Hali ya utaifa inatisha

Hali ya utaifa inatisha

Natamani mzee wangu urudi hapa usome hizi comments.
Binafsi natamani huyu kiumbe AFE hata leo

Sina namna nyingine ya kueleza machungu yangu dhidi ya uzalimu wa serikali hii, ni zaidi ya wakoloni

Kila mtu analia tumekuwa watumwa kwenye taifa letu.


Wafanyabiashara wanatekwa, wananyanyaswa na kufungiwa biashara

Wafanyakazi wanalia, wanatia huruma mno wanavyodhalilishwa kila siku na viongozi wa ccm ( juzi tu tumeshuhudia daktari akimpigia magoti kada wa ccm), wanatishwa kwenye vikao, walimu wanacharazwa viboko

Wakulima wamekosa pa kusemea mahindi mbaazi, choroko kunde hakuna pa kuuza vinaoza huko vijijini

Wanasiasa wanapigwa riasasi hadharani badala ya kufanya uchunguzi, mgonjwa anavuliwa ubunge

Wanahabari wanatekwa wanapigwa, wanabambikiwa kesi kwasababu wanasema ukweli

Mkuu wa nchi anapaswa kujua yeye sio Mungu, nchi haiendeshwi kwa visasi chuki, upendelo na double standards.

Huwezi ukawafukuza walimu wenye vyeti feki halafu ukamuatamia Bashite halafu unataka watu wakupende HOW?!
 
Mwasisi wa chuki hizi za kichama anajulikana na hili halitamuacha salama kamwe. Umoja wa kitaifa tuliokuwa nao kabla ya awamu ya tano kuingia Madarakani tumeshaupoteza na itatugharimu sana kuurejesha.
 
Sijui wengine wanaona kile kile ninachokiona mimi. Kama ni hivyo basi inatisha kwa kuwa sijawahi kuona hali hii ikijiri katika nchi yetu pendwa tangu ninakuwa mtu mzima miaka ile ya 1960s'. Katika historia ya taifa letu siku zote watanzania tumekuwa tunaunganika katika masuala yenye maslahi ya taifa. Lakini katika miaka ya hivi karibuni tunaanza kuona baadhi ya watu wakifurahia pale nchi yetu inapokuwa imeshikwa pabaya. Kwa mfano hivi sasa kuna hili suala la ndege yetu kuzuiliwa huko Afrika Kusini. Kuna watu wanashangilia. Kuna watu walishangilia pale IMF ilipotoa takwimu zake kuhusu kukua kwa uchumi kwa kuonyesha ukuaji wa 5% tofauti na takwimu za serikali zilizoonyesha ukuaji wa 7.1%. Hata kwenye mashindano ya Afcon yaliyoisha hivi karibuni huo Cairo kuna watu walioshangilia pale tulivyofungwa na Kenya! Kwa ufupi chochote kile kinachoonyesha Tanzania inafanya vibaya kinafanya baadhi ya watu wafanye sherehe. Kwa hakika hali hii haipendezi. Nini kimetokea hadi tukafika mahali watu wanafurahi nchi yao ikishikwa pabaya? Tutafakari na tufanye kile Waingereza wanasema "soul searching". Haipendezi tukiendelea hivi kama taifa.
Haya yote yaanzia juu kwa kuendekeza ukabila na ukanda almost kila sehemu. Nonsense
 
fanyeni kama Iran tumeni wanajeshi wateke ndege ya SA ngoma iwe droo
 
Kumbukizi ....nilijua shetani yuko state house ........nipale watu wa dini walipo jikusanya kutaka kuombea watu wa pinzani waliopata majanga kama lisu ...mbowe, matiku polisi wakawa wanakuja kuwaondoa nilishangaaa sana nakati mtu kama yule akiombewa lazima na mkulu na yeye angeombewa ......kwa kweli yamefanyika mengi kwanzia uongo,mauji ya raia wasiokua na watu kuzulumiwa haki zao hatakama ,ubabe usiokuwa walazima ,majibu ya shombo ,ukatili ambao mpaka leo kuna wanalipia gharama ya hivyo vitu vyote iwe kwa lawama,damu,mda ,uhai ......matokeo ndo hayo
 
I think serikali ya awamu hii imesababisha sana matabaka ya kisiasa, kila kitu ni politics sasa serikali iliomadarakani inapokandamiza vyama fulani au viongozi wa vyama fulani tegemea hata wafuasi wa hivo vyama ambao ni watanzania wataona wanakandamizwa......yani serikali ya sasahivi huo ndio u dhaifu wake
 
Kwenda kinyume na taifa lako ni dhambi kubwa, pinga viongozi na sio taifa.
 
Sijui wengine wanaona kile kile ninachokiona mimi. Kama ni hivyo basi inatisha kwa kuwa sijawahi kuona hali hii ikijiri katika nchi yetu pendwa tangu ninakuwa mtu mzima miaka ile ya 1960s'. Katika historia ya taifa letu siku zote watanzania tumekuwa tunaunganika katika masuala yenye maslahi ya taifa. Lakini katika miaka ya hivi karibuni tunaanza kuona baadhi ya watu wakifurahia pale nchi yetu inapokuwa imeshikwa pabaya. Kwa mfano hivi sasa kuna hili suala la ndege yetu kuzuiliwa huko Afrika Kusini. Kuna watu wanashangilia. Kuna watu walishangilia pale IMF ilipotoa takwimu zake kuhusu kukua kwa uchumi kwa kuonyesha ukuaji wa 5% tofauti na takwimu za serikali zilizoonyesha ukuaji wa 7.1%. Hata kwenye mashindano ya Afcon yaliyoisha hivi karibuni huo Cairo kuna watu walioshangilia pale tulivyofungwa na Kenya! Kwa ufupi chochote kile kinachoonyesha Tanzania inafanya vibaya kinafanya baadhi ya watu wafanye sherehe. Kwa hakika hali hii haipendezi. Nini kimetokea hadi tukafika mahali watu wanafurahi nchi yao ikishikwa pabaya? Tutafakari na tufanye kile Waingereza wanasema "soul searching". Haipendezi tukiendelea hivi kama taifa.

Yaani wewe unaona suala la ndege ndilo la kitaifa zaidi? Watu walibomolewa nyumba kimara, Akwilina aliuwawa, Azory alipotea na Lissu kupigwa risasi eneo la bunge. Haya yote watawala wetu na watu wnegine hawakuyaona ya kitaifa. Leo ndiyo mnataka suala la kushikiliwa ndege tuungane kitaifa!!. Upuuzi huo. Masuala ya uhai wa watu ni muhimu sana kuliko haya ya ndege kushikiliwa.
 
Mbona wakati tundu lissu kapigwa risasi, azory kupotea, ben saa nane n.k n.k hamkutuunga mkono tulivyokuwa tunalia kuulizia wapo wapi? ya kwenu mnataka tuwaunge mkono, ya kwetu ya utaifa hamuyaoni eheee
Utaifa kwemye maslahi yao mzee baba amewaita watendaji wa kata wote maana yake nn ccm ishinde kwa namna yoyote hell noo wacha na sisi tufurahie japo ili mkiuanza kutunyuka wakati wauchaguzi nyie mfurahi sisis tulie ila hatutakubali
 
..kuna waTz wanajiita wazalendo wanafurahia na kusherehekeakea wakiona wenzao wakitekwa, wakiteswa, wakibambikiwa kesi za hovyo-hovyo, na hata wakipigwa risasi.

Kinachoendelea nchi hii sio uzalendo ila ni unafiki. Je uzalendo gani wa kuwa na double standard kwenye maaumizi?

Cheti feki ni halali kwa Ngosha lakini kwa Mangi ni haramu!

CCM na vijana wao wanaruhusiwa kufanya mikutano ya hadhara na kuongea lolote na mpaka kutishia kuua, ACT wakifanya mkutano wa ndani wanakamatwa!

Tanzanite wanaruhusiwa kumwita mtu yoyote shoga au mwizi bila mahakama kuthibisha. Mwakyembe kimyaaaa! Ngoja Mwanahalisi aandike tena kwa kutumia neno tuhuma uone jinsi jinsi Wizara nzima ya Habari watakavyotoa matamko!

Hii ndo ila watani zangu wazaramo wanasema " Kusafiri asafiri Mwarabu, akisafiri Mzaramo kaenda ngomani"!
 
Sijui wengine wanaona kile kile ninachokiona mimi. Kama ni hivyo basi inatisha kwa kuwa sijawahi kuona hali hii ikijiri katika nchi yetu pendwa tangu ninakuwa mtu mzima miaka ile ya 1960s'. Katika historia ya taifa letu siku zote watanzania tumekuwa tunaunganika katika masuala yenye maslahi ya taifa. Lakini katika miaka ya hivi karibuni tunaanza kuona baadhi ya watu wakifurahia pale nchi yetu inapokuwa imeshikwa pabaya. Kwa mfano hivi sasa kuna hili suala la ndege yetu kuzuiliwa huko Afrika Kusini. Kuna watu wanashangilia. Kuna watu walishangilia pale IMF ilipotoa takwimu zake kuhusu kukua kwa uchumi kwa kuonyesha ukuaji wa 5% tofauti na takwimu za serikali zilizoonyesha ukuaji wa 7.1%. Hata kwenye mashindano ya Afcon yaliyoisha hivi karibuni huo Cairo kuna watu walioshangilia pale tulivyofungwa na Kenya! Kwa ufupi chochote kile kinachoonyesha Tanzania inafanya vibaya kinafanya baadhi ya watu wafanye sherehe. Kwa hakika hali hii haipendezi. Nini kimetokea hadi tukafika mahali watu wanafurahi nchi yao ikishikwa pabaya? Tutafakari na tufanye kile Waingereza wanasema "soul searching". Haipendezi tukiendelea hivi kama taifa.
Ccm ikifa nchi utarudi kuwa ma amani. Kwa sasa ccm Ni adui wa taifa hili.
Wameasisi Mambo mengi yanayoligawa taifa. Huwezi kuwa na vijana wa ccm wanaoomba ruhusa ya rais waue wapinzani halafu ukategemea umoja.
 
Uzalendo na utaifa ungeanzia kuanzia pale watz wenzetu wanavyotekwa na wengine kupigwa risasi.

Yani akimiminiwa mtu risasi 16 mwilini mnajifanya mko busy sana hamuwezi kukemea leo imekamatwa ndege ambayo hata haina roho mnataka tulie pamoja??
 
Sijui wengine wanaona kile kile ninachokiona mimi. Kama ni hivyo basi inatisha kwa kuwa sijawahi kuona hali hii ikijiri katika nchi yetu pendwa tangu ninakuwa mtu mzima miaka ile ya 1960s'. Katika historia ya taifa letu siku zote watanzania tumekuwa tunaunganika katika masuala yenye maslahi ya taifa. Lakini katika miaka ya hivi karibuni tunaanza kuona baadhi ya watu wakifurahia pale nchi yetu inapokuwa imeshikwa pabaya. Kwa mfano hivi sasa kuna hili suala la ndege yetu kuzuiliwa huko Afrika Kusini. Kuna watu wanashangilia. Kuna watu walishangilia pale IMF ilipotoa takwimu zake kuhusu kukua kwa uchumi kwa kuonyesha ukuaji wa 5% tofauti na takwimu za serikali zilizoonyesha ukuaji wa 7.1%. Hata kwenye mashindano ya Afcon yaliyoisha hivi karibuni huo Cairo kuna watu walioshangilia pale tulivyofungwa na Kenya! Kwa ufupi chochote kile kinachoonyesha Tanzania inafanya vibaya kinafanya baadhi ya watu wafanye sherehe. Kwa hakika hali hii haipendezi. Nini kimetokea hadi tukafika mahali watu wanafurahi nchi yao ikishikwa pabaya? Tutafakari na tufanye kile Waingereza wanasema "soul searching". Haipendezi tukiendelea hivi kama taifa.
Tatizo lilianza kwa bashite
 
Watu wanauchukia utawala na sio ndege, , , viongozi wajitathimini wanavyo endesha nchi
 
Back
Top Bottom