1.5 za Kitanzania.

Lakini mimi jana nimefunga solar ya nyumba nzima 😭💃
Tukapitisha waya hadi kwenye fremu zote za nje.

Hii solar inapampu maji, tutawasha fridge za ndani, na hata wine shop yangu itatumia fridge bila stress 😭💃 Wapangaji wote wa fremu watatumia pia.

Kwa jumla tumetumia kama milioni 6.5 za Kitanzania 😭 lakini sasa:

✅ NEPA bye bye 👋
✅ Hakuna bili za umeme tena
✅ Hakuna mafuta ya generator tena
✅ Hakuna kelele za majenereta tena 😭💃

Tanzania nyumbani habari 👋🇹🇿

#shanystoryteller #truestory #viralpost
una undugu na kidukulilo? au wewe ni muhaya?
 
Hata wewe ungewashauri Bashite na wabunge wenzake wapuuzi waachane na safari ya kwenda kuishangilia Serengeti boys na wabaki bungeni wajadili mambo ya maendeleo kwa nchi.
Akili za lissu hizi,!?
Katika taifa ni lazima kila kitu kiende kwa mpangilio wake,michezo iendelee,barabara zijengwe,wanafunzi waende shule,na wajawazito wajifungue 😃😃😃
 
Akili za lissu hizi,!?
Katika taifa ni lazima kila kitu kiende kwa mpangilio wake,michezo iendelee,barabara zijengwe,wanafunzi waende shule,na wajawazito wajifungue 😃😃😃
Na hizi ulizotumia ndizo hasa tabia na umburula wa wana-CCM mlivyo kiuhalisia wenu.Hamna vipaumbele wala kipi kianze kabla ya kuongeza umahiri na umakini kwa vingine.Kurukiarukia vitu hovyo tu.
 
Na hizi ulizotumia ndizo hasa tabia na umburula wa wana-CCM mlivyo kiuhalisia wenu.Hamna vipaumbele wala kipi kianze kabla ya kuongeza umahiri na umakini kwa vingine.Kurukiarukia vitu hovyo tu.
Nchi siyo familia yako ndugu,katika nchi kila kitu kinatakiwa kwenda,hayo unayofikiri wewe ni management ya kifamilia 🌀
 
Tanzania wanapenda kujilinganisha na ujinga? Umeme hata south Africa tatizo lakini je uchumi wetu na wao sawa idadi ya viwanda vyao na vyetu sawa embu tuache ujinga bhn
 
Back
Top Bottom